Magufuli alikuwa sahihi kutokuongeza mishahara ya watumishi kwa miaka 5. Uzembe umejaa makazini

CCM inawapenda sana mijitu mijinga mijinga kama wewe.

Mna rundo la mat
CCM inawapenda sana mijitu mijinga mijinga kama wewe.

Yaani unakuta jitu lina rundo la matatizo ila halijui nani chanzo cha matatizo yake.

Unadhani ukiongelea suala la udogo wa mishahara hao PSSF hata wanakuelewa.

Hayo ni mashirika ya Umma mishahara yao ma posho posho wanajipangia wenyewe kupitia BODI YA WAKURUGENZI.

Hakuna mwenyewe mshahara mdogo huko.

Tunapoongelea mishahara panya tunazungumzia watumishi wa kawaida kama wa serikali kuu, halmashauri na njaa wengine.

Kwanza huko kwenye mashirika hakuna Mtoto wa kajamba nani.

Ishtoshe pia, suala la kukngeza mishahara siyo la takataka fulani ikijisikia kwasababu pesa siyo zake ni za walipakodi wa nchi hii.

Kama wao wenyewe wamashindwa kuweka mifumo ya uwajibikaji, hiyo siyo sababu ya kuwanyima watu haki zao.
 
mkuu hapa umeingia cha kike, uwajibikaji wa miaka 5 hii ni bora zaidi mara mia ya awamu ilopita hivo haki za wafanya kazi zimepuuzwa pasina sababu ya msingi
 

Unamshitaki Magufuli kwa wananchi kuwa ameshindwa kuwasimamia hao watumishi kwa miaka yote mitano aliyofanya nao kazi
 
Hasa watu walioajiriwa upande wa IT serikalini, shida sana
Kwa upande wa maIT sikupingi kabisa..yani ni wazembe na wavivu hatari..halafu cha kushangaza wengi walikua walimu wamejiupdate vikozi vya IT leo ndo wanao endesha masuala yote ya IT..hawa jamaa ni total disaster kama ulivyosema mleta uzi.

Badilikeni ma IT wa utumishi wa umma mna tudharirisha.

#MaendeleoHayanaChama

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Hayo no matokeo ya kukosa hamasa,kutowapatia stahiki sii dawa ya kuongeza ufanisi.Bali yaweza kuwa ni dawa ya kupunguza ufanisi.Hamasa ni Jambo dogo sana, hats ahdi na lugha mzuri ingetosha kuwapa Ari ya kufanya kazi kwa weledi zaidi. Kamwe vitisho na manyanyaso Yana haribu badala ya kujenga.
 
Uzembe kazini ni hulka ya baadhi ya watu
Ingawa hapa ni wengi sana lakini hata wanaokula mishahara minono bado ndio wazembe wa kutupa
 
Huo uchumi wa kati umeletwa na yeye mwenyewe kufanya kazi office zote nchini peke yake?
 
Hiyo mifuko pssf na nssf huyohuyo mh. Rais ndiyo aliyoifilisi.

Shida yako ni kushindwa kulitambua hilo.

Kwa nje mh. Rais anasema na kutoa ahadi kufurahisha watu lakini mifuko kaifilisi yeye na haina hela na hivyo na kusababisha watumishi wawazungushe wastaafu.

Hio sio shida ya watumishi wa mifuko ni shida ya Rais

Mfano, aliposema wastaafu walipwe kwa kikokotoo cha zamani mpaka 2024, unadhani ni kweli wanalipwa 50% ya zamani?
 
Ni kweli mimi naomba sana asipandishe kabisaa mishahara kwa sababu kiuchumi huitaji mshahara mkubwa bali unachohitaji ni pesa yenye thamani nchi za watu walishasahau kupandisha mishahara wanachofanya ni kuboresha huduma za jamii na kuongeza thamani ya pesa maana ukiongeza mshahara hasara ni kubwa kuliko faida maana pesa inashuka thamani na bidhaa zinapanda bei kwa hyo magu asipandishe.mishahara ila utafute mgawanyo sawa kulingana na viwango vya elimu na ukubwa wa kazi pia huduma za jamii ziboreshwe kama zinavoboreshwa sasa umeme maji barabara zisiwe tatizo ifike wkt laki 5 unanunua gari hapo pesa inathamani zimbabwe walipandisha mishahara hadi pesa ikapotea thamani yake.... Magu ndio kiongozi sahihi maana anachafanya anacho amini kina manufaa sio kusikiliza kelele za watu ili wakushangilie asikudanganye mtu tunataka pesa yenye thamani ili tununue vitu vingi zaid...
 
Muongezewe mishahara kwani mmeongezewa kazi? Anyway, huo ni uzembe hasa
 
Kuna mambo ukiyaangali unajisemea kimoyo moyo " acha tu Magufuli aendelee"
Kuna shithole zimekaa kwenye ofisi za umma hasa NIDA, police na uhamiaji vitambi vimejaa kinyesi, tija Ni zero halafu wanalalamika wasipopandishiwa mishahara
Hao ni wazembe pia wana uhakika wamepata kazi za kudumu ndio maana wamebweteka.
 
Madhara yake ndiyo hayo. Wafanyakazi wote hawatamchagua.!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…