Magufuli atengua uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, F. Mramba. Amteua Dkt. Mwinuka kukaimu

Magufuli atengua uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, F. Mramba. Amteua Dkt. Mwinuka kukaimu

kwanza wapunguze expenses
-wafanyakazi wanapewa units za bure kila mwezi,zipunguzwe
-haiwezekani kulipana bonus kwa hali iliyonayo shirika
-deal na umeme unaopotea njiani
-wapiga dili km iptl awatafutie mwarobaini akishauriana na AG office
Let us wait and see huyo anayekuja kama atayafanya hayo. Na impact say ya kuondoa units za bure ni ipi?
 
Wewe punguani kweli kuna mjadala gani sasa hapo wewe na waziri wa nishati pamoja na rais nani anaijua Tanesco.

Nimekujibu hivyo kutokana na wewe kijiona una uwezo wa kujadili kila kitu na kuwajibu wenzako kwa kejeli.

Rais kafuta mpango wa Tanesco kupandisha umeme wewe endelea kuandika gazeti lako.

Kwa hiyo wewe mwenye uwezo wa kujadili ulitaka bei ya umeme ipande.
Mkuu, hako ka kofia ka Merry Christmas kwenye avatar yako kameipendezea kweli! Sema "Haleluya"
 
wapate faida kwanza ndio wajipe umeme bure...

ila kupandisha mabei ovyo ndio source ya kutumbuliwa...

nitajie kampuni au shirika lolote duniani linalogawa huduma bure kipindi ambapo linapata hasara...

only in tanzania
i/Hili ni shirika la Serikali linapata ruzuku.

ii/Wafanyakazi/Waajiriwa wapo wangapi nchi nzima?ambapo wanasababisha hasara.

iii/Mashirika na Taasisi nyingi kama sio zote zinatoa huduma yake karibu na bure kwa Waajiri wake.

iv/Serikali kuu ndio iliyosababisha matatizo haya yote kwa kuingilia utendaji na kutoa maelekezo yanayoleta sintofahamu kwa shirika hili bila kujali ushauri wa wataalamu na matokeo tarajiwa.

v/Serikali haitaki kuleta utaratibu wa kampuni binafsi kuzalisha na kusambaza umeme huku wakifahamu fika Shirika hili haliwezeshwi ipasavyo kuendana na maendeleo endelevu.

vi/Kwanini Serikali inashindwa kumiliki vitalu vya gesi vitakavyopewa shirika hili na kutoa tenda kwa kampuni za uchimbaji na uchakatishaji wa gesi na wakimaliza tu wanakabidhi mradi na TANESCO wamiliki kwa 100%?

Utumbuaji huu hauna faida wala mantiki yoyote kwa kuwa bado utendaji na utaratibu unabaki kuwa ule ule uliotupelekea kufika hapa tulipo, hizi gharama zitapanda kama kawaida. Tusubiri tu.
 
Hivi vyeo vya kupewa shida sana, Jana kila mtu akikuona kazini anakunyenyekea kesho mpaka mfagizi wa ofisi anakudharau
 
kamua baba kamua namba bado hutujaisoma vema weka za kirumi na kigiriki kuna wengine hizi za kiarabu wanajifanya hawazijui kanyaga twende .
 
Huyu alikuwa mmoja wa watu waadilifu kwenye hii nchi. Na uchafu wa wakina muhongo nashangaa hawa watendaji wanawezaje kufanya kazi
hakuna md aliyeimudu tanesco kama mramba wakati utasema
 
Wewe punguani kweli kuna mjadala gani sasa hapo wewe na waziri wa nishati pamoja na rais nani anaijua Tanesco.

Nimekujibu hivyo kutokana na wewe kijiona una uwezo wa kujadili kila kitu na kuwajibu wenzako kwa kejeli.

Rais kafuta mpango wa Tanesco kupandisha umeme wewe endelea kuandika gazeti lako.
Ukweli mchungu-Tanesco ilihujumiwa na CCM 1993/1994, ndani ya ofisi za CCM Lumumba, Wala sio Serikalini/Wizarani. Kuanzia hapo likawa ni shamba la bibi la viongozi wa CCM kuvuna. Mkaanza ficha ficha kwa ruzuku etc lakini wapi. Sasa mnamtafuta mchawi maana maji yamewafika shingoni na mnalaghai wananchi eti mnawatetea kumbe ni nyie nyie mliowaangamiza katika suala la umeme.

Danganyeni wengine, wale wa utafiti wa matatizo ya akili, the 25% of the population na naona hata humu mnawapata kweli kweli. Lakini ukweli una tabia moja - haujifichi!
 
umeme ni shida katika Nchi hii badala kushughulika kuondoa Tatizo la umeme kukatika katika . Kweli serikali hii viongozi lazima wawe na uoga Kwa kufanya maamuzi. Sijajua maamuzi ya kupandisha bei yamefanywa na mkurugezi pekee yake mpaka uteuzi kutenguliwa.
bodi umehusika wizara inajua na hata waziri anajua toka mwanzo siasa ni tatizo jamaa wanatafuta kick
 
Leo 1.1.2017 Prof. Muhongo amehojiwa na Radio One na kueleza sababu za kusitisha mpango wa EWURA wa kupandisha bei ya Umeme kwa 8.5% kama ifuatavyo: -
1. Kwenye mikutano ya 'public hearing' nchini kote wadau walipinga myongeza ya bei;
2. hadi jana 31.12.2017 EWURA, kinyume na matakwa ya sheria, haikuwa imepeleka ripoti ya uamuzi wake kwa waziri mwenye dhamana, kujadiliwa na kupitishwa/kuthibitishwa kabla ya kutangazwa kwa pendekezo la bei mpya;
3. Ufumbuzi wa matatizo ya kifedha (madeni) wa TANESCO hauwezi utatuliwa kwa kupandisha bei ya Umeme. TANESCO inatakiwa kuwa na mkakati wa ku-improve efficiency kwenye management yake badala ya kuongeza bei ya Umeme; na
4. Wakuu wa TANESCO hawawpaswi kulipana bonus kila mwisho wa mwaka kiasi cha kufikia Tzs. 60m/- kwa mtu mmoja wakati shirika linashindwa kujiendesha isipokuwa kwa kupandisha bei ya Umeme. Hii inamaanisha kuwa wananchi wakamuliwe ili ipatikane pesa ya mabosi wa TANESCO kulipana bonus! Prof. Muhongo amesema ameagiza hata hiyo bonus isilipwe au irudishwe kwa waliokwisha kulipwa.

Kuliko hizo bonus za wakuu wa Tanesco,kinachoila zaidi na TANESCO ni mikataba mibovu ambayo hao viongozi wa TANESCO hawana mamlaka nayo.

Ukitaka upunguze matumizi ya TANESCO ni lazima uvunje mikataba ya IPTL na mingineyo ambayo Waziri hawezi kuizungumzia. Hiyo mikataba ndio inayoiumiza TANESCO na wala sio mishahara wala posho.
 
Siungi mkono utumbuaji.


Still bado Tanesco na idara ya maji Kuna uozo mkubwa. Gharama tunazolipa aziendani na huduma tunazopata
 
Safii sana , amtumbue na DG wa EWURA
Dah... Siyo EWURA.... ni EURA....hawa ishu ya maji waliachana nayo kitambo sana.... hailipi...wao wanadili na umeme, mafuta na gesi... ndiyo kunamshiko..[emoji13] [emoji13]
 
Ukabila ktk ubora wake ndg. Mramba anatokea wapi?
Mramba fala tu, kwann uombe kupandisha bei badala ya kuomba kushusha ili kuwapa nafuu watanzania? Isitoshe Tanesco hupatiwa ruzuku na serikali, bora angeomba ruzuku iondolewe ndo apandishe bei.
 
Ebana eeee,,,,maamuzi yako yanakuponza walizoea zamani kupandishapandisha tuu bei ya umeme sasa mhhhhh hatar sana
 
Back
Top Bottom