Zanzibar-ASP
JF-Expert Member
- Nov 28, 2013
- 11,550
- 40,697
Mgombea urais wa CCM John Magufuli hana historia yoyote katika maisha yake hususani toka awe mwanasiasa ya kujihusisha na mambo ya sanaa, burudani na michezo.
Hakuna kumbukumbu zozote kzinazomuonyesha John Magufuli akishiriki matukio muhimu ya sanaa na burudani hususani mchezo wa soka, Muziki nk.
Hana tofauti kubwa sana Benjamin Mkapa ambaye kipindi cha uongozi wake suala la michezo halikuwa kipaumbele chake kabisa, na hata Mkapa mara kadhaa alipohojiwa kuhusu nini anachofahamu na kilichokuwa kinaendelea katika mchezo wa soka nchini alisema hajui chochote zaidi ya kusikia mizozo na migogoro tu. Pamoja na yote hayo bado Mkapa aliacha kumbukumbu kubwa katika michezo kwa kuwezesha kujengwa kwa uwanja mpya wa kisasa wa Taifa.
Hali hii ya Magufuli ni tofauti kabisa na Mtangulizi wake, Jakaya Kikwete ambaye alikuwa ni kinara katika kujihusisha na mambo ya burudani na michezo kabla ya kuteuliwa na CCM Kugombea urais na hata baada ya kushinda urais, jambo ambalo Mzee Ally Hassan Mwinyi pia alikuwa akilifanya.
Hili la Magufuli limejidhihirisha wazi hivi karibuni baada ya Magufuli kuwasili mjini Zanzibar na kuulizwa na waandishi wa habari kuhusu ushabiki wake katika mchezo wa soka na hapo alijibu kuwa hana timu yoyote anayoishabikia zaidi labda ataishabikia Timu ya Taifa ya Tanzania.
Yote kwa yote Magufuli siku ya jana alialikwa na TFF kwenda uwanja wa taifa kufungua mashindano ya Kombe la Kagame, lakini pasipo kutegemea Magufuli hakudhuria katika ufunguzi huo tena bila kutoa taarifa kwa TFF waliomualika na badala yake aliendelea na ratiba ya shughuri zake za kisiasa mkoani Mwanza.
Huenda huu ukawa mwanzo mgumu kwa sekta ya michezo na tasnia ya sanaa nchini ambayo ilishaanza kuzoea na kubweteka kuwa wao ni watu muhimu na wa thamani sana kwa kuwa rais anayeondoka madarakani Jakaya Kikwete alikuwa karibu nao sana lakini mategemeo kwa mtu anayetaka kuchukua nafasi ya Kikwete hana muda kabisa na michezo na burudani.
Hakuna kumbukumbu zozote kzinazomuonyesha John Magufuli akishiriki matukio muhimu ya sanaa na burudani hususani mchezo wa soka, Muziki nk.
Hana tofauti kubwa sana Benjamin Mkapa ambaye kipindi cha uongozi wake suala la michezo halikuwa kipaumbele chake kabisa, na hata Mkapa mara kadhaa alipohojiwa kuhusu nini anachofahamu na kilichokuwa kinaendelea katika mchezo wa soka nchini alisema hajui chochote zaidi ya kusikia mizozo na migogoro tu. Pamoja na yote hayo bado Mkapa aliacha kumbukumbu kubwa katika michezo kwa kuwezesha kujengwa kwa uwanja mpya wa kisasa wa Taifa.
Hali hii ya Magufuli ni tofauti kabisa na Mtangulizi wake, Jakaya Kikwete ambaye alikuwa ni kinara katika kujihusisha na mambo ya burudani na michezo kabla ya kuteuliwa na CCM Kugombea urais na hata baada ya kushinda urais, jambo ambalo Mzee Ally Hassan Mwinyi pia alikuwa akilifanya.
Hili la Magufuli limejidhihirisha wazi hivi karibuni baada ya Magufuli kuwasili mjini Zanzibar na kuulizwa na waandishi wa habari kuhusu ushabiki wake katika mchezo wa soka na hapo alijibu kuwa hana timu yoyote anayoishabikia zaidi labda ataishabikia Timu ya Taifa ya Tanzania.
Yote kwa yote Magufuli siku ya jana alialikwa na TFF kwenda uwanja wa taifa kufungua mashindano ya Kombe la Kagame, lakini pasipo kutegemea Magufuli hakudhuria katika ufunguzi huo tena bila kutoa taarifa kwa TFF waliomualika na badala yake aliendelea na ratiba ya shughuri zake za kisiasa mkoani Mwanza.
Huenda huu ukawa mwanzo mgumu kwa sekta ya michezo na tasnia ya sanaa nchini ambayo ilishaanza kuzoea na kubweteka kuwa wao ni watu muhimu na wa thamani sana kwa kuwa rais anayeondoka madarakani Jakaya Kikwete alikuwa karibu nao sana lakini mategemeo kwa mtu anayetaka kuchukua nafasi ya Kikwete hana muda kabisa na michezo na burudani.