Magufuli hayupo kipi kinawafanya CHADEMA kuliachia hewani suala la Wabunge 19 wa Viti Maalum?

Hatuwalaum,swali letu kwao ni kwamba wao kama chama wameshakata tamaa tayar juu ya suala Hilo?

This is outcast question...

Unasahau kuwa kila upande ktk jambo hili una wajibu wake wa kisheria na kikatiba wa kutekeleza/kutenda...

Sasa kama CHADEMA wao wamekwisha kufanya wajibu wao, unataka waende na bungeni kulisaidia bunge kufanya wajibu wake...?

Kama ni ishu ya kupush na kutia pressure ili sheria na katiba ifuatwe, ni kwa vipi tena jukumu hilo liwe la CHADEMA peke yake...?
Jukumu la kuilinda katiba ni la kila mmoja wetu...

As far as I know, CHADEMA pamoja na kuwa wao wameshatekeleza wajibu wao wa kisheria na kikatiba juu ya swala la wabunge hawa 19 walio bungeni kinyume cha katiba...

....Lakini bado CHADEMA wanapiga kelele kwa mhimili wa bunge kutofanya wajibu wake wa kikatiba wakisaidiwa na wananchi wenye mapenzi mema na nchi hii kama sisi huku nje ili kulinda katiba...

Katika hili unalaumu na kunyoshea kidole watu wasio na kosa kikatiba unless uwe unafanya kwa maslahi yako ya siasa maji taka. Katika hili elekeza lawama mahali sahihi, kwa taasisi ya bunge...
 
Waende mahakamani wakaiombe mahakama itoe tafsiri ya mambo yatakayotokea yatakayomfanya mbunge kupoteza ubunge wake kwa mujibu wa katiba ya nchi iliyopo, watapata ushindi asubuhi tu mana COVID-19 sio wanachama wao, walishawafukuza.

Vyema,ni kusema kwamba chadema pamoja na weledi wa watu waliokuwa nao,wameshindwa kuliona hilo?
 

Na kwa nn wasijaribu Tena option ya mahakaman?

Au hawana iman nayo moja kwa moja hata baada ya mwendazake kwenda zake??
 
Not exactly,je tuwaulize njia waliyotumia haijaleta positive outcomes,wamekata tamaa??kodi yetu inatumiwa vibaya kwa mgongo wa chama Chao sasa
Kodi zetu wananchi ndio zinachezewa na sio kodi za Chadema, wao walishafanya njia zao ila jobo kawakumbatia..... nadhani sasa lingekua ni swala la wananchi wote.
 
Kodi zetu wananchi ndio zinachezewa na sio kodi za Chadema, wao walishafanya njia zao ila jobo kawakumbatia..... nadhani sasa lingekua ni swala la wananchi wote.

Chadema,wamejaribu kwa kias Cha kutosha kulileta hili suala kwa wananchi?
 
Shida waliweza kujificha kwenye kichaka cha Magufuli na sasa Magufuli is dead and gone watamwimbie wanaogopa nini kama wao ni wana mabadiliko?
Jobo katunisha misuli kuwakumbatia...
 
Chadema,wamejaribu kwa kias Cha kutosha kulileta hili suala kwa wananchi?
Chama kimeplay part yake vema tu, wamevuliwa uanachama, wamemuandikia spika barua...ila majibu ya spika tunayajua na yupo bega kwa bega na covid anawalinda kwa nguvu zote.....

Hadi hapo ilipaswa kuwa kwa wananchi, ila wananchi wenyewe ndio sisi waoga kuliko hata uoga wenyewe, harakati zetu kwenye mitandao tu tena kwenye fake IDs 😁
 
Wewe mwenyewe umeandika ukakasi swala la covid si Kamati Kuu ilishawavua uanachama unataka nini tena
 
Mbowe ambaye baba yake alikuwa sehemu ya mfumo enzi za JKN ni vigumu kuamini kwamba yeye na CCM sio kitu kimoja. Naamini hawa wanasiasa wanaovuka kutoka CDM na kuingia CCM ni wale wale tu ambao mfumo unawaandaa kuanzia sekondari na wachache kuanzia shule ya msingi.

Wakati unakuwa umefika wa kurudi 'nyumbani' na wanakuwa wamepitia njia ya Freeman ambayo ni maarufu na yenye kukubaliwa na mfumo uliopo. Siasa ni za kuzielewa vyema ili zisije siku moja zikakuumiza kichwa.
 
Bila kitendo alichofanya Ndungai hata mana asingekuwepo hapo alipo.
 
Mkuu sasa wewe unataka Chadema wafanye nini tena?
Wao wameshakaa kamati kuu na kuwavua uanachama hao wakina dada na wakinamama kwa hayo makosa yao waliyofanya na wameshamtaarifu spika kupitia utaratibu rasmi wa barua japokuwa naibu spika alijaribu kukana ofisi ya spika kupokea hiyo barua lakini baadae spika akathibitisha kuipokea lakini akaiita ni kipeperushi na akadai apewe na nyaraka zingine sijui mihutasari ya kikao cha kamati kuu nk. alimradi tu kuwasumbua chadema na kutaka kuwakumbatia hao wasaliti na ni vitu ambavyo havikuwa vikidaiwa wakati wa nyuma inapotokea mbunge kufukuzwa kwenye chama... Barua rasmi na iliyothibitishwa kutoka kwa katibu mkuu ilikuwa inatosha na spika alikuwa akichukua hatua mara moja!! Hii issue inabaki bungeni kwa spika mwenyewe kama ameamua kuwakingia kifua ni sawa tu tatizo si la chadema tena wao wameshamaliza.
Ulitaka Mbowe au Chadema waanzishe maandamano nchi nzima kushinikiza hao Covid-19 waondolewe bungeni?? Ya nini kupoteza muda na nguvu kwa sababu ya ujinga kama huo? Mi naona Hakuna sababu kabisa., wao wamemaliza.
 
Vyema,ni kusema kwamba chadema pamoja na weledi wa watu waliokuwa nao,wameshindwa kuliona hilo?
Ruzuku ndio imewapofua macho wamejifanya hawajaliona hilo, mana wanajua kuwatimua hao covid-19 bungeni ni kupunguza ruzuku inayoingia chamani.
 
Waende mahakamani wakaiombe mahakama itoe tafsiri ya mambo yatakayotokea yatakayomfanya mbunge kupoteza ubunge wake kwa mujibu wa katiba ya nchi iliyopo, watapata ushindi asubuhi tu mana COVID-19 sio wanachama wao, walishawafukuza.
Here is the problem again...

Kwanini CHADEMA ndiyo waende? Kwanini tusiwe sisi wananchi? Kwanini usiwe wewe?

Hivi Katiba ya JMT ni ya CHADEMA au ni wananchi wote?

Kama inavunjwa nani mwenye wajibu wa kuzuia isivunjwe? CHADEMA au kila raia halali wa Tanzania..?

CHADEMA ni taasisi iliyopo hapo kwa mujibu wa sheria na katiba. Inatekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria na katiba ya nchi...

Wao wameshamalizana na hao watu kwa mujibu wa sheria na katiba. Yupo mwingine anayepaswa kukamilisha machakato huu wa kikatiba.....BUNGE

Pigeni kelele kuelekea huko..

NB: On the other hand, CHADEMA wanaweza kwenda mahakamani kwa jambo moja tu kwa sasa. Kwa kinamama hawa kutumia IDENTITY ya CHADEMA kufanya shughuli zao za kibunge ikiwemo kujinasibisha na chama ambacho sio wanachama kwa mujibu wa sheria...
 
Kuna issue ya kuitisha Baraza Kuu ili “kubariki” maamuzi yale, kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA. Nadhani ni moja ya wajibu pia.

Need to tie up all loose ends…
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…