Magufuli hayupo kipi kinawafanya CHADEMA kuliachia hewani suala la Wabunge 19 wa Viti Maalum?

Here is the problem again...

Kwanini CHADEMA ndiyo waende? Kwanini tusiwe sisi wananchi? Kwanini usiwe wewe?Hivi Katiba ya JMT ni ya CHADEMA au ni wananchi wote?
Tulishindwa kutoka nje wakati uchaguzi wote unaporwa Nov 2020 unadhani watu watakuwa na morale ya kutoka sasa hivi kwenda kudemand hii kitu?

Sijui hata ile movement ya BAWACHA kwenda Bungeni kumchomoa Halima iliishia wapi?
 
Na kwa nn wasijaribu Tena option ya mahakaman?

Au hawana iman nayo moja kwa moja hata baada ya mwendazake kwenda zake??

1. Mahakamani CHADEMA kama wao waende kufanya nini labda? Kuliomba Bunge liwaondoe hao kinamama hao kwa sababu si wanachama wao tena? Kwa vipi hili liwe jukumu la CHADEMA?

2. Jambo hili ni la kikatiba. Na kumbuka katiba imeweka wajibu wa kila taasisi na vile vile wananchi (mimi na wewe)

3. Katiba iweka utaratibu (chain of command) wa kushughulika na jambo/case moja ili iwe imeshughulikiwa ipasavyo na kwa ukamilifu wake kikatiba..

4. Katiba imesema ili mtu akose sifa ya kuwa mbunge, moja ya sababu ni kutokuwa mwanachama wa chama cha siasa kilichosajiliwa kisheria...

5. Katika chain of command kwa jambo hili, CHADEMA wamewafuta uanachama kinamama hawa. Kikatiba na kisheria, si wabunge tena...

6. Sasa unaweza kupata picha chain of command imekatikia wapi ili kuukamilisha mchakato wa kikatiba...

7. Honestly, ktk ishu hii wanaopaswa kwenda mahakamani si CHADEMA bali ni;

å Mwananchi yeyote au wote kwa pamoja ili kuitetea katiba kwa sababu ktk kesi hii, kuna kwa makusudi au kutojua anaikanyaga katiba

å Hawa kinamama 19 ili watetee uanachama and subsequently ubunge wao iwapo wanadhani wameonewa kufutwa uanachama wao na CHADEMA...

8. Absolutely, kwa ishu ya uanachama wa Halima Mdee na wenzake 18, CHADEMA wametimiza wajibu wao wa kisheria na kikatiba 100% bila kujali wamewafuta uanachama kwa haki au kuwaonea...

9. CHADEMA wanaweza kwenda mahakamani kwa jambo jingine. Hili ni la hawa kinamama 19 kuendelea kufanya shughuli zao wanazoziita "za kibunge" ndani na nje ya bunge kwa kutumia "POLITICAL PARTY IDENTITY" ya CHADEMA huku ukweli ukiwa siyo. Kamwe CHADEMA hawawezi kwenda mahakamani eti kulishitaka bunge na Spika Ndugai kwanini hawajawaondoa hawa kinamama bungeni....!!

Kama ni kwenda mahakamani ili kuomba tafsiri ya kikatiba juu ya ubunge wa hawa kinamama, pia napata shida kuelewa, kuwa, waombe tafsiri gani huku mchakato wa kushughulikia kesi hii ikiwa imekwamishwa na taasisi ya bunge kwa kushindwa kutenda wajibu wake wa kikatiba...?
 
Kwa hili shehe hata nami nimejikuta najiuliza sana..... nini kimewasibu Chadema?
Walianza vizuri very aggressively lakini naona hii miezi ya karibuni wamepoa sana. Why?

John Mnyika Chadema Diaspora
 
Kwa nini Chadema wasifungue kesi ya kikatiba?
 
tuliwaambia mkulima amefariki,nyani wakashangilia lakini muda ulipokwenda wanagundua kumbe ndiyo alikuwa analima mahindi wao wanakula.

kwa sasa utasimama wapi,ukiwa na nani,unafanya nini ili tu watu wakusikilize kisha uanzishe mada ya kuwatoa bungeni wabunge 19 waliofukuzwa uanachama chadema!!!
ukweli ni kwamba hutasikilizwa hata na unaotaka kuwaelezea,achana na unaotaka watekeleze hilo.

chadema ina agenda nyingi mno katika mikakati yake,lakini tatizo ni kuruhusu kila mtu aamue kuwa mwanaharakati ndani ya chama.leo hii kuna watu hawaitaki chadema ila wanampenda lissu,kuna watu hawamtaki mbowe ila wanaipenda chadema,kuna watu wanapenda itikadi za chadema ila sio watu waliomo kwenye uongozi wa chama nk.
nadhani tungeruhusu hatma ya chama iwe mikononi mwa mbowe pekee,swala la covid kukosa uanachama lisingekuwepo.na chama kingekuwa na nguvu sana by now tunavyoongea.

but so sad,chadema imekuwa sikitu.
 
Kuna issue ya kuitisha Baraza Kuu ili “kubariki” maamuzi yale, kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA. Nadhani ni moja ya wajibu pia.

Need to tie up all loose ends…
å Huu siyo wajibu wetu kujua kama taratibu za kuwafutia uachama zimefuatwa kwa mujibu katiba yao au la. Na wala si wajibu wa Spika Ndugai na bunge lake. Huu ni wajibu wa mwanachama mwenyewe kutetea uanachama wake kwa kufuata taratibu zinazokubalika kisheria ikiwemo kwenda mahakamani kama taratibu za kichama hazimpi haki...

å CHADEMA publicly wamesha tangaza kwa umma kuwa hawa si wanachama wao tena na kuzitaarifu mamlaka na taasisi zote za kikatiba zinazofanya kazi na kinamama hawa kwa jina la "WABUNGE WA CHADEMA - VITI MAALUMU"

å Inashangaza kwamba, eti taasisi hizi zinapinga maamuzi halali ya taasisi halali kisheria nje ya utaratibu wa kisheria. It's absolutely absurd...

å Kwa hiyo, wanaopaswa kupinga maamuzi ya chama ni kina Halima na wenzake 18 walioathirika na maamuzi ya chama chao. Kama wanaona wameonewa na hawapati haki yao ndani ya taratibu za kichama kwa mujibu wa katiba yao, ipo mahakama na itataka yote haya uliyoandika hapa...

å Kama mahakama itaona utaratibu wa kuwafuta uanachama kwa mujibu wa katiba yao haukufuatwa kikamilifu, basi itatoa maelekezo ya kufuatwa ili kuhalalisha uamuzi wao kisheria na kwa maana hiyo kina Halima watarudishiwa haki yao ya uanachama na ubunge automatically....

å Kinachofanyika sasa ndani ya bunge na nje huku ni siasa tu za kuisigina na kuinajisi katiba na taratibu zetu za za nchi za kulinda haki ya kila mtu...
 
Unadhani haya yako CHADEMA tu...?

Bila tofauti ya mitazamo na misukosuko ndani ya chama cha siasa, basi elewa kuwa hakuna chama hapo...

Hata ndani ya familia nyingi migawanyiko kama hii ipo. Mathalani ktk familia ya Mzee Isaka (kwenye Biblia), Baba Mzee Isaka, mtoto wake kipenzi alikuwa Essau lakini mama (Rebecca) mtoto wake kipenzi alikuwa Yakobo (Israel)...

Nadhani, ishu hapa ni kwa namna gani kunapotokea mgogoro mnakaa chini na ku resolve tofauti zenu....

Honestly, miongoni wa taasisi [vyama vya siasa imara], hakika ktk miongo mitatu hii mpaka sasa, CHADEMA yaweza kuwa ni number one despite misukosuko yote iliyopitia toka kwa Mkapa, Kikwete na kisha kwa huyu aliyekuwa hatari na balaa zaidi - Mwendazake Magufuli...
 
Waende mahakamani wakaiombe mahakama itoe tafsiri ya mambo yatakayotokea yatakayomfanya mbunge kupoteza ubunge wake kwa mujibu wa katiba ya nchi iliyopo, watapata ushindi asubuhi tu mana COVID-19 sio wanachama wao, walishawafukuza.
Hilo Sio chadema tu hata wewe waweza kwenda...
 
kwamba baada ya magufuli bado chadema iko imara!!!!

guys!!!
 
Tulishindwa kutoka nje wakati uchaguzi wote unaporwa Nov 2020 unadhani watu watakuwa na morale ya kutoka sasa hivi kwenda kudemand hii kitu?

Sijui hata ile movement ya BAWACHA kwenda Bungeni kumchomoa Halima iliishia wapi?
Woga wa kutenda hakuondoi wajibu wako au wa mtu/watu mwingine wa kutenda...

Na kumbuka "woga" ni temporal situation. Unaweza kuingiwa na woga sasa, lakini ktk swala hilohilo kesho ukawa na ujasiri wa kulitenda...
 
kwamba baada ya magufuli bado chadema iko imara!!!!

guys!!!
Absolutely, YES..

Unashangaa hili kwa sababu wewe unajadili siasa mitandaoni tu na kusikia tu wengine wanasemaje. Kwa hiyo wewe ukiletewa mashudu, unakula tu...

Walioko ndani na kufanya siasa practically wanalijua...

Kwa taarifa yako hata kifo cha mwendazake Magufuli, the main cause ni pressure ya CHADEMA akiwa anadhani akiifuta CHADEMA eti atatawala nchi hii milele bila pressure...

Mwisho wa siku ikawaje?

Kwa shinikizo la nia yake ovu ukapelekea kuharibika kwa afya yake ya akili na kuanza kutenda mambo kikatili na mwisho wa siku akafa yeye na kuwaaacha aliokuwa anawapiga vita ili wafe....!!!

Jiongeze ili ujifunze kuelewa mambo. Usisikie tu, ukaamini na kutenda. Utapotea...!!
 
bado unaandika vitu vya ajabu mkuu.kwamba magufuli ameuawa kwa pressure ya cahdema[emoji16][emoji16].

eh!!!
 
bado unaandika vitu vya ajabu mkuu.kwamba magufuli ameuawa kwa pressure ya cahdema[emoji16][emoji16].

eh!!!

I thought ni Covid 19 Mkuu,

Hata Mimi sijaelewa,Ila ulimsoma kwa makin jamaa ana hoja yule
 
I thought ni Covid 19 Mkuu,

Hata Mimi sijaelewa,Ila ulimsoma kwa makin jamaa ana hoja yule
hata sio covid pia.
hoja yake niliiona ndio sababu nikamuuliza kama ananaanisha kweli kusema hata baada ya kifo cha jpm bado cdm iko imara.
 
THE BIG SHOW umesahau kuweka maoni yako unashauri nini Chadema wafanye kwa wakati huu??

Mkuu Mchambuz,

Chadema ni mahodari katika mobilization,nguvu Yao katika hili la Covid 19 haijaonekana vya kutosha,sawaa wamechukua hatua zote wanazopaswa kuzichukua,lakin hazijaleta positive outcomes na wale watu bado wapo bungeni wakifuja kodi zetu kwa jina la chadema, before hawajaendelea kudai katiba mpya,chadema watuoneshe jins walivyo aggressive katika kuitetea hii iliyopo isivunjwe,kama hofu ni jiwe,jiwe limeondoka zake
 
Hasn’t it crossed your mind labda akina Halima wanasubiri Baraza Kuu lifanye finishing (kwa mujibu wa Katiba ya Chadema) ili labda ndipo waende Mahakamani?

Kwanini waende Mahakamani kabla ya Baraza kutolea maamuzi rufaa zao?
 
Mkuu nimeshindwa kukuelewa uliposema suala la hawa wabunge 19 linafuja pesa zetu za jasho la kodi yetu. Nijuavyo mimi idadi hiyo ya wabunge ipo kikatiba na ni sehemu ya wabunge 393 wanaopaswa kuwepo bungeni na bajeti yao tayari imeshapangwa.Kwahiyo sioni kama hoja yako ya kufuja pesa zetu sisi walipa kodi kama ina mashiko. suala lililopo ni kwamba nyinyi hamtaki hayo majina yaliyopelekwa, mnataka majina yatoke mfukoni kwa mbowe, ambapo kimsingi sisi walipa kodi hatuangalii ni kina nani wapo Bungeni bali kama uwakilishi umetosheleza kama katiba inavyosema basi tumeridhika tunasubiria 2025.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…