Elections 2015 Magufuli lugha za Kimataifa ni Kizungumkuti, wenye ufahamu tujadiliane

Elections 2015 Magufuli lugha za Kimataifa ni Kizungumkuti, wenye ufahamu tujadiliane

hebu jaribu kutuonyesha ukweli wa hicho ulichoandika!; wapi alichemsha?? Tupe angalau video clip!!!

mimi nataka rais kama magufuli kama hajui kimombo. Hii inatokana na ukweli kwamba watazania wengi wanakidharau kiswahili chao na badala yake wanashadidia kiingereza utadhani wamezaliwa londoni. Uzalendo kwanza ni kutumia lugha ya kiswahili katika mambo mengi ikiwa ni pamoja na raisi kutokutumia kiingereza wakati wowote.
Napendekeza rais ajaye asitumie kiingereza ili apate sifa kuwa rais wa kwanza duniani kwa kuwa mzalengo kwa lugha yake na nchi yake lakini pia anatambua utamaduni wa taifa lake. Nina uchungu mkubwa sna kuona kwamba watu wanashadidia vya ulaya lakini wanasau mambo yao ya msingi ambayo yanatambulisha utaifa wao ambayo ni pamoja na kiswahili.
Ahsante sna sana san
 
Hakuna anayeshadidia vya ulaya. Ungekuwa umesoma comments za watu hapa usingeandika haya. Hatusemi kiingereza ni bora kuliko kiswahili ila tunamshangaa alisomaje mpaka ngazi ya phd huku hawezi kuzungumza hata sentensi moja ya kiingereza kwa usahihi. Tunaquestion uwezo wake na kutosha kwake kwa nafasi anayoomba!
 
Hawa wadhungu nadhani alikua anaongea nao kisukuma
 

Attachments

  • 1443738770387.jpg
    1443738770387.jpg
    12.6 KB · Views: 211
Kuna watu nao humu kumbe ni sawa tu na huyo bondia hv mtu unalinganishaje IQ na vyeti nadhan hujui hata maana ya IQ
Kwa kifup IQ ya magufuli ni zero kabixa ndo maana anaweza kuruka kny magari na kupiga push up ovyo ovyo
 
Nimejaribu kufuatilia uwezo na uelewa na mwenzetu huyu katika arena za kimataifa ni zero na uwenda akafanya vituko kama vya ndugu Mulugo aliyekuwa naibu waziri wa elimu kuwa Tanzania ni muungano wa Tanganyika na Zimbabwe.

Hiyo ilitokana na kushindwa ngeli na kubaki kukariri tu.Upungufu huu wa exposure kimataifa na lugha ni tatizo na ndio maana watu wasio na uwezo kama akina Makamba wanajitia kimbelembele kama wapiga zomari kwa Magufuli huku wakinyendea nafasi kama washuri wake akibahatika kuwa rais kama shetani atabariki.Mungu yupo upande wa Legwanani the Great.

Hivi kama alikuwa mwalimu alifundisahaje huko? Natafuta wanafunzi wake angalau nipate expreience ya huyu ndugu yetu Magufuli.

==================




What the https://jamii.app/JFUserGuide, yaani ndiyo anataka urais wakati hajitambui? Kumbe ndiyo maana kwenye mikutano yake anatanguliza wasanii kupiga saa moja then yeye anakuja kuongea kwa dakika 15. This is nonsense now. Watanzania msishtuke tu na kupatwa na ugonjwa wa moyo, inabidi kuhamka na kuona mbele.
 
Magufuli ana kipaji cha lugha, sijui ilikuwaje kwenye kizungu!! Hii inaonyesha ni jinsi gani tulivyo na mfumo wa elimu mbovu.

Kwa serikali yenye sera tegemezi kama CCM inatakiwa kizungu kiwe kinapanda. Sasa huyu mwenzetu sijui ataongea nao nini!!!?
 
Pombe kwenye mikutano atasalimia salamu za makabila mengi lakin siyo gud morning, gud afternoon, good evening, whatsapp, how do u do, hello, hi!
 
Hawa wadhungu nadhani alikua anaongea nao kisukuma

Anajitutumua kuongea lakini anavunjavunja kama Form One! Sidhani km hata walimwelewa. Watu watatushangaa sana watanzania kwamba hivi hatukuju akwamba huyu mtu hawezi kucommunicate kwa kiingereza halafu tunampa nafasi kubwa namna hiyo inayolzima kujua vizuri lugha!
 
mwacheni pombe aingie Ikulu achape kazi hagombei uwaziri wa Mambo ya nje mbona Rais wa China hajui kingereza. Hapa kazi tu
 
Anajitutumua kuongea lakini anavunjavunja kama Form One! Sidhani km hata walimwelewa. Watu watatushangaa sana watanzania kwamba hivi hatukuju akwamba huyu mtu hawezi kucommunicate kwa kiingereza halafu tunampa nafasi kubwa namna hiyo inayolzima kujua vizuri lugha!

Suala ni kuwa kwa mfumo wa elimu ya Tanzania kiingereza ni somo la lazima toka SHULE ya msingi hadi Sekondari (form 4). Lugha ya kiingereza ni lugha ya kujifunzia toka Sekondari hadi PhD! Suala linakuja inawezekanaje MTU katika mazingira haya asijue kabisa kuunda hata sentensi moja iliyo sahihi? Rais wa China mazingira yake ya SHULE hayakumpa fursa ya kujua kiingereza kama ambavyo watanzani hatujui kijerumani. Kama magufuli angeshindwa kuongea kijerumani tusingeshangaa?
Lakini kwa sasa tuna sababu ya kuhoji uwezo wake kitaaluma hata kuhoji uhalali wa vyeti vyake!
Napendekeza mdajalo kwa lugha ya kiingereza kati ya Magufuli na wanafunzi wa kidato cha tatu tuone kama kuna atakayepona kuvunjika mbavu!!!!
CC magembe 32
 
Congratulations....

Naona alitamka....


CONJRWAJURESION to you....😂😂😂


Poorest pronounciation ever...!!!
 
Kiingereza siyo lugha ya Taifa. Namshauri Rais Magufuli atufungulie ukurasa mpya kwa kutumia kiswahili popote aendako na kwenye dhifa za kitaifa. Sisi Tanzania ni nchi pekee katiba nchi zilizotawaliwa na uingereza yenye lugha ya Taifa. Magufuli onyesha mfano kwa kuikuza ienee duniani kote. Kiingereza ni lugha ya biashara acha ibaki kwenye makabrasha wataalamu waihangaikie. Usijali UDSM watakupa wakalimani kila unaposafiri ambako hawajui kiswahili. Ukiweza hili utawaonyesha viongozi wa Sfrika kuwa Tanzania bado inaendelea kuwakomboa.
subiri akapewe digrii akiwa madarakani kama akipata. na hata ikibidi uprofesa. sijawahi kusikia kiongozi kama obama anatunukiwa degree akiwa madarakani. ni hapa bongo tu ndo inatokea
 
subiri akapewe digrii akiwa madarakani kama akipata. na hata ikibidi uprofesa. sijawahi kusikia kiongozi kama obama anatunukiwa degree akiwa madarakani. ni hapa bongo tu ndo inatokea

Wewe vipi? Naona hujaelewa nilichoandika. Magufuli anayo shahada ya uzamivu(PhD). Hapa tunazungumzia matumizi ya kiswahili kwa viongozi wetu nje ya nchi ili kienee dunia nzima.
 
Degree za magufuli alisoma kwa lugha ya kisqahili ndio maana n'gen'ge halipandi...
 
Back
Top Bottom