Binafsi nilishitushwa sana na Kauli ya Jana ya Mhe.Rais kuwa aliwahi wekewa sumu baada ya kupongezwa na Rais mstaafu Benjamin Mkapa.
Nimejiuliza maswali mengine sana.
Je!inawezekana wenyewe kwa wenyewe wanapowekeana sumu wasio wa kwao wanapotezwa kama Azory,Ben saanane?
Je!inawezekana wenyewe kwa wenyewe wanapowekeana sumu wasio wa kwao wanapigwa Risasi kama Lissu?
Je!inawezekana wenyewe kwa wenyewe wanapowekeana sumu wasio wa kwao wanatekwa kama Mo,na wengineo?
Je! Inawezekana wenyewe kwa wenyewe wanapowekeana sumu wasio wa kwao wanauawa kama Mawazo?
Kuna Maswali mengi sana ya kujiuliza lakini pia maswali haya hayana majibu.
Lakini swali la mwisho la kujiuliza ni hili,Hii Amani ya kweli ya nchi yetu kama tunavyoimba kwenye wimbo wa Taifa,au tunaimba kwaajili tu ya kuifurahisha Dunia? Mungu atunusuru na haya.kama kweli Dhamiri zetu zimekufa kiasi hiki hata kuchakachua uchaguzi nini kitatushinda?