mojax
Member
- Aug 18, 2015
- 13
- 23
ELIMU BIASHARA
MAGUMU YASIKUTISHE
Wengi wanaacha kutimiza malengo mara magumu yanapotokea lakini magumu ni kichocheo cha kuinoa akili yako kutenda katika viwango vya juu vya ubora lakini zaidi hukusaidia kuwa imara na usiyetetereka huko katika ufalme wa mafanikio yako. Leo nitakupa mfano wa wazi. Watoto wa maskini wengi hufaulu vizuri huko mashuleni kwa kuwa umaskini unawakera na wanaona elimu ni njia ya ukombozi lakini watoto wengi wa matajiri hawafanyi vizuri huko mashuleni si kwa kuwa hawana akili bali hawana jambo linalowasukuma kusoma kwa bidii.
Wahindi wengi (niliopata kusoma nao) hawafanyi vizuri shuleni na wengne huishia njiani kwa kuwa hawana changamoto ya kuhitaji elimu ile ya darasani ila wanafanya vizuri katika maduka ya wazazi wao kwa kuwa kwao kufeli biashara ni kujiandaa kufa maskini. Kitu cha kujifunza ni kwamba, Pasipo changamoto ni nadra kwa watu kukubali kujituma. Hakuna anayetafuta ukombozi kama tayari ana ukombozi, hakuna anayetafuta uponyaji kama ni mzima, hakuna anayetafuta shibe kama amevimbiwa. Hata kama umefanikiwa unaweza kujipa changamoto kwa kujiwekea malengo makubwa ambayo hata wewe yatakutisha maana kitisho ni changamoto.
Maisha yetu yamejaa changamoto nyingi sana hebu chagua changamoto za kuzipa kipaumbele na uanze kuelekea kufanikiwa kutokana na msukumo wa changamoto hizo. Kila changamoto ina msukumo wake na majibu yake. Changamoto ya usafiri husukuma juhudi za kutafuta baiskeli, pikipiki au gari na zaidi, kwa hiyo hapo itategemea na uzito uliouweka kwa changamoto uliyoipa kipaumbele, ila mtu hupokea anachokifikiria kichwani mwake na SI ZAIDI YA PALE.
JIKUNG'UTE, JIPANGE, ANZA.
Instagram Account: Elimu_biashara
MAGUMU YASIKUTISHE
Wengi wanaacha kutimiza malengo mara magumu yanapotokea lakini magumu ni kichocheo cha kuinoa akili yako kutenda katika viwango vya juu vya ubora lakini zaidi hukusaidia kuwa imara na usiyetetereka huko katika ufalme wa mafanikio yako. Leo nitakupa mfano wa wazi. Watoto wa maskini wengi hufaulu vizuri huko mashuleni kwa kuwa umaskini unawakera na wanaona elimu ni njia ya ukombozi lakini watoto wengi wa matajiri hawafanyi vizuri huko mashuleni si kwa kuwa hawana akili bali hawana jambo linalowasukuma kusoma kwa bidii.
Wahindi wengi (niliopata kusoma nao) hawafanyi vizuri shuleni na wengne huishia njiani kwa kuwa hawana changamoto ya kuhitaji elimu ile ya darasani ila wanafanya vizuri katika maduka ya wazazi wao kwa kuwa kwao kufeli biashara ni kujiandaa kufa maskini. Kitu cha kujifunza ni kwamba, Pasipo changamoto ni nadra kwa watu kukubali kujituma. Hakuna anayetafuta ukombozi kama tayari ana ukombozi, hakuna anayetafuta uponyaji kama ni mzima, hakuna anayetafuta shibe kama amevimbiwa. Hata kama umefanikiwa unaweza kujipa changamoto kwa kujiwekea malengo makubwa ambayo hata wewe yatakutisha maana kitisho ni changamoto.
Maisha yetu yamejaa changamoto nyingi sana hebu chagua changamoto za kuzipa kipaumbele na uanze kuelekea kufanikiwa kutokana na msukumo wa changamoto hizo. Kila changamoto ina msukumo wake na majibu yake. Changamoto ya usafiri husukuma juhudi za kutafuta baiskeli, pikipiki au gari na zaidi, kwa hiyo hapo itategemea na uzito uliouweka kwa changamoto uliyoipa kipaumbele, ila mtu hupokea anachokifikiria kichwani mwake na SI ZAIDI YA PALE.
JIKUNG'UTE, JIPANGE, ANZA.
Instagram Account: Elimu_biashara
Last edited by a moderator: