Shin Lim
JF-Expert Member
- Mar 27, 2012
- 7,837
- 14,198
Yule msanii anayesemekana kuwa ni bilionea kuliko msanii mwingine yeyote Tanzania ambaye pia ameanza kujenga hekalu lake huku likiwa halijakamilika kwa mvua tatu sasa (miaka mitatu), ambaye pia amekuwa akiwafunika wasanii wote wa Tanzania kwa shoo kali na ghali, ambaye pia amekuwa akiombwa namba za simu pamoja na collabo na wasanii wa Marekani akiwemo Chriss Breezy mkali wa so cold na with you bila kusahau forever, lakini yeye huwakatalia kutoa namba na collabo kwa sababu ni mkali mno.
Msanii ambaye vilevile Mbeya nzima hakuna Hotel ya kulala yeye wakati huo huo amepanga magheto mawili yenye price ya thirty five thousands huko maeneo ya Sinza, sasa mashabiki kama si wa Keko, Ukonga au Segerea, nyimbo kama kamwambie, my number one na kitorondo hazitakuwa ngeni masikioni mwao kwa sababu burudani hiyo mujarabu watakuwa wakiipata face to face tena bure kabisa kutoka kwa Diamond kwa sababu sasa atakuwa akilala na kuamkia jela kwa kwa fifteen years period na hata uji wa mahindi wa kesho uliowekwa chumvi ataanza kuuupata huko na kama hili litafanyika, basi atatoka akiwa na umri wa January Makamba.
Hii imetokana na msanii huyo nguli kabisa kutinga gwanda za kijeda na kukatia miuno jukwaani wakati wa shoo fiesta mwishoni mwa wiki jana.
Pamoja na mbwembwe hizo, mashabiki walionekana kumzomea na kutaja jina la mfalme Kiba mzee wa cinderela macmuga na mwana.
Kwa mujibu wa magazeti, inasemekana jamaa zake wa karibu walimwambia kuhusu hizo gwanda lakini alitia ngumu.
Kwa undani wa habari hizi jisomee gazeti la leo la lete mambo na Visa.
Msanii ambaye vilevile Mbeya nzima hakuna Hotel ya kulala yeye wakati huo huo amepanga magheto mawili yenye price ya thirty five thousands huko maeneo ya Sinza, sasa mashabiki kama si wa Keko, Ukonga au Segerea, nyimbo kama kamwambie, my number one na kitorondo hazitakuwa ngeni masikioni mwao kwa sababu burudani hiyo mujarabu watakuwa wakiipata face to face tena bure kabisa kutoka kwa Diamond kwa sababu sasa atakuwa akilala na kuamkia jela kwa kwa fifteen years period na hata uji wa mahindi wa kesho uliowekwa chumvi ataanza kuuupata huko na kama hili litafanyika, basi atatoka akiwa na umri wa January Makamba.
Hii imetokana na msanii huyo nguli kabisa kutinga gwanda za kijeda na kukatia miuno jukwaani wakati wa shoo fiesta mwishoni mwa wiki jana.
Pamoja na mbwembwe hizo, mashabiki walionekana kumzomea na kutaja jina la mfalme Kiba mzee wa cinderela macmuga na mwana.
Kwa mujibu wa magazeti, inasemekana jamaa zake wa karibu walimwambia kuhusu hizo gwanda lakini alitia ngumu.
Kwa undani wa habari hizi jisomee gazeti la leo la lete mambo na Visa.