Magwiji mmu na multi-id's

wakati nakua
mashindano ya ngoma za asili
yaliamliwa kwa mwenye watu wengi hadi muda ngoma inaisha ndio mshindi

ikikaribia muda wa kuisha ngoma
ndo ulikuwa muda wa viroja
maana kila mmoja anata kukusanya watu
wapo walovua hadaharani
wapo walodi...na hadharani

ndo yamekuwa hivi.
 
Wewe gwiji unaonaje ukitupa walau link ya hiyo sredi tujionee wenyewe jinsi gwiji mwenzako alivyo chemka
 
mh! hapa ni magwiji na ugwiji wao! bahati nzuri wanajuana kwa style zao..Mitishamba akiwa katibu..:biggrin:
 
Mamako naye alikuwepo?
 
Wewe gwiji unaonaje ukitupa walau link ya hiyo sredi tujionee wenyewe jinsi gwiji mwenzako alivyo chemka
nitakuwa nimemkaanga sana, mana ni mtu ambaye mnamuona kama vile kila anachosema humu mnakishabikia.
 
Shughuli ya kuwa na mult id's si ndogo inataka muda ila sishangai na nakubali wapo watu! Mana kweli unatakiwa uwe na muda wa ziada na wapo watu they are beyond addiction aisee hii id moja tu inanisumbua kuparticipate nipendavyo!

Suala la watu kujiona wanamiliki jukwaa hilo usiseme! Kuna mtu kasema wanalipia,hivi kuna kulipia humu tujuzeni vizuri! Humu kuna watu wanajua kupotezea hata hawana muda na michango ya watu wengine wanakuwa busy wao wanaojuana mi nimejiunga muda mrefu jf lakini si mchangiaji mzuri sababu zilizo nje ila nimeliona hili na huwa naona bonge la ushamba mana watu wamefahamiana humu lakini utazani wanajuana uraiani kama wamefikia kujuana walitokea humu yani si jukwaa la mmu peke yake watu wanapenda sana kupotezea wakiona ni new id kwao sielewi sababu ni nini kama si ushamba mana mchango ni mchango tu!
 
Wamekusoma hiyo!

Halafu wewe ni wa siku nyingi humu, kulikoni mbona huonekani?
 
Dah!

Umenikumbusha siku nilikuwa najijibu thread yangu moja kwa kutumia ile ID yangu nyingine klorokwini

Hakuna aliyenistukia........ Sredi iliuza kishenzi
 
Hilo nimelikumbuka.Kabla ya ku-join JF (nikiwa guest) na baada ya kuingia nikahisi kuna kitu kama hicho..by the way "nina uelwa kiasi wa kusoma katikati ya mistari"(namshukuru trainer wangu).Nilimuuliza mmoja wa member wa zamani ambaye amestaafu ku-post akaniambia ni kweli wapo wengi wenye mult IDS namalengo yanatofautiana: kuna ya kimkakati na ya kijinga..nitaeleza ya kijinga;

a/ili uonekane unapata wachangiaji wengi wa thread zako (kutafuta umaarufu wa kijinga).

b/ID moja kwa ajiili ya mambo ya msingi au yenye story zinazoeleweka na nyingine kwa ajili ya ku-comment kwa matusi thread za
mtu mwingine,kumchokoza mtu ambaye pengine unamfahamu na ku-post jambo la kijinga.

c/Ili uonekane umetoa mawazo yenye maana kwa sababu una wachangiaji wengi (kwa mtazamo wa mwenye mult IDS).

d/uoga wa kutoa mawazo yako kwa ID inayojulikana kwa sababu unahisi utakejeliwa au kutukanwa au kuonekana mjinga (kwa mtu mwoga/asiejiamini).

c/Kuona wenzako kama threat kwako unatumia IDS nyingine kuonyesha kwamba aliendika hajui lolote.

d/Kwa wanawake Hofu ya kuibiana mabwana hasa kama couple wako wote JF (anahisi awe na ID nyingi ili kumtisha kwa njia yeyote ile anayehisi ni threat kwa mahusiano yake -hatuwezi kudharau hili, wanawake wa nchi hii baadhi wanasifika hata nchi jirani kwa wizi wa waume/wapenzi za watu) ni hofu ya kijinga lakini ina logic kidogo.

Kwa la kuwa na ID nyingi kwa malengo ya kimkakati linatumiwa zaidi na wanasiasa na wapambe wao na maafisa wa usalama..naweza kuelezea siku nyingine.
 

Huu siyo ugunduzi bali kwa kiswahili kilicho nje ya kamusi wanaita UMBEA...!
 

Legends!!!!
 
Dah!

Umenikumbusha siku nilikuwa najijibu thread yangu moja kwa kutumia ile ID yangu nyingine klorokwini

Hakuna aliyenistukia........ Sredi iliuza kishenzi

Kumbe..halafu nilishakushtukia wewe!!hujambo lakn?
 
Sijui kama unajua navyokumisi.... sina uhakika.

Ila sijambo, na weye nijalie haliyo.

Mie mzima honey,,switi hati...because this is the day..the Lord has made.we will rejoice and be glad..
Halafu na mie nimekumisi lakn kidogo tu.....ila ntakuja kukusalimu hivi karibuni...
 
Mie mzima honey,,switi hati...because this is the day..the Lord has made.we will rejoice and be glad..
Halafu na mie nimekumisi lakn kidogo tu.....ila ntakuja kukusalimu hivi karibuni...
Haya yote in bold nayahifadhi moyoni mwangu.... deep inside......

mengine sijayasoma.
 
Posa kuna mtu namsaidia kuchanga changa akifikisha kiasi alete nyumbani. . . labda nikuunganishie kwa desh desh?

Heheh. . . hiyo ni siri ya watu watatu.
hakuna siri hapo tena.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…