Mahakama kutokuwa na uwezo kusikiliza kesi

kALEnga kidamali

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2015
Posts
542
Reaction score
735
Kwenu wadau..
Huwa napata sana shida ninaposikia mtuhumiwa kafikishwa mahakamani na kasomewa mashitaka lakini hakutakiwa kujibu chochote kwa kuwa mahakama haina uwezo wa kusikiliza aina hiyo ya kesi ya mtuhumiwa.

Sasa kwa wajuzi wa sheria na taratibu za mahakama, huwa kuna ulazima gani wa kumpeleka mtuhumiwa kwenye mahakama ambayo haina uwezo wa kuisikiliza kesi yake? Na huo utaratibu upo duniani kote au ni hapa kwetu tu?

Nawasilisha,
==================
kALEnga kidamali
 
Jamanj nasubiri majibu hapa, niliagiza lita moja ya ulanzi hadi inaisha sipati jibu kwani leo kuna shughuli za mahakama? Huwa najua hata wale mawakili wasomi kwa leo wikiendi watakuwa nyumban wakipumzika kwa kazi kubwa wanayoifanya wiki nzima.

Naongeza lita nyingine ya ulanzi huku nikiwa nikiendelea kusubiri majibu hapa kwa mama kipyatiro.
 
Mahakama zetu zimegawanywa kwa vitengo na mienendo tofauti tofauti kwa kuanzia chini kwenda juu, chini kwa maana ya mabaraza ya kata, wilaya, mahakama za mwanzo, wilaya, hakimu mkazi, kuu na Baba lao mahakama ya rufaa... sasa makosa mengi hasa ya kihalifu ni lazima yaanzie ngazi za chini kwanza ili kuweka utaratibu mzuri wa ukusanyaji taarifa za awali, ushaidi, utambuzi wa waarifu, aina ya kosa mpaka kosa kua completed na kupelekwa mahakama husika, mfano kesi za mauaji itawalazimu kwanza kuanzia mahakama ya wilaya ili kukamilisha mambo yote haya nliyokutajia then kesi hio itapelekwa mahakama husika ambayo ni kuu, lengo vile vile ni kuokoa muda sio kumkimbizia mtu kwenye mahakama kubwa ilihali mahakama hio kwa namba iko ndogo na ina kesi nyingi za kuskiliza so wanatakiwa wakienda huko kila kitu kiwe kinajulikama then kesi ianze mara moja.

Sheria imekua tofauti kwa upande wa madai kwakua huku bwana wanaangalia thamani ya deni, mali au madai yenyewe na utaona sheria kama CPC inatamka wazi tu kua kama kutakua na madai ya kiasi flani basi mdai atalazimika kwenda moja kwa moja mahakama flani.
 
Hizo ni taratibu za uendeshaji wa makosa ya jinai ,imelekezwa kisheria kwenye CPA(criminal procedure Act) mfano makosa ya mauaji,uwezo wa kusikilizwa ni mahakama kuu,za chini inapitia tu kwa utaratibu ampapo mtuhumiwa haruhusiwi kujibu chochote
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…