Mahakama Kuu: Freeman Mbowe (CHADEMA) afungua shauri kupinga mashtaka dhidi yake

Mahakama Kuu: Freeman Mbowe (CHADEMA) afungua shauri kupinga mashtaka dhidi yake

KESI IMEFIKA PATAMU, SASA DUNIA YOTE ILIYOKUWA HAIFAHAMU MATENDO YA CCM YA AWAMU YA 5 NA YA SASA YA AWAMU YA 6 YATAANIKWA NA KUFAHAMIKA KINAGA UBAGA

Kesi hii ya Mbowe itakuwa ktk vitabu kama kesi ya serikali ya makaburu dhidi ya Nelson Mandela. Kesi hii itasomwa ktk historia baada ya CCM kungolewa kutoka madarakani kwa kupitia uchaguzi huru kama kesi ya : Mpinzani Freeman Mbowe ndani ya 'mahakama' za CCM. ifahamike katika mabano neno 'mahakama' ni kuwa CCM inataka kuburuza Mahakama zitumike vibaya pamoja na mfumo wa kusimamia / kuchunguza za jinai (criminal justice system) nzima, lakini imani yetu bado ipo kuwa Mahakama hapa bila "mabano" ni mhimili huru na itatenda haki na kukataa mbinyo wa aina yoyote ile toka upande wowote.

Historia inasema makaburu waliokuwa ktk serikali ya kibaguzi ya Afrika ya Kusini iliona waAfrika raia wengine waliokuwa wanadai kuwa watu-uhuru, kutaka demokrasia shirikishi na Marndeleo ya watu wote walikuwa ni hatari na wangeweza kuchelewesha maendeleo ya vitu kama madaraja, reli, flyovers pamoja ni miradi mingine mikubwa iliyokuwa ya mfano barani Afrika. Madai hayo ya serikali ya kibaguzi ya wachache ya miaka hii yanarudiwa na CCM miaka hii ya 2015 - 2025. Na CCM pamoja na serikali yake kudai wapinzani ni watu hatari wasio na uzalendo na wasioitakia Tanzania maendeleo.

Soma utetezi wa Nelson Mandela alipofikishwa mbele ya korti na utetezi huo wa Nelson Mandela kuenziwa na watu wote duniani na taasisi kubwa za kimataifa na vyuo vikuu vijana kufunguliwa macho juu ya tawala kandamizi za kibaguzi, katili na vinazokandamiza utu wa watu na haki zao kwa kisingizio cha kujenga uchumi, madaraja, flyovers, mabwawa ya umeme n.k
AMEN
 
6 August 2021
Dar es Salaam, Tanzania

MVUTO WA KESI YA MBOWE NA WENGINE 4 : WAENDESHA MASHTAKA WA SERIKALI WABADILISHA HATI YA MASHTAKA
Purukushani za media katika Mahakama ya Hakimu Mkuu Mkazi Kisutu Dsm



Upande wa mashtaka leo siku ya ijumaa tarehe 6 Agosti 2021 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu umebadilisha hati ya mashtaka yaliyokuwa yanamkabili mwenyekiti wa CHADEMA na wengine wanne.

Maoteo kuwa kesi inayomkabili kiongozi wa chama cha siasa cha CHADEMA Freeman Mbowe na wenzake 4 kuvuta hisia mbalimbali za waandishi wa habari za media zote leo jijini Dar es Salaam Tanzania zimetimia.

Waandishi wengi wa vyombo vya habari walijitokeza ili waweze kuhabarisha umma wa waTanzania na dunia kwa ujumla na kila mwandishi habari alijitahidi kuhakikisha anaondoka na habari timilifu za picha za mnato, video, mitandao ya kijamii, magazeti, redio na Televisheni.

Tutegemee hali hii ya utulivu mahakamani ya waandishi kuweza kupata habari itaendelea namna hii mpaka hitimisho la kesi hii inayomkabili mwenyekiti wa CHADEMA kamanda Freeman Aikael Mbowe na wenzake 4.
Source : DARMPYA TV
 
jamani watanzania wenzangu wenye magonjwa kama;
1. KISUKARI
2. UKIMWI
3. SARATANI
4. KIFUA KIKUU
5. CELI MUNDU
Chukueni tahadhari hili wimbi la tatu lina puputisha balaa, aise.
 
7 August 2021

PROF: LIPUMBA AMZUNGUMZIA MBOWE KUHUSU SUALA LA UGAIDI.




Prof. Ibrahim Haruna Lipumba asema Haingii akilini gaidi akapelekewa salamu za rambirambi tarehe 8 Julai 2021 na Rais ambaye ni amiri jeshi Mkuu wa vyombo vyote vya ulinzi na usalama, halafu tarehe 23 Julai 2021 Freeman Mbowe akakamatwe kwa ugaidi wa mwaka 2020. Maana rais kila siku hupewa taarifa za usalama za nchi nzima, iweje tarehe 8 Julai 2021 Freeman Mbowe apelekewe salamu za rambirambi za msiba wa kaka yake. Ina maana rais alikuwa hana taarifa za ugaidi wa Freeman Mbowe anahoji Prof. Ibrahim Haruna Lipumba.


Source : StarTV Habari
 
Jenerali Ulimwengu - Kesi hii ni medani nyingine ya kufanyia Siasa. Na Mahakama sasa kuwa uwanja mwingine wa kufanyia siasa

Mwandishi mkongwe na wakili wa mahakama kuu Jenerali Ulimwengu amesema tuhuma zinazomkambili mwanasiasa Freeman Mbowe ni muendelezo wa njama za kumtoa ktk reli ya kisiasa mwenyekiti wa CHADEMA

"Tafakuri ya kisiasa ni kuwa mbinu hii mpya ni hatua nyingine ya kujaribu kumtoa Freeman Mbowe katika uwanja wa siasa baada ya mbinu zingine zilizotumika huko nyuma kushindwa kufikia lengo la kumzima kiongozi huyo shupavu wa upinzani nchini Tanzania" anahitimisha maoni yake mwandishi wa habari na mchambuzi wa kisiasa Jenerali Ulimwengu.


Haiishi hadi inapokwisha.

Aluta Continua.
 
jamani watanzania wenzangu wenye magonjwa kama;
1. KISUKARI
2. UKIMWI
3. SARATANI
4. KIFUA KIKUU
5. CELI MUNDU
Chukueni tahadhari hili wimbi la tatu lina puputisha balaa, aise.

Waambie hawa:

IMG_20210711_205649_038.jpg


Kuhangaika na watanzania ni kutojitendea haki.

Habari ndiyo hiyo.
 
7 August 2021

PROF: LIPUMBA AMZUNGUMZIA MBOWE KUHUSU SUALA LA UGAIDI.




Prof. Ibrahim Haruna Lipumba asema Haingii akilini gaidi akapelekewa salamu za rambirambi tarehe 8 Julai 2021 na Rais ambaye ni amiri jeshi Mkuu wa vyombo vyote vya ulinzi na usalama, halafu tarehe 23 Julai 2021 Freeman Mbowe akakamatwe kwa ugaidi wa mwaka 2020. Maana rais kila siku hupewa taarifa za usalama za nchi nzima, iweje tarehe 8 Julai 2021 Freeman Mbowe apelekewe salamu za rambirambi za msiba wa kaka yake. Ina maana rais alikuwa hana taarifa za ugaidi wa Freeman Mbowe anahoji Prof. Ibrahim Haruna Lipumba.


Source : StarTV Habari


Aibu kubwa sana kwa serikali ya SSH.

Mbatia, Zitto na sasa Lipumba wametoa misimamo yao.

Asasi za dini, azaki, madhehebu, vyama vingine nk matamko yenu kwenye kadhia hii yaliyochelewa mno yanakuwa hayana maana sana.
 
Back
Top Bottom