Mahakama kuu imetoa hati kukamatwa Nabii na Mtume Josephati Mwingira

Wanamsaka vp wkt tuko naye hapa kona baa tunakula bata kweupee!!
 
Kwahiyo waumini wa MWINGIRa ni wakatili kiasi hiki cha kuwabomolea wanawake na yatima kule Mapinga halafu mnajiita wakristo!!!!

Wakristo my #$s.
kama nyie ni kweli wakristo pamoja na uozo huo basi mimi ni Mtume Paulo!!!
 
Afadhali kuwa brained washed by Mwingira, na siyo Shehe Yahaya kama wewe

Mimi ninaamini kuwa manabii ni akina Eliya, Elisha, Isaya, Jeremiah, Ezekiel na wengineo tunaosoma habari zao katika agano la kale. Nabii wa mwisho alikuwa Yohane Mbatizaji. Kazi ya hawa manabii ilikuwa kuwatayarisha watu kwa ujio wa Masiha Bwana Yesu Kristo. Hawa walikuwa wanapokea ujumbe moja kwa moja toka kwa Mungu na walikuwa wanaleta mapya katika ujumbe wao.

Bwana Yesu alipokuja aliteua mitume 12: Petro, Andrea, Yakobo, Yohane, Thoma, Yakobo, Filipo, Bartholomeo, Mathayo, Simon, Thadeo na Yuda Iskariote. Kisha akachaguliwa Mathia kuchukua nafasi ya Yuda Iskariote. Paulo akatokewa na Yesu naye na kuchaguliwa kuwa Mtume. Hawa ni waliolelewa na Bwana Yesu mwenyewe na kuteuliwa kuwa na kazi ya kumshuhudia ulimwenguni pote: "Nanyi mtakuwa mashahidi wangu .... hata miisho ya dunia" Matendo 1:8

Muda huu tunaoishi sasa Enzi ya Manabii na mitume imepita. Hebu tuambie ni ujumbe gani mpya anaouleta Mwingira? Na unabii wake ulishuhudiwa na nani kwamba yeye ametumwa na Mungu na kwa ishara gani? Na unapomweka mwingira kuwa nabii baada ya Yesu una maana gani? Kuwa ufunuo wa Yesu haukukamilika?

Anapojiita mtume ana maana gani? Yuko sawa na akina Petro? Ina maana aliteuliwa na Yesu moja kwa moja kama hao walioambiwa "njoo unifuate"? Au kama Paulo ambaye alitokewa naye njiani kwenda Damascus?

Anapounganisha unabii na utume ndio anaharibu kabisaaa! Ina maana haoni tofauti ya hayo mawili? Au ndio awe mkubwa zaidi? Au ndio apate wafuasi wengi? Au ndio aweze kujichukulia sheria mkononi?

Halafu mtu mwenyewe ndio huyo hata sheria za nchi hawezi kuzifuata.

Be serious mkuu, kama sio kuwa brainwashed ni nini?

Afadhali angejiita Askofu au Mchungaji, then tungeangalia hata anachokifanya. Hicho alichokifanya ni kujitafutia utukufu wa hapa duniani (kujikweza). "
Na ye yote atakayejikweza, atadhiliwa; na ye yote atakayejidhili, atakwezwa." Mt. 23:12

"Jihadharini na manabii wa uongo. Wao huja kwenu wakionekana kama kondoo kwa nje, lakini kwa ndani ni mbwa mwitu wakali"
.
Mt. 7:15
 

Mkuu elimu yako katika maandiko y biible na jinsi unvyochmbua mambo huwa najifunza mengi. Tumuomobee huyu mchungji mristu mwenetu anayejita mtume aache kujikweza.
 
Waatakuwa wambea.wanamsaka vipi?si waende mwenge kanisani au nyumbani kwake kibaha?kwani kajificha?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…