Black Butterfly
Senior Member
- Aug 31, 2022
- 130
- 368
Serikali kupitia Vyombo vya Ulinzi na Usalama inawajibika kuwalinda raia wake kila wakati bila kujali hali zao au matendo yao. Haki ya Kuishi inakoma tu pale Mahakama inapotoa adhabu ya Kifo kwa mkosaji.
Ibara ya 14 hadi 17 ya Katiba ya Tanzania inalinda Haki ya Kuishi kwa Sheria namba 15 ya mwaka 1984 Ibara ya 6 inayotamka kuwa "Kila mtu anayo haki ya kuishi na kupata kutoka kwa jamii hifadhi ya maisha yake, kwa mujibu wa sheria".
Haki ya Kuishi pia ni Ibara ya 3 katika tamko la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa. Ibara hii inasema Kila mtu ana Haki ya Kuishi na kwamba haki hiyo inalindwa na Sheria na hakuna Binadamu anayepaswa kunyimwa haki hiyo.
Ibara ya 14 hadi 17 ya Katiba ya Tanzania inalinda Haki ya Kuishi kwa Sheria namba 15 ya mwaka 1984 Ibara ya 6 inayotamka kuwa "Kila mtu anayo haki ya kuishi na kupata kutoka kwa jamii hifadhi ya maisha yake, kwa mujibu wa sheria".
Haki ya Kuishi pia ni Ibara ya 3 katika tamko la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa. Ibara hii inasema Kila mtu ana Haki ya Kuishi na kwamba haki hiyo inalindwa na Sheria na hakuna Binadamu anayepaswa kunyimwa haki hiyo.