JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,780
- 6,607
Mahakama Kuu ya Tanzania imeliamuru gazeti The Citizen kumlipa fidia ya shilingi bilioni mbili aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Mchechu kwa kuchapisha habari zilizomshushia hadhi.
Hukumu hiyo imetolewa leo Mahakama Kuu, Masijala ya Dar es Salaam, ikielezwa kuwa gazeti hilo lilichapisha taarifa ambazo zilimtuhumu Mchechu juu ya matumizi mabaya ya fedha za umma na kutumia maneno yaliyoshusha hadhi yake, huku wakidai walinukuu maneno ya aliyekuwa Rais wa Tanzania, hayati John Magufuli alipokuwa akizindua mradi wa nyumba za NHC zilizopo Dodoma mwaka 2017.
Chanzo: Azam TV
Hukumu hiyo imetolewa leo Mahakama Kuu, Masijala ya Dar es Salaam, ikielezwa kuwa gazeti hilo lilichapisha taarifa ambazo zilimtuhumu Mchechu juu ya matumizi mabaya ya fedha za umma na kutumia maneno yaliyoshusha hadhi yake, huku wakidai walinukuu maneno ya aliyekuwa Rais wa Tanzania, hayati John Magufuli alipokuwa akizindua mradi wa nyumba za NHC zilizopo Dodoma mwaka 2017.
Chanzo: Azam TV