Mahakama yamgomea Rigathi Gachagu

Mahakama yamgomea Rigathi Gachagu

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Mahakama ya Rufani nchini Kenya chini ya jopo la majaji watatu imekataa kuingilia kati mchakato wa kuondolewa madarakani kwa Naibu wa Rais Rigathi Gachagua kupitia ombi la kuzuia mchakato huo.

Aidha, mahakama hiyo imesema mchakato huo utaendele kama ulivyopangwa bila kuingiliwa na mamlaka hiyo kwa sasa.

Mahakama iliyoketi mapema leo Jumatano Oktoba 16,2024 ilikataa kutoa maagizo ya kusitisha kesi ya kushtakiwa kwa Naibu wa Rais Rigathi Gachagua katika Bunge la Seneti.

Majaji Erick Ogolla, Antony Mrima na Frida Mugambi wamesema hakuna suala lolote litakalomkuta Gachagua, iwapo Bunge la Seneti litaendelea na hoja ya kumtimua katika wadhifa huo.

Hata hivyo, Majaji hao wamesema uamuzi huo haumuzuii Gachagua kukata rufani kuupinga katika korti nyingine kama hatoridhika nao na pia mahakama bado inaweza kuamua matokeo ya mchakato wa Bunge.

Wakijibu uamuzi huo, timu ya wanasheria wa Gachagua imetaka kurekebisha ombi hilo kulingana na kile ambacho kinaweza kushuhudiwa katika Bunge la Seneti.
 
IMG-20241016-WA0006.jpg
 
Sema huyu jamaa akiondoka ruto naye ajiandae sioni Ruto akitoboa zaidi ya 2027
 
Mahakama ya Rufani nchini Kenya chini ya jopo la majaji watatu imekataa kuingilia kati mchakato wa kuondolewa madarakani kwa Naibu wa Rais Rigathi Gachagua kupitia ombi la kuzuia mchakato huo.

Aidha, mahakama hiyo imesema mchakato huo utaendele kama ulivyopangwa bila kuingiliwa ba mamlaka hiyo kwa sasa.

Mahakama iliyoketi mapema leo Jumatano Oktoba 16,2024 ilikataa kutoa maagizo ya kusitisha kesi ya kushtakiwa kwa Naibu wa Rais Rigathi Gachagua katika Bunge la Seneti.

Majaji Erick Ogolla, Antony Mrima na Frida Mugambi wamesema hakuna suala lolote litakalomkuta Gachagua, iwapo Bunge la Seneti litaendelea na hoja ya kumtimua katika wadhifa huo.

Hata hivyo, Majaji hao wamesema uamuzi huo haumuzuii Gachagua kukata rufani kuupinga katika korti nyingine kama hatoridhika nao na pia mahakama bado inaweza kuamua matokeo ya mchakato wa Bunge.

Wakijibu uamuzi huo, timu ya wanasheria wa Gachagua imetaka kurekebisha ombi hilo kulingana na kile ambacho kinaweza kushuhudiwa katika Bunge la Seneti.
Kenya wanajielewa hadi raha ila hayabyote yalikuja baada ya kumwaga damu uchaguzi 2007 au 8 ile.
Katiba yao ya Mwaka 2010 iliyopatikana kwa ncha ya upanga ndio imezaa matunda haya mazuri tunayoyaona.
Baada ya machafuko mabaya ya umwagaji damu ya mwaka 2007/2008 Sasa hivi Wakenya wanaheshimiana.
 
Katiba yao ya Mwaka 2010 iliyopatikana kwa ncha ya upanga ndio imezaa matunda haya mazuri tunayoyaona.
Baada ya machafuko mabaya ya umwagaji damu ya mwaka 2007/2008 Sasa hivi Wakenya wanaheshimiana.
Naona mnatamani sana kumwaga damu shida sasa upande huu wamejaa ma keyboard warriors.....labda badamu bamwagike kwenye keyboard
 
Naona mnatamani sana kumwaga damu shida sasa upande huu wamejaa ma keyboard warriors.....labda badamu bamwagike kwenye keyboard
Hakuna mtu hata mmoja ambaye ni raia mwema anayetamani kumwaga damu za watu wasio na hatia, isipokuwa pale inapobidi tu. Na hii hutokea baada ya watu waovu kuwalazimisha watu wema kufanya hivyo Kama ilivyotokea huko Kenya. Hata hapa Tanzania nako pia Watu waovu wanatulazimisha sisi raia wema kufuata mkondo huo huo wa Kenya, hii ni kutokana na sababu za kufululiza kwa vitendo viovu vya utekaji, utesaji na mauaji ambavyo vimekuwa vikielekezwa kwa raia wema wasio na hatia. Vitendo hivyo viovu vya utekaji na mauaji ya kiholela mpaka Sasa tayari vimewaamsha baadhi ya raia wema kukaa mguu sawa kwa ajili ya kuchukua hatua ama za kujihami navyo au wajibu mapigo ili kupinga kufanyiwa uovu huo.
 
Hakuna mtu hata mmoja ambaye ni raia mwema anayetamani kumwaga damu za watu wasio na hatia, isipokuwa pale inapobidi tu. Na hii hutokea baada ya watu waovu kuwalazimisha watu wema kufanya hivyo Kama ilivyotokea huko Kenya. Hata hapa Tanzania nako pia Watu waovu wanatulazimisha sisi raia wema kufuata mkondo huo huo wa Kenya, hii ni kutokana na sababu za kufululiza kwa vitendo viovu vya utekaji, utesaji na mauaji ambavyo vimekuwa vikielekezwa kwa raia wema wasio na hatia.
Mnalazimishwa wapi.....mnavyojitutumuaga kwenye keyboard kama majasiri kweli vile,,,,,mkiambiwa muandamane tu mkiona kagwanda ka ffu nduki sembuse mletewe kabisa mabakabaka
 
Rip deputy
Mnawasisitiza vijana wajiajiri
Nyie mkikataliwa kwenye nafasi zenu mnang'ang'ania
Sepa Babu
 
Mnalazimishwa wapi.....mnavyojitutumuaga kwenye keyboard kama majasiri kweli vile,,,,,mkiambiwa muandamane tu mkiona kagwanda ka ffu nduki sembuse mletewe kabisa mabakabaka
Kwa mtazamo wangu, kuandamana naona kama siyo njia muafaka ya kupinga vitendo viovu vya utekaji na mauaji ya kiholela.
 
Naona mnatamani sana kumwaga damu shida sasa upande huu wamejaa ma keyboard warriors.....labda badamu bamwagike kwenye keyboard
Badamu abamwagiki please muzee!
 
Badamu abamwagiki please muzee!
Hehe hawa wanaongea tu,,, hamna mwenye ubavu wa kufanya hivyo.......hawa wengi wanaosema mambo ya kuvuruga amani unakuta wametulia zao canada huko
 
Sema huyu jamaa akiondoka ruto naye ajiandae sioni Ruto akitoboa zaidi ya 2027
Ruto did his math very well, akaziona hasara za kuendelea kubaki na huyu jamaa, na akaiona fursa kumtema inavymletea political advantage kubwa na ushindi mkubwa zaidi 2027
 
Wewe ni Malaya wa kisiasa na CHAWA huwezi kuelewa kwa sasa kwa kuwa katiba inakubeba .Unapata chakula kwa kazi hiyo .Ipo siku utaelewa tu
Mnalazimishwa wapi.....mnavyojitutumuaga kwenye keyboard kama majasiri kweli vile,,,,,mkiambiwa muandamane tu mkiona kagwanda ka ffu nduki sembuse mletewe kabisa mabakabaka
 
Wewe ni Malaya wa kisiasa na CHAWA huwezi kuelewa kwa sasa kwa kuwa katiba inakubeba .Unapata chakula kwa kazi hiyo .Ipo siku utaelewa tu
Sawa malaya mwenzangu leo unatokea kitambaa cheupe ,,lile danga lako la juzi linakuulizia
 
Back
Top Bottom