Black Butterfly
Senior Member
- Aug 31, 2022
- 130
- 368
Hata hivyo, imekataa ombi la kusimamisha mchakato wa uchaguzi huo ambao sasa utaendelea kama ulivyokuwa.
Uamuzi huo umetolewa leo, Julai 17, 2024 na Jaji Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Salma Maghimbi baada ya kupitia maombi ya Mwabukusi na hoja zilizotolewa na wajibu maombi ambao ni TLS.
Mwabukusi alifungua shauri hilo Julai 11, 2024 katika Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Dar es Salaam.
Wakili huyo alikuwa miongoni mwa wagombea sita waliopitishwa na Kamati ya Uchaguzi ya TLS kugombea nafasi hiyo Juni 24, 2024.
Wagombea wengine waliopitishwa kuwania urais katika uchaguzi uliopangwa kufanyika Agosti 2, 2024 jijini Dodoma ni Ibrahim Bendera, Emmanuel Muga, Revocatus Kuuli, Paul Kaunda, na Sweetbert Nkuba.
Ikielezwa ni kwa sababu ya doa la kimaadili, Kamati ya Rufaa ya Uchaguzi TLS ilimuengua Mwabukusi kwenye kinyang’anyiro hicho kitendo anachokipinga.
MWANANCHI
PIA SOMA
- Mwabukusi afungua kesi kupinga maamuzi ya Kamati ya Rufaa ya TLS kumuengua kugombea Urais wa TLS
- Kamati ya Rufaa ya Uchaguzi imemuengua Boniface Mwabukusi kugombea nafasi ya Rais wa TLS