Mahakama yaridhia Wakili Mwabukusi afungue kesi ya kupinga kuenguliwa kuwania Urais TLS

Mahakama yaridhia Wakili Mwabukusi afungue kesi ya kupinga kuenguliwa kuwania Urais TLS

Black Butterfly

Senior Member
Joined
Aug 31, 2022
Posts
130
Reaction score
368
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imemruhusu wakili Boniface Mwabukusi kufungua shauri la marejeo ya uamuzi uliomwengua kwenye orodha ya wagombea urais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS).

Hata hivyo, imekataa ombi la kusimamisha mchakato wa uchaguzi huo ambao sasa utaendelea kama ulivyokuwa.

Uamuzi huo umetolewa leo, Julai 17, 2024 na Jaji Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Salma Maghimbi baada ya kupitia maombi ya Mwabukusi na hoja zilizotolewa na wajibu maombi ambao ni TLS.

Mwabukusi alifungua shauri hilo Julai 11, 2024 katika Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Dar es Salaam.

Wakili huyo alikuwa miongoni mwa wagombea sita waliopitishwa na Kamati ya Uchaguzi ya TLS kugombea nafasi hiyo Juni 24, 2024.

Wagombea wengine waliopitishwa kuwania urais katika uchaguzi uliopangwa kufanyika Agosti 2, 2024 jijini Dodoma ni Ibrahim Bendera, Emmanuel Muga, Revocatus Kuuli, Paul Kaunda, na Sweetbert Nkuba.

Ikielezwa ni kwa sababu ya doa la kimaadili, Kamati ya Rufaa ya Uchaguzi TLS ilimuengua Mwabukusi kwenye kinyang’anyiro hicho kitendo anachokipinga.

MWANANCHI

PIA SOMA
- Mwabukusi afungua kesi kupinga maamuzi ya Kamati ya Rufaa ya TLS kumuengua kugombea Urais wa TLS

- Kamati ya Rufaa ya Uchaguzi imemuengua Boniface Mwabukusi kugombea nafasi ya Rais wa TLS
 

Mwabukusi Kurudi Kinyang'anyiro cha Urais TLS 2024.? Siku ya Ijumaa Julai 26 2024 Hatma Kujulikana


View: https://m.youtube.com/watch?v=5QgrazCqbi4
Wakili msomi Jebra Kambole akiwa katika viunga vya Mahakama Kuu baada ya kumwakilisha mteja wao wakili Boniface Mwabukusi aelezea hali ilivyokuwa.... na umuhimu wa wanachama wa TLS kupata nafasi ya kuchagua kiongozi wanaye muafiki badala ya kuletewa...


Jopo la mawakili wasomi 18 wamejenga hoja kumshawishi jaji kuhusu haki ya wakili msomi kuweza kugombea nafasi ya urais TLS ambao sasa utaanza kutumikiwa kwa muhula wa miaka mitatu tofauti na huko nyuma ambapo muhula ulikuwa wa mwaka mmoja tu...


Mawakili walifurika katika Mahakama Kuu kufuatilia mwenendo wa kesi hii ya wakili Boniface Mwabukusu kupinga kuenguliwa na kamati ya Chama cha Mawakili Tanganyika -TLS kuwa hafai kugombea nafasi ya urais TLS ...
 
Huyo mheshimiwa kwa jinsi inavyoonesha kuungwa mkono na wenzake wengi, akiruhusiwa kurudi kwenye kinyanganyiro atashinda uchaguzi huo hata bila kupiga kampeni.
 

Mwabukusi Kurudi Kinyang'anyiro cha Urais TLS 2024.? Siku ya Ijumaa Julai 26 2024 Hatma Kujulikana


View: https://m.youtube.com/watch?v=5QgrazCqbi4
Wakili msomi Jebra Kambole akiwa katika viunga vya Mahakama Kuu baada ya kumwakilisha mteja wao wakili Boniface Mwabukusi aelezea hali ilivyokuwa.... na umuhimu wa wanachama wa TLS kupata nafasi ya kuchagua kiongozi wanaye muafiki badala ya kuletewa...


Jopo la mawakili wasomi 18 wamejenga hoja kumshawishi jaji kuhusu haki ya wakili msomi kuweza kugombea nafasi ya urais TLS ambao sasa utaanza kutumikiwa kwa muhula wa miaka mitatu tofauti na huko nyuma ambapo muhula ulikuwa wa mwaka mmoja tu...


Mawakili walifurika katika Mahakama Kuu kufuatilia mwenendo wa kesi hii ya wakili Boniface Mwabukusu kupinga kuenguliwa na kamati ya Chama cha Mawakili Tanganyika -TLS kuwa hafai kugombea nafasi ya urais TLS ...

Mkuu hawa Mawakili sasa wana tuchanganya; unamkataaje wakili mwenzako, ambaye ni mwanachama wenu? Au huko TLS kuna uwanachama wa mwanachama kamili, na robo ama nusu?
 
Habari njema leo hii.

Awali ya habari zote zinazo trend leo.

Nape alaaniwe.

Sheria ni msumeno.
 
Back
Top Bottom