Mahakama yatupilia mbali ombi la Jacquiline Ntuyabaliwe (Mjane wa Reginald Mengi) kuutambua wosia alionao

Mahakama yatupilia mbali ombi la Jacquiline Ntuyabaliwe (Mjane wa Reginald Mengi) kuutambua wosia alionao

USSR

JF-Expert Member
Joined
Jul 15, 2015
Posts
10,904
Reaction score
26,184
Mjane wa aliyekuwa mfanyabiashara maarufu Reginald Mengi, Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi ameangukia pua baada ya mahakama kutupilia mbali rufaa yake.

Ntuyabaliwe aliitaka mahakama iutambue waraka wa wosia wa marehemu Mengi ambao ulikataliwa na mahakama kuu.

USSR
---
Mahakama ya Rufani imetupilia mbali shauri la maombi ya marejeo lililofunguliwa na mjane wa Reginald Mengi, Jacquiline Ntuyabaliwe na wanawe wawili, ambao wamekuwa wakipambana kutetea wosia unaodaiwa kuandikwa na Mengi ambao Mahakama Kuu iliubatilisha.

Katika shauri hilo, Jacquiline na wanawe anaowasimamia, Jayden Kihoza Mengi na Ryan Saashisha Mengi walikuwa wanaiomba mahakama irejee na hatimaye itengue uamuzi uliotupilia mbali shauri la maombi ya mapitio, walilolifungua awali mahakamani hapo wakipinga hukumu ya Mahakama Kuu, iliyoukataa wosia huo.

Hata hivyo, katika shauri hilo la maombi ya marejeo namba 748/01 la mwaka 2022, mahakama hiyo katika uamuzi imewakatalia maombi ya kuurejea uamuzi huo ikisema sababu zilizotolewa hazina mashiko.

Katika uamuzi huo uliotolewa na jopo la majaji watatu waliosikiliza shauri hilo, Rehema Mkuye (kiongozi wa jopo), Abraham Mwampashi na Zainabu Muruke, mahakama imesema sababu walizozitoa si miongoni mwa zile za kuomba mahakama kufanya marejeo ya hukumu yake, bali zinahusu rufaa.

Uamuzi huo ulioandikwa na Jaji Muruke kwa niaba ya jopo hilo, ulitolewa Agosti 5, 2024 na unapatikana katika tovuti ya Mahakama iitwayo Tanzlii.

PIA SOMA
- Jacqueline Mengi aendelea kudondokea pua rufaa, mahakama yaondoa maombi yake ya kutaka kuurudisha wosia
 
Mjane wa aliyekuwa mfanyabiashara maarufu Reginald Mengi Jacline Tuyabaliwe ametangulia pua baada ya mahakama kutupiliwa mbali rufaa yake .

Ntuyabaliwe aliitaka mahakama iutambue waraka wa wosia wa marehemu Mengi ambao ulikataliwa na mahakama kuu .


USSR
Apunguze tamaa.
Aridhike na alichokwisha pata maana siyo haba.
Tamaa haijawahi kuacha mtu salama
 
Watu walimshauri akae karibu na watoto wakubwa, aombe kua anapata huduma na ada za watoto, akashupaza shingo sasa ataambulia aibu kubwa, waraka wenyewe umekaa kimchongo sana , mahakama kamwe haiwezi kuuzingatia kabisa
 
Mjane wa aliyekuwa mfanyabiashara maarufu Reginald Mengi Jacline Tuyabaliwe ametangulia pua baada ya mahakama kutupiliwa mbali rufaa yake .

Ntuyabaliwe aliitaka mahakama iutambue waraka wa wosia wa marehemu Mengi ambao ulikataliwa na mahakama kuu .


USSR
Bashite alisema wasiende Mahakamani, wanapoteza muda na watapoteza ‘haki zao’ hivyo waende kwake.
 
Nae anataka kuwa kama mtikila (R.i.p) Kila siku mahakamani angeishi vizuri na hiyo familia tena akiwa na dam Yao mbona angeishi poa though hata Sasa anaishi poa shida yake anataka awe super woman atambie wenzake as powerful woman in tz
 
MTU ukipata bahati ya kuwa karibu a smart guy Kama Dr Mengi unbidi kuvuna na kuchota AKILI yake na sio MALI na FEDHA pekee.

Unfortunately watu huwa hawajui hii siri .

Nandi alipata bahati ya kutembea na Ruge mtahaba na Ruge alichofanya alimpa njia za kuishi mjini na kufanikiwa.



The same harmonize kwa diamond.

Hivyo watu wengine hasa wanawake ukipata bahati ya kuwa na kibopa mchote AKILI na maarifa ili hata mkiachana usiterereke kiuchumi.


Just imagine MTU Kama Jack amekaa na Mengi muda wote Ila ameshindwa kujitengeneza kuwa brand na kufanikiwa .

Pasipo hata kupewa urithi kitendo cha kuwa karibu na mengi alibidi kuwa ameshajipata tangu zamani.
 
Back
Top Bottom