Mahakama zetu Tanzania zijifunze kitu kutokana na kilichotokea Kenya hivi Punde

buhange

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2011
Posts
505
Reaction score
110
HAbari wanajukwaa!

Nimefuatilia kwa karibu usomwaji wa kesi na maaamuzi ya mwisho katika kesi ya msingi iliyofunguliwa na Muungano wa vyama vya upinzani nchini Kenya NASA kupinga matokeo ya uchaguzi, na kugundua kwamba kuna haja wa mhimili wetu wa Mahakama nchini Tanzania kujifunza kitu kutokana na kilichofanywa na jopo la Majaji 7 kutengua uhalali wa matokeo ya uchaguzi ambayo yalimpatia nafasi tena ya kuongoza Rais Kenyata. Maamuzi ya Majaji wetu yazingatie uhalisia wa Mambo na weredi, wasifanye maamuzi kuridhisha Tabaka tawala.

Aksante.
 
Kwa matokeo ya urais katiba ndio mbovu na sio mahakama.

mafisadi hayana rangi
 
Huenda mahakimu wanakuaga na upande wao. Vipi kama hao mahakimu watano ni wa upande wa pili na wale wawili ni wa upande mwingine.

Sababu haiwezekan kama humu humu tulikuwa tunasifia tume ya uchaguz ya Kenya kuwa ni tume huru na ya kuigwa. Hiyo hiyo tume imetangaza upupu kwa mujimu wa mahakama za nchi yenye democracy ya kuigwa Africa according to members fulan fulan humu ndani. Tuwe na akiba ya maneno wakuu, ni hayo tu..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ila watanzania kwa kudakia ajenda tunaongoza. Unafiki ndo mkate wetu wa kila siku. Vidole na bundle vinatufanya tuongee kila linalotoka. Leo kila cha kenya kizuri. Sijui kama mna idea ya maisha Ila Sio mbaya. Mtandao ndo home Petu. ODINGA katukanwa wewe kisa Rafiki wa JPM Kama JPM binadamu mwenye haki ya kuwa na urafiki na mtu yeyote. Watu kama Mange leo wanasemaje. Watabadilisha Gia angani lakini nobody atauliza maswali magumu. Sisi tuliowahi tukablockiwa. Ila utaskia Demokrasia. Demokrasia sio ya mbinguni ni ya hapa .tujifunze ukweli ndo Hutuweka huru. Kama mwanamke nimejifunza Mengi sana. Hatujitambui na mwenye kelele ndo Mshindi bongo
 
Mahakama tz zinaegemea u pande wa serikali, always, ni vigumu sana kuwa haki mahakamani, na kama ipo basi viongozi wa uwamsho wangekuwa huru hivi sasa, Sina imani na mahakama Tanzania

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Hakuna aliyesema tume huru haiwezi kufanya kosa. Hata mahakama huru yaweza kufanya makosa. Judgement bado haijatolewa na tunaingoja. Mahakama ilisema itatoa hukumu yote kabla ya tarehe 22.

Hayo malamilishi yaliyoletwa ni ya transmission sanasana na IEBC sio Communications Authority of Kenya. Kwa maoni yangu, naona Majaji walikosea sana.
 
Mleta mada umesoma katiba ya nchi yako?
Ama unadhani mhimili wa mahakama unafanya kazi kama afanyavyo SIZONJE?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…