Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Undugu upi Sasa 😂😂.Hakuna kibaraka anaweza chaguliwa.Kibaraka kashinda uchaguzi ndani ya chama chake kihalali. Raila ana undugu na bi tozo
Undugu upi Sasa 😂😂.Hakuna kibaraka anaweza chaguliwa.
Bi Tozo amekampenia Watanzania kibao na Wameshinda .
Vibaraka kama kina Lisu watachaguliwa na watu wajinga kama wewe 🤣🤣
Sasa ameshindaje? 😁😁 Alikuwa anashindana na nani? 🤪🤪Angejikampenia na yeye ndani ya chama ashinde kihalali
Cheo Cha waziri mkuu kina nuksi sanaHuyu mzee ana roho mgumu aisee
Tangu kijana mpaka leo bado anatafuta cheo tu
Ila hana bahati masikini
Yaani umchague mtu dizaini ya Mwendazake?Raundi ya kwanza
Odinga 20, mgombea wa Djubut 18 na Mgombea wa SADC 10
Round ya pili
Raila Odinga 22, mgombea wa Djubut 19 na Mgombea wa SADC
Unadhani kwanini Raila Odinga amefeli? 🐼
Non sense excusesUmoja wa Africa umetaliwa na watu wanaongea kifaransa na uislamu kama hauna hizo sifa ni ngumu sana...
Sasa ameshindaje? 😁😁 Alikuwa anashindana na nani? 🤪🤪
View: https://x.com/Rahma_Simba/status/1890791620234371458?t=1bSCLnt1xnoSnzvM6-LJRQ&s=19
Huwezi kuwa inatokea Nchi ya wasakiti na vibaraka kama Kenya harafu ukashinda.
Odinga ni mgombea sahihi ilakutoka Nchi ya hovyo 🤣🤣🤣😬
Pole sana Mzee ndio hivyo tena maisha yaendelee.
View: https://x.com/TheCitizenTz/status/1890788433095770264?t=QRzw9yOabqLLKXXgzZhezA&s=19
My Take
Hii ni mara ya pili Kenya kuangukia pua,Tanzania hatujawahi shindwa popote.
View: https://www.instagram.com/p/DGGTdQ-oSgC/?igsh=emRtNDhycXcxcjNu
Useless narationTunapenda sana kukimbilia neno amani kama kichaka cha kujifichia na kuendelea kuwafanya watanzania wajinga.
Amani ya Tanzania hapo kwasababu ya CCM, Amani ya Tanzania ni Baraka tu ambayo Mwenyezi Mungu ametutunuku, ndio maana hata kabla hata ya CCM, watanzania hawakuwa watu wa kupiganapigana, Uhuru watanzania waliudai Kwa majadiliano mezani na ukapatikana, ,hizi ni Baraka tu za Mwenyezi Mungu.
Sasa imekuwa amani ndio kichaka cha kujifichia kila wahujumu uchumi wa Tanzania na watu wake wakiguswa.
Tutambue Dhulma ikizidhidi sana amani sio tunu tena, hata hao watunza amani aka wananchi watachagua kufa kuliko hiyo amani.
Tuache Dhulma, tutende haki na tuishi kwa haki.
Mzee anamzungumzia Tundu Lissu eti kibaraka, kati ya Tundu Lissu na CCM nani ni vibaraka wa Wazungu, Waarabu na Wahindi, ni Tundu Lissu aliyewapa Wazungu migodi wachimbe madini? ni Tundu Lissu aliyewapa waarabu naa wahindi bandari, ni Tundu Lissu anayeyapa kazi makampuni ya barabara ya kichina tenda za ujenzi?
Ni Tundu Lissu aliyepokea ndege ya kijeshi kutoka jeshi la SAUDIA na siku chache baadaye tunasikia hadithi za Saudia na bandari Bagamoyo, ni Tundu Lissu anayehusika na mikataba mibovu na kuitia nchi hasara?, ni Tundu Lissu aliyetoa vibali vya uwindaji huko mapolini Kwa makampuni ya uwindaji? Ni Tundu Lissu aliyetoa tender ya kuuza sukari na kuingiza mafuta in bulk, Ni kibaraka Tundu Lissu aliyeingia mikataba ya IPTL na kuzuka escrow, Ni Tundu Lissu aliyepiga hela pale Songas Ubungo miaka nenda rudi, Ni Tundu Lissu anayeshindwa kumalizia Stieggler pale watanzania wapate 2200MW na ikiwezekana bei ya umeme ishuke.
Ni Tundu Lissu aliyeshindwa kuifikisha SGR Mwanza Kwa haraka Watanzania waache kufa barabarani kama kuku kwenye ajali, ni Tundu Lissu anayesababisha mfumo wa elimu kuwa mbovu, Ni Tundu lissu anayeshindwa kujenga miundo mbinu Bora Kila mahala Tanzania, NI Tundu Lissu anayeshindwa kuwapa Watanzania huduma Bora za Afya kila mahala, NI Tundu Lissu anayetumia hovyo hela za nchi kwenye matamasha ya wasanii mitaani, Ni Tundu Lissu anayeshindwa kukomesha wizi na rushwa Serikali.
Muwaambie hawa wazee siasa za propaganda zimeisha maana vijana wa sasa wana maarifa na akili nyingi za kupata taarifa na kutatua matatizo, Waambieni hawa wazee dunia ya sasa inahitaji watu wenye akili kuendesha mifumo na kukimbizana na maendeleo ya dunia, Mwambieni Mzee wakati yeye china mbaya huko aliko anatetea wanasiasa basi wenzie na familia yake wanasosomola tu keki ya Taifa.
Inaonesha jinsi wenzake wasivyomuamini na kufeli diplomasia ya Tanzania kwa ujumla..Rais Samia Suluhu ameshindwa kuwashawishi viongozi wenzake wampigie kura Raila Odinga.
..enzi za Nyerere, Mwinyi, Mkapa, na Kikwete, mgombea aliyeungwa mkono na Tanzania ilikuwa lazima ashinde.
Sasa ameshindaje? 😁😁 Alikuwa anashindana na nani? 🤪🤪
View: https://x.com/Rahma_Simba/status/1890791620234371458?t=1bSCLnt1xnoSnzvM6-LJRQ&s=19
Sasa kati ya Kenya na Djibouti nani mshirika wa karibu wa NATO?Kumpa Raila Odinga uenyekiti wa AU ingekuwa ni kumzawadia Ruto na wafuasi wake. Kumbuka Kenya ni "Mshirika Mkuu Asiye wa NATO"!
Djibouti ni taifa linalohangaika bila ushawishi mkubwa. Hakuna mtendaji mkuu mwenye ushawishi.
Lakini nadhani baadhi ya kambi za wapiga kura wa Afrika zilikuwa na sababu tofauti za kukataa kupanda kwa Kenya kwenye nafasi hiyo ya ushawishi. Odinga ni mwathirika wa sera mbovu za kigeni za nchi yake chini ya Ruto.
Ni hoja halali ya kimaendeleo, lakini si lazima iwe muhimu kwa kambi za wapiga kura wa AU. AU hupiga kura kulingana na maslahi ya kambi. Hatujui jinsi SADC ilivyopiga kura, hasa ikizingatiwa kuwa Marekani inatishia kuiwekea vikwazo Afrika Kusini.
Inaonyesha jumla ya kura ilikuwa 48 na Odinga hakufikia nusuHapa mimi sijamuelewa kabisa mleta mada.
Yaani round ya pili Odinga kapata kura 22 na mpinzani wake wa karibu kura 19, halafu Odinga kashindwa!
Kivipi?
Wenye D mbili embu njooni mtueleweshe, sisi wengine hatukufika kidato.