Maharage Chande: Treni ya umeme itatumia umeme wa TANESCO

Maharage Chande: Treni ya umeme itatumia umeme wa TANESCO

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Maharage Chande amesema kuwa usafiri wa Treni ya Umeme unaotarajiwa kuanza Nchini utatumia umeme wa shirika hilo.

Amesema hayo alipokuwa akizungumza na Wanahabari Ijumaa ya Desemba 16, 2022, Dar es Salaam ambapo ametoa ufafanuzi huo baada ya kuulizwa swali na mwandishi wa habari kuhusu umeme utakaotumika kuendesha usafiri huo.

Maharage amesema: “Unapozungumzia umeme unaohitaji kuendesha mradi kama huo unatakiwa kujiuliza unatosha? Ubora wake upoje na ni umeme wa uhakika?

“Kwa treni yetu ya umeme mfano itakayokuwa inatoka Dar es Salaam kwenda Moro na Dodoma, hiyo ina njia yake, hivyo masuala ya uhakika, kutosha na ubora yamezingatiwa ndio maana nasema umeme wa TANESCO ndio utakaotokea.”
 
Umeme ukikata tutaganda sehemu hadi urudi tena???

Kwa TANESCO hii ninashauri yatafutwe majenereta yawekwe kwenye behewa moja ili yawe backup umeme ukikatwa
 
Huyu kuitwa Maharage ni sahihi..labda waliompa Hilo jina watoe sababu za kimungu ndio nitaelewa...

Vinginevyo tubaki na swali la Maharagwe ya wapi?
 
Yani ukiwa unawasikiliza TANESCO unaweza kudhani ni chombo la kazi kwelikweli kumbe huku ground ni kinyume kabisaa ... Ni waomba Mungu tu kama sisi.

Sasa majumbani tu tia maji tia maji, mtayaweza ya treni?
 
Kwa train hii mbona hata umeme wa limao unasaidia tu tusiwaze wala nini [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
IMG-20221213-WA0000.jpg
 
Back
Top Bottom