Mahmoud Ahmadnejad: Rais aliyekataa mshahara mkubwa na kuendelea kupokea mshahara wa mwalimu na kurudi na kufundisha baada ya miaka 8 ya urais

Namkubali sana jamaa ni mtu simple
 
Ahmadinejad aliisababishia Iran vikwazo vingi. Ni ultra nationalist ila mbishi na haangalii risks za ubishi na msimamo wake, ndio maana wanasiasa, bunge, supreme leadership na jeshi hawampendelei. Anapendwa na masheikh na wananchi wengi wenye msimamo mkali ambao hawajui dunia inaendaje uko nje. Ila kwenye masuala ya kijamii yuko vizuri hivyo akigombea kura anapata, mambo ya kiuchumi sio mzuri sana na mahusiano ya kimataifa ni muaribifu kabisa.

Mtu kama Raisi, Rais wao wa sasa ni mtulivu, haongei kwa jazba na hafanyi maamuzi kwa kukurupuka. Anauma na kupuliza, anakuja mikutano ya kimataifa anawahadaa kisha nyuma uko anafanya kile nchi yake inataka, he is buying time. Ahmadinejad ni mtata sana na controversial, kuwa na mkuu wa nchi mwenye mihemko ni risk. Yeye kuanzisha vita kwake ni kitu chepesi, wakati jeshi linajijua uwezo wake halisi ukiachana na mazungumzo ya public.
 
Marais wa Afrika wametoka katika familia masikini sana tena sio Marais tu hadi mameneja hivyo wakipata pesa au madaraka lazima waoneshe ulimbukeni na kuigiza kwingi yote ni kwa sababu ya maisha ya dhiki waliyokulia na ndio maana hata wakienda ulaya halafu wakaleta hiyo mikogo yao wazungu wanawacheki na kucheka sana wanawaona kama ni mizigo ya mavi tu.
 
Lakini vikwazo vilivyo wekwa kipindi cha Nejad huwezi kulinganisha na vikwazo vilivyo wekwa kipindi cha Rohan kipindi cha Rohan Iran iliwekewa vikwazo ambavyo havikuwahi kuwekwa hapo kabla pamoja na kwamba Rohan sio mtu wa msimamo mkali.
 
Watakuja kuponda na kuleta visababu vya darasa la pili unusu,ila ingekua ni Mzungu wangesifu mpaka Shati alilolivaa.
Poor reasoning. Hizi ni fikra za mtu ambaye ana upeo mdogo kabisa ambaye ameathiriwa na either wazungu, waafrika au waarabu. Mwandishi ameelezea vizuri kisomi kabisa. Nadhani mwandishi ni mtu aliyeelimika siyo wenzangu na mimi hawa ambao ndo hivyo tena. Uzungu, Uarabu Uafrika siyo issue hapa. Issue ni moyo aliyo nao hyo rahisi. Usihamishe magoli sababu ya kuji feel inferior au kuwa tu mlalamishi.
 
Haya matapishi umeniambia mimi?

Hivi umeelewa nilichokiandika? Nimeelezea jinsi ambavyo watu hua wana divert mada,

Ongeza umakini kabla hujaamua kumquote mtu.
 
Mwamba ni Doctor (PhD) wa Civil Engineer (wa kusoma kabisa) ila huoni akiitwa Dr. Ahmadnejad kipindi chote cha uRais wake
 
aliifanyia nini nchi yake kipindi Cha uongozi wake?
 
Lakini vikwazo vilivyo wekwa kipindi cha Nejad huwezi kulinganisha na vikwazo vilivyo wekwa kipindi cha Rohan kipindi cha Rohan Iran iliwekewa vikwazo ambavyo havikuwahi kuwekwa hapo kabla pamoja na kwamba Rohan sio mtu wa msimamo mkali.
Rohan aliendeleza sana mradi wa nyuklia, angekuwepo Ahmadinejad na akafanya development vile angepewa vikwazo vingi zaidi. Rohan mnaenda kwenye vikao anawachekea anawadanganya atakubali kisha akirudi kwake anafanya kwa siri, Ahmadinejad mkienda kwenye kikao anawachana atafanya na anawafokea.
 
Ukiangalia Homeland Season 3(2013) unaona kabisa jinsi wamarekani walivyopanga kumuua jenerali mkubwa kabisa wa Iran. Mwaka 2020 kweli wakaja kumuua Jenerali Qasem Soleimani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…