Mahusiano na dada wa kambo

Mahusiano na dada wa kambo

Penzi la kificho huwa ni tamu kama nawaona[emoji23][emoji1787]
Yaani we acha tu just imagine toka tuna miaka 17 .Mapenzi kajifunzia kwangu na mimi mapenzi nimejifunzia kwake. Mwanzo tulikuwa tunafurahia mchezo tukasema tutaacha

Baadaye ndio hivyo hisia zikajiingiza. Tulijaribu kuwa na mahusiano tofauti tukashindwa maana tulianza kuoneana na wivu na kuumia tu
 
Hadi kulileta huku, means nafsi zenu ziwasuta na hamna amani. Sasa ya nini kung'ang'ana!!
Ni kweli Tupo kwenye denial . Halafu hii siri inanitafuna sina mtu wa kuzungumzia naye kuhusu hili ili huku ni kama safe space hakuna anayenijua nikimwadithia rafiki nitaonekana wa ajabu sana
 
Habari wa ndugu, Heri ya mwaka mpya natumaini wazima ,

Nimekuja na hii mada sio kwa lengo la kujisifia au kutangaza dhambi ya zinaa ninazofanya nimekuja na huu uzi sababu nahitaji ushauri pengine msaada wa kimawazo maana nahisi sio kawaida

Nisikuchoshe nipunguze maneno ni hivi kipindi nipo sekondari mama aliachana na baba baada ya kipindi kupita akaolewa tena na huyo mume aliyemuoa alikuwa ana binti yake alizaa na mwanamke mwengine mimi na mama wote tuliamia kwenye familia hiyo ambapo ni baba anaishi na binti yake makamu yangu hata kidato tulikuwa kimoja, Sasa sijui kuishi ndugu wawili wakike na wakiume wasio wa damu inachangia au shetani au ni tamaa zetu mbovu tulijikuta mimi na huyo binti ambaye ni dada yangu wa kambo tunaingia kwenye mchezo mchafu.

Tulifanya kwa siri . Kipindi wazazi walikuwa hawapo tulikuwa tunafanya mapenzi sana saa nyingine binti ananyata usiku anakuja chumbani kwangu saa nyengine naenda chumbani kwake saa nyengine sebuleni ikawa ndio michezo yetu mpka tukanogewa tukajikuta tunapendana maana hizi constant casual sex na mtu mmoja lazima mcatch feelings . So ikaenda ikaenda ye akapata mahusiano mapya na mimi pia lakini bado roho zetu hazikuridhika ilibidi dada yangu aachane na mtu wake na alikuwa na wivu na mimi na hakutaka kujihusisha na mahusiano ikafikia kipindi nikaenda chuo na yeye mkoa tofauti bado tukawa tunafatana kitendo cha mimi na yeye kuwa mbali kinatuumiza moyo in short tunapendana sana

Mama yangu hakufanikiwa kuzaa na huyo baba wa kambo na walikuja kuachana lakini sisi hatukuacha mawasiliano na mahusiano wote tumekuwa na mahusiano na watu mbalimbali lakini tumeshindwa maana kila mmoja moyo wake yupo kwa mwenzake .sasa tunajitegemea kila mtu yupo kwake lakini tumeshindwa kuachana

Natamani kumuoa lakini alikuwa dada yangu wa kambo na tayari baba yake alishaachana na mama yangu natamani tusipendane lakini tunashindwa , mahusiano yetu ya siri toka tuna miaka 17 na sasa ni watu wazima jamii itanichukuliaje ikijua ?nifanye nini nimsahau? nimchukie au pengine tunahitaji msaada wa kisaikolojia hata sielewi maana wote tulipanga tuachane lakini imeshindikana sometimes najuta kwa nini nilikutana naye au kwa nini mama yangu alikubali kuolewa na baba yake .


Natamani nimkimbie nibadili mawasiliano lakini atafanya juu atanipata saa nyengine nashindwa kujificha kuna kipindi tuliachana tulishindwa maana tulikuwa katika hali mbaya sana kiufupi tunapendana sana na tunatamani uhusiano wetu uwe wazi tuoane lakini ndio hivyo sio sawa katika jamii.

Ni hayo tu samahani kwa ambao bandiko hili litawakwaza
Hakuna kosa kumpenda dada wa kambo na unaweza kumuoa bila kikwazo,msijiumize bure halalisheni uhusiano wenu,mie nipo tayari kuwa mshenga wako,iwapo utapenda
 
Muoe kwani ndoa ni ya wawili. Pia nyie sio ndugu. Ila ndio vizuri umelipiza kisasi cha baba yako usikute uyo Jamaa ndio sababu ya baba yako kuachwa na mama yako.
Ngoja tuone mkuu hisia zangu zikidi akili nitajua nafanya nini

Na chengine naangalia na maoni kama ya kuona niko sawa yapo mengi hata kama sio sawa hili jambo sina budi kufanya vile nilivyokusudia maana nipo kwenye denial

Naangalia mzani lakini bado hisia zimenitawala
 
Yaani we acha tu just imagine toka tuna miaka 17 .Mapenzi kajifunzia kwangu na mimi mapenzi nimejifunzia kwake. Mwanzo tulikuwa tunafurahia mchezo tukasema tutaacha

Baadaye ndio hivyo hisia zikajiingiza. Tulijaribu kuwa na mahusiano tofauti tukashindwa maana tulianza kuoneana na wivu na kuumia tu
Mimi kwakweli siwalaumu kabisa mapenzi ni upuuzi mno dah Muombeni tu Mungu awasaidie
 
Kimaadili si sawa na si sawa hata mbele za Mungu pia, maisha mliyoishi hayakua sahihi na ndio maana mlifanya siri. Pia hujui kwa nini mama yako aliachana na huyo baba yako wa kambo. In short mahusiano hayo ni batili mbele ya Wazazi wenu, Mbele ya Jamii na Mbele za Mungu pia. Sitisha haraka sana na upate msaada wa kiroho kwa watumishi wa Mungu maana hiyo inaweza kuja kuwa sababu ya laana kwa maisha yako na watoto wako baadae.
Sawa kiongozi [emoji120]. Pengine nahisi pia nahitaji msaada wa kisaikolojia.
 
Ni kweli lakini huyo sio mwanamke wa kawaida ni dada wa kambo
sumu ya penzi ukishailamba hata kwa maziwa huwezi kupona...
Kuachana itakuwa ngumu sana na kuendelea pia ni vibaya hapo ndio pagumu mkuu
 
Hilo suala wazazi wenu hawatakuwa tayari.
Baba wa huyo dada yako alikulea kama mtoto wake, namama yako akamlea huyo binti kama mwanae, hii mnaleta aibu kwa wazazi wenu na jamii nzima.

Usije kushangaa wazazi wakawalaani mkijifanya mnapendana sana na kutowasikiliza.
Kama mtaendelea kulana kimasikhara endeleeni ila suala la kuoa, utamfanya mama yako akuone ni mtoto mjinga na huna akili.
Kama wanapendana waoane tu, kwanza mpaka hapo tayari washaoana.
 
Ipo ndio kama hivyo tumependana na tumeshindwa kuwa na mahusiano na watu wengine
Tayari Mna Mahusiano Tangu Na Tangu Mnahitaji Mahusiano Na Watu Wengine Ya Kazi Gani??Boresheni Mahusiano Yenu Yenye Muunganiko Murua Na Historia za kuupa Moyo Furaha Na Amani Kila Mnapofanikiwa Kuwa Pamoja,,Let Love Lead,,,Msijibane Nyie Si Ndugu,,Ipeni Na Ionyesheni Dunia Pendo Lenu Lilivyomea Kwa Huba Na Hisia Bora Za Mapenzi.
 
Subirini wazazi wenu wafariki hafu muoane
Hili ni wazo zuri lakini kusubiri mpaka mzazi afe na umri ndio hivyo unakwenda je wasipotangulia nikifa mimi

Lakini bado huyo binti ana ndugu watachukuliaje hili swala unajua baba yake akikubali sitasemwa mimi tu hata wazazi watasemwa au kutengwa kwa nini wamekubali kidogo nahisi uzito wa jambo utapungua maana nitakuwa na support

Yaani hizi akili hizi saa nyingine nawaza hivyo
 
Kama wanapendana waoane tu, kwanza mpaka hapo tayari washaoana.
Sio kuoana tu, mfano nikuulize, wewe utakubali rafiki yako wa karibu aje kuoa mke wako uliye achana nae na umeishi nae kwa miaka na mlipata mtoto? kwa sababu mliachana na hakuna mahusiano ni sawa rafiki yako wa karibu aoe x wife wako? na je? utabariki hio ndoa pasipo shingo upande?

Marafiki wa kiume huwa wanatofautiana kupigiana ma ex na ushikaji hadi unakufa, sasa vipi kwa wazazi kuona wanao wanaoana?
 
Ndugu..jitahidi kuweka hisia pembeni - wewe hasa kama mwanamme. Yaani baba yake kamlala mama yako, na wewe unamlala mtoto wake..jamani...Hizi ny-e-g mshindo vipi?? Ukiona unafanya kitu lkn huna amani au unawasiwasi mpaka unaanza kuuliza watu ujue tayari nafsi yako iliishakuambia sio sawa - tii hiyo sauti...utamletea aibu mama yako....
 
Hakuna kosa kumpenda dada wa kambo na unaweza kumuoa bila kikwazo,msijiumize bure halalisheni uhusiano wenu,mie nipo tayari kuwa mshenga wako,iwapo utapenda
Yaani pamoja na kuandika huu uzi sipo tayari kumuacha na yeye hayupo tayari kuniacha mzani wa maoni ukizidi upande wangu sitajali chochote nitafanya nilichokusudia


Nipo kwenye denial mkuu na maoni ya huu uzi ukichanganya na hisia zangu mda si mrefu nitapata ujasiri wa kufanya kile ninachokusudia
 
Yaani pamoja na kuandika huu uzi sipo tayari kumuacha na yeye hayupo tayari kuniacha mzani wa maoni ukizidi upande wangu sitajali chochote nitafanya nilichokusudia


Nipo kwenye denial mkuu na maoni ya huu uzi ukichanganya na hisia zangu mda si mrefu nitapata ujasiri wa kufanya kile ninachokusudia
Kwa mila za kiafrika hakuna dosari,muoane haraka,hiyo ndio destiny yenu,ni Mola ndio kawakutanisha
 
Ndugu..jitahidi kuweka hisia pembeni - wewe hasa kama mwanamme. Yaani baba yake kamlala mama yako, na wewe unamlala mtoto wake..jamani...Hizi ny-e-g mshindo vipi?? Ukiona unafanya kitu lkn huna amani au unawasiwasi mpaka unaanza kuuliza watu ujue tayari nafsi yako iliishakuambia sio sawa - tii hiyo sauti...utamletea aibu mama yako....
Ni kweli . Natamani ningepata wengi wakunipa maneno haya ya ukweli na uchungu maana hata kwa akili ya kawaida mahusiano yangu sio sawa kuendelea kuyaamini nazidi kujiumiza
 
Back
Top Bottom