Mahusiano ya mtandaoni

1: Tulikutana watsup kwenye group la vijana la dini ilikuwa mtu akijoin unajitambulisha na kutuma picha… nakumbuka tulijoin siku moja tulipishana masaa yeye alijoin saa6 usiku mimi nikajoin asubuhi mida kama saa 3 hivi

Basi bhn nilivyotuma picha yangu kama kawaidia kwenye msafara wa mamba na kenge hawakosekani zikajaa sms za wakaka inbox kila mtu ananiulizAA kweli umeokokaa mara unasali wapi wengine hapo hapo wanataka kunioa

Usiku wa siku ile nikafungia sms ya huyo kijana alituma tu sms ya kuniita jina langu Mamamzungu basi tukawa marafiki kama mwezi mmoja baadae akanambia amenipenda anataka kunioa[emoji19][emoji19] ..Huyu nilionana nae live mara mbili tu nyie likaka lilikuwa lizuri limasaii basi bhn tukadate almost 2 yrs tukaja kubreak sababu za kipumbavuu niliumiaa kichizi,, sema alikuwa bahili sanaa

2: Huyu nae tulifahamiana kupitia watsup kwenye group la dini mimi nilituma sms kuna mtu nilitaka anitafute si akanitafuta yeye inbox [emoji23][emoji23] Huyu nimeonaa nae mara nyingi mpk kwake nimefika mara nyingi mno sema ni Kabahili pesa anayotoa ni nauli yupo Radhi atoe nauli ya kigoma-Dar kuliko kukutumia hela ya vocha … Kwa sasa hivi ni kama hatuna mahusiano

3: Huyu bhn ndio laazizi wangu tulikutana Facebook… siku ya kwanza kuonana nae nilikuwa naogopa balaa kwanza nilikuwa naogopa asije akanikimbiaa labdaa siendani na picha zangu…. Mmmh Alichonambia ni mzuri kuliko picha sema ni mfupi[emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Anyway nina mwaka wa3 na kijana wangu wa facebook mambo ni yenteyente nampenda mnooooooo
 
wangu tulikutana hapa jf,first time tunakutana tulikuwa ilikuwa nikama watu waliojuana kwa miaka an it's all b'coz ya uhuru tuliokuwa nao,kuwekana wazi,mawasiliano mazuri,tulijiachia sana japo nikupitia simu ila ilifanya tukazoeana zaidi na nakurudhiana!!siku tulipoonana ana kwa ana tuliishia kutimiza wishes zetu zote na ilikuwa nisiku yakipekee kuwahi kutokea,,namshukuru mungu sasa ni mume wangu,itoshe tu kusema nampenda sana baba T
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]kwanini sasa umemtaja jina
 
Me tulikutana marafiki.com enzi hizo sasahivi ni mume wa ndoa 10years, kwa kweli sijawahi juta kukutana na huyu kaka, it was fate. Japo halikuwa lengo langu kuwa na mtu kutoka kwenye mtandao na nilikuaga naponda sana hilo swala jamani maisha haya😛, kweli usitukane mamba kabla hujavuka mto 😀 na kwenye profile yangu niliandika nina mahusiano so nisisumbuliwe, na nilikuaga sijibu msg za dm wala sizisomi nikifungua nafuta zooote. Sasa kuna jina lilikuwa linajirudia sana, yani kila nikisema nifungie kufuta msg lazma nione msg yenye hilo jina, siku moja nikaamua kufungua msg yake, nikakuta salam tu, nikaijibu then nikafuta, sasa ikawa kila nikifungua lazma nikute kanisalimia, na mimi najibu salam basi. Siku moja akaniomba namba ya simu nikamwambia sina simu, alijua nimemdanganya ila hakulazimisha tukaendelea na salam tu dm, kuna kipindi akapotea i ddnt bother kumtafuta nikamsahau. Akaja akaibuka tena, akaniomba tena namba nikakataa tena, akaomba atleast email address, hiyo nikampa, enzi zile za yahoo messenger, so tukawa tunawasiliana huko japo si sana, mana hakuwa muongeaji sana, tukaenda hivyo for almost a year, akaniomba tena namba ya simu akasema hii ni mara ya mwisho kama kweli sina simu yuko tayari kununulia ila kama namnyima tu namba basi hatanisumbua tena kuhusu hilo, baada ya siku 2 nikampa namba, mawasiliano yetu yakaanzia hapo,it took me 6 months kukubali kuonana nae, mana nilikuaga muoga sana. But that day nilipokutana nae, katika kuongea akaniambia i will marry you next year tarehe fulani na mwezi fulani, i thout he was joking. But he wasnt joking, kweli mwaka uliofuatia tarehe ile ile na mwezi ule ule aliosema tukafunga ndoa Takatifu pale St. Joseph, and it has been an amaizing 10 years of marriage. Bcz he is everything i ever wanted, huwa nasema ni Mungu tu sio hivi hivi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…