Maisha ni kitendawili...wengi hufa bila kutegua...

Maisha ni kitendawili...wengi hufa bila kutegua...

ha haa life is funny DC
siku zote watu 'they want what they cant have'
hata kama ni upuuzi tu


Hata mie huwa sielewi huyu kiumbe binadamu kaumbwaje...ukimpa vitu vizuri yeye ndipo anahangaika kutafuta maji taka!!

Anyway, ngoja niendelee kukaa kimya labda nitajifunza kitu zaidi....nipate mafuta ya kuzipaka hizi mvi zangu!!

Babu DC!!
 
Kweli maisha ni kitendawili
na leo nimethibitisha wengi hufa bila kutegua.....

hebu fikiria hiii

kuna wanawake na wasichana wangapi
ambao pengine walikuwa wako tayari kumpa 'faraja na amani na mapenzi ya kweli Kanumba'?

watakuwa ni weengi mno...maelfu na maelfu na mamilioni labda...

but tazama wanawake waliokuwa katika maisha yake

Wema Sepetu na wengine..
na mwisho akafia kwa kitoto Lulu.....

utasema hakuwahi 'kupendwa kikweli kweli na na mwanamke wa maana'

yet kuna miliions walikuwa probably wanamtaka.....awe their man forever....

maisha ni kitendawili......kikubwa....

inawezekana wewe au mimi pia tunahangaika kila siku na 'wapenzi wetu full micharuko'
hadi tunakata tamaa while kuna maelfu kila siku wanakutazama na kimoyomoyo wanasema
'ningempata mimi yule' dah....

mwisho siku ukifa ndo wanalia hadi kuzimia.....while ulipokuwa hai...
walishindwa tu namna ya kukusogelea na kufunguka labda.....
au walikusogelea ukashindwa kuwatambua ukachagua micharuko

think about it..........
kweli lakini ni ngumu kuwajua maana binadamu ni walewale tofauti ni majina tu
 
The Boss
Siku zote maisha ni kitendawail Tegua
Maisha ni mtihani -kabiliana nao.
Mapenzi hayaeleweki ..huwezi jua nani anakupenda kweli na nani hakupendi
Unayedhani anakupenda anaweza kuwa anakuenjoy
Lakini mwisho wa yote ni mauti .
 
inawezekana wewe au mimi pia tunahangaika kila siku na 'wapenzi wetu full micharuko'
hadi tunakata tamaa while kuna maelfu kila siku wanakutazama na kimoyomoyo wanasema
'ningempata mimi yule' dah....

mwisho siku ukifa ndo wanalia hadi kuzimia.....while ulipokuwa hai...
walishindwa tu namna ya kukusogelea na kufunguka labda.....
au walikusogelea ukashindwa kuwatambua ukachagua micharuko

think about it..........


Acha tu...hiyo mbaya sana unampenda mtu na yeye hajui au hakuoni kama upo. The other side of story, kama haujasema au tamka vipi mlengwa atajua kama unampenda. Inataka mfalme njozi kujua.


Kanumba was hanging with birds of the same feathers, so I was not expecting he would have someone different.
 
Na hivyo ndivyo maisha yanavyopaswa yawe. Ndiyo maana idadi kubwa ya wanaume wanaishi na wanawake wasiowapenda but ndiyo waliokuwa available wakati wanatafuta wake wa kuoa, na kuna wanawake wanaoishi na wanaume wasiowapenda but ndiyo waliowatokea wakati huo wakiwa wanawatamani wengine. Na wapo pia ambao wameshindwa kabisa kuolewa au kuoa kutokana na kuendelea kumfikiria fulani na kuwakataa wote wanaojitokeza mbele yake. So huu ndiyo mfumo wa maisha ulivyo. Huwezi kuutegua.

Hapo umesema ukweli mtupu, hasa wanawake inawalenga hii as long as kachaguliwa hata jamaa hafai au haelekei anajikubalia tu. Mwishowe, unhappy married!

Na hapo kwenye bold ndio mbaya zaidi ni kama prison hivi, ni bora usioe/usiolewe waiting for the best match but not fulani
 
the boss
siku zote maisha ni kitendawail tegua
maisha ni mtihani -kabiliana nao.
Mapenzi hayaeleweki ..huwezi jua nani anakupenda kweli na nani hakupendi
unayedhani anakupenda anaweza kuwa anakuenjoy
lakini mwisho wa yote ni mauti .
unaempenda,hakupendi wala hajui kama unampenda,anaekupenda humpendi wala hutaki kumuona
anaekupenda mwingine hata humjui
full mcharuko
 
ni kweli mkuu ... mapenzi ni upofu na nafasi . wenye mapenz halisi hawakuwa a afasi ya kumfikia na ndo maana alizugukwa na wa aina ya temporary with somethin
 
oss, hakuna binadamu yeyote aliyewahi kutegua kitendawili cha maisha:yell:
 
unaona smile kama mungu siku moja angefua mioyo yenu na kuonyesha tunayoyawaza mmmh...mambo yangekuwa sio mambo..
mapenzi ni kitu cha ajabu sana
feelings? Achana nazo.unaweza kukaa na mtu basi tu umfeel wala nini,but i love u baby ni kwa sana mmmh angejua?
 
mapenzi ni kitu cha ajabu sana
feelings? Achana nazo.unaweza kukaa na mtu basi tu umfeel wala nini,but i love u baby ni kwa sana mmmh angejua?

yaani huu moyo...kweli ni afadhari huwezi kusoma mawazo ya mtu..tungechanganyikiwa
 
The Boss,
Umeona kitu ambacho sikukifikiria. Unajua mazoea mabaya. Ukishaanza na mmoja mzuri ukammwaga, akaja mwingine ukafanya hivyo hivyo, then unajenga katabia kuwa hiyo ni kitu ya kawaida.Kwa bahati mbaya wengine kufunguka pale wanapofikiria wamefika ni kitu kigumu. Na kweli maisha mara nyingine tunashindwa kutegua kila kitendawili kinachopita karibu yetu.
 
unaempenda,hakupendi wala hajui kama unampenda,anaekupenda humpendi wala hutaki kumuona
anaekupenda mwingine hata humjui
full mcharuko

Yaani kama Mungu angekua anatuonyesha tu huyu anakupenda kiukweli naona ingesaidia,maana unaweza kumkataa mtu aliyekudondokea kwa mapenzi ya dhati lakini ukamuona muongo anakuyeyusha tu,matokeo yake unaenda kuangukia pua kwa jamaa ambae shida yake ilikua kupita tu......kitendawili kigumu sana hiki.
 
mie sitakusukuma ila nina chupa ya jack daniels....karibu.

Poa basi. Nikukute kwa Bed. Naenda kuoga. No simu toka kwa Pedeshee wala Dushelele wala Serengei Boys. Nina wivu miye. Patachimbika na Kitanuka . . . We haya wee . . . .

Halafu kuna mwingine ananipenda humu, anaona aibu kusema au kujitokeza. halafu nikifa machozi kibao . . . nitakuja kuamka nimtie mtu viboko, shauri yenu.

Jitokezeni wooooote mapemaaaa . . . lol (Jokes wandugu)
 
ukitaka furaha usimwamini mtu usiweke akiba yote ya mapenzi kwa mtu bakisha kidogo

Mmhh smile mpenzi mimi hapa nakataa ni bora tu ujitoe mzima mzima maana ukisema ubakishe hiyo ingine utampa nani?utatafuta wa pembeni au?
Seriously, kama umempenda mtu kutoka moyoni na ukamuamini huwezi kujizuia am telling you yaani hiyo habari ya kubakisha utaisahau. Ukiamua kuwa mguu mmoja ndani mmoja nje basi ujue huyo hajakuingia kumoyo....lol
 
Back
Top Bottom