Uzi huu nime uandika ili uwe Kama kengele ya ukumbusho, kwa kila mmoja wetu.
πMaana kumezuka na Mambo ambayo yame kuwa Kama kikwazo, kwa baadhi ya watu katika safari ya maisha yao.
WIVU, kila mmoja wetu ana wivu katika maisha yake.
πIla baadhi ya wengi wetu tumekuwa na wivu ambao si rafiki katika maisha haya.
πUme ona mtu kajenga au ana kazi nzuri kukuzidi, mzee Pambana ufikie Malengo yako, jiulize yeye kafikaje hapo??. Zidisha juhudi na SI uchawi na husda.
SUALA LA MAPENZI, hapa ndo kama wabongo wengi tulipo rogwa, Kama Kijana una mengi ya kuzingatia katika maisha yako.
πUSI kubali kuyumbishwa au kupoteza muda wako, eti kisa kiumbe mwenye manyoya mwili mzima.
πKama uhusiano huo si rafiki basi achana nao mzee, Kumbuka una mengi na watu wengi Wana kutegemea wewe mpendwa.
AMINI KATIKA WAKATI SAHIHI, ndugu haya maisha Kuna watu tuna jipa stress za kipuuzi Sana.
πEti kisa fulani ana kazi au maisha mazuri, una Anza kuji ona wewe kama bwege uliye kosa mwelekeo.
πIna kupasa uzingatie katika barabara yako, na si njia ya mwingine.
πKama biashara haiendi vizuri, basi Tafuta namna ya kutafuta wateja, kwa maana Hakuna kitu kina kuwa kwa usiku mmoja.
-learn how to hold
-learn the right time to fold
-learn the right time to let go.
π I MEAN NO MALICE TO NOBODY
View attachment 2760528