Maisha sio muhimu na bora kama uzima

Wewe umechukua mistari baadhi, na kwa sababu hiyo umepotosha wazo zima la andiko lenyewe: andiko au ujumbe unawahusu akina nani.

Ungeanza kusoma kuanzia Rum 8: 31-39.
Kama nimepotosha, ni haki yako kusahihisha. Kukosoa bila kusahihisha haina afya katika kujifunza
 
Uko sahihi kwamba Mungu anakaa kwenye Moyo ulio safi.

Je unaweza kufaulu kuwa na moyo safi kama Mungu akiangalia shughuli na juhudi za maisha yako? Kama jibu lako ni NDIYO basi endelea kufanya juhudi ili uwe msafi.

Kama jibu ni HAPANA, basi kubali kuwa kwa juhudi zako huwezi kuwa safi hivyo huwezi kuwa pamoja na Mungu na hivyo mwisho wako ni mauti.
Na itakupasa utafakari kuwa "Kama juhudi zako haziwezi kukufanya uwe msafi wa Moyo, je ni nini kinacho safisha moyo wa mtu?"

Kutambua kuwa kwa matendo yako utapata uzima ni kujikweza na kufanya msalaba wa Yesu ukose maana. Hebu jiulize kama kwa matendo yetu tunaweza kuokoka na kuwa na uzima basi yeye alikufa ili iweje?
 
Kutambua kuwa kwa matendo yako utapata uzima ni kujikweza na kufanya msalaba wa Yesu ukose maana. Hebu jiulize kama kwa matendo yetu tunaweza kuokoka na kuwa na uzima basi yeye alikufa ili iweje?
Hakuna mtu ambaye hawajibiki au hatawajibika. Yesu hakuja duniani au hakufa msalabani, ili kuondoka hilo.

Kwa hiyo, kifo cha Yesu msalabani, hakimuondolei mtu uwajibikaji. Kila mtu atawajibika kadiri ya matendo yake.

Yesu Kristo, kwa kuja kwake duniani, mafundisho yake, matendo yake, mateso, na kifo chake msalabani, amemrejeshea mtu haki yake ya asili (origin justice) aliyoipoteza kwa dhambi.

Kifo cha Yesu msalabani hakiondoi wajibu.
 
Uzima una viambata au inputs ambazo ndo hizo harakati ulizozitaja.Hapo vitu vyote vinategemeana
 
Jibu hilo swali...

Je unaweza kufaulu kuwa na moyo safi kama Mungu akiangalia shughuli na juhudi za maisha yako?
 
Ndio. Ninaweza
Kwa kuwa nia ya mwili ni mauti; bali nia ya roho ni uzima na amani. Kwa kuwa ile nia ya mwili ni uadui juu ya Mungu, kwa maana haitii sheria ya Mungu, wala haiwezi kuitii.
Rum 8:6‭-‬7 SUV

Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu; wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu.
Efe 2:8‭-‬9 SUV

Kwa matendo yetu hatuwezi kupata haki. Mungu ametuumba ili tutende matendo mema na ni asili yetu kutenda mema, Lakini mwili wetu hauwezi kutenda matendo mema kama tusipokiri kuwa wokovu/uzima wetu si kwa matendo.

Tukikiri kuwa tumeokolewa si kwa matendo yetu, ndipo Mungu anachukua nafasi ya kuongoza maisha yetu na hivyo matendo mema tutayatenda si kwa sababu ya kuokolewa kwetu bali ni kwa sababu ya roho wa Mungu atakaeishi ndani yetu baada ya kukiri kuwa kwa juhudi zetu hatuwezi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…