Maisha ya mfungwa anayesubiri kunyongwa gerezani

Maisha ya mfungwa anayesubiri kunyongwa gerezani

Hivi punde

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2017
Posts
2,554
Reaction score
8,587
Anasema wafungwa ambao wanasubiri kunyongwa kwa siku hupewa dakika 15 tu za kutoka nje na muda mwingi hubaki ndani.

“Kwa kuwa wanakuwa wengi gerezani, basi kuna baadhi wanaweza kukaa muda mrefu bila kuona hata jua na baadhi wamefikia hatua ya kuchanganyikiwa kutokana na msongo wa mawazo,” anaeleza.

Kwa mujibu wa Moringe, kila anapokumbuka matukio hayo, hupatwa huzuni hasa anaposikia mtu amefanya mauaji dhidi ya mwingine kwa sababu yoyote ile ikiwamo wivu wa mapenzi.

“Kama utashuhudia maisha ya gerezani kwa watuhumiwa wa mauaji, sidhani kama utathubutu kuua mtu, kwani damu ya mtu haiwezi kupotea bure ni lazima utajutia tu.

“Ukiwa kule mwisho wa kukaa macho usiku ni saa tatu hivyo unapaswa kuwa kimya na kulala japo unalala katika kipande cha blanketi moja umetandika chini na jingine unajifunika.

“Nakumbuka kutokana na upweke na kuchanganyikiwa, kuna wakati ulitokea ugomvi, mfungwa mmoja kudai wenzake wanamloga hivyo, kuanza kupigana hadi viongozi wa magereza wakajitokeza na kutoa adhabu,” anasema.
 
Niliwahi kuingia gereza moja mkoa fulani, nilifuata nini huko sikumbuki, yaani kupita mpaka ukute wafungwa ilikuwa siyo kazi ndogo.

Nakumbuka nilipelekwa sehemu wanapokaa yaani kwenye kieneo wapo wafungwa wa kunyonywa na mahali fulani hivi wapo wafungwa wa kifungo cha maisha.

Was bad feelings ever,
 
.

“Nakumbuka kutokana na upweke na kuchanganyikiwa, kuna wakati ulitokea ugomvi, mfungwa mmoja kudai wenzake wanamloga hivyo, kuanza kupigana hadi viongozi wa magereza wakajitokeza na kutoa adhabu,” anasema.
Kaingiaje na uchawi gerezani wakati wanapekuliwa hadi Togo?
 
Najaribu kuvuta picha wanatamani ata wawe wafungwa wa kawaida huko wanaume wanageuzana. Wanataman kufa lakini haiwezekani. Damu ya mtu kweli haipotei buree.
 
Kuna njia nying za kutoa mafunzo na kumfanya mtu ajutie makosa yake hata life imprisonment iangaliwe...watunga sheria binadamu hajakamilika ila daah soma kama story mtandaon usiombe yakukute

but me i don judge nasubiri siku kuona majaji watakapo kujakujajiwa na God
 
Bora wawanyonge tu ieleweke sio kuwaweka watu wanaishi kwa hudhuni na mateso hata Miaka 40 anasubiri hukumu isiyo tekelezeka
 
Maweni, Tanga... kuna siku nilipita kuzurura huko hali sio nzuri kabisa.
Wasambaa wanaliogopa hilo gereza mpaka basi. Wengi wanaona bora wakizingua, basi wapelekwe gereza la Korogwe. Ila siyo Maweni.

Sijui lina changamoto gani hili gereza! Maana lipo barabarani, na siyo mbali kutoka Tanga mjini.
 
Inasikitisha sana, tatizo binadamu wa siku hizi ni wabishi sana...
 
Bora wawanyonge tu ieleweke sio kuwaweka watu wanaishi kwa hudhuni na mateso hata Miaka 40 anasubiri hukumu isiyo tekelezeka

Kauli yako ni kwa sababu huna ndugu aliyehukumiwa kunyongwa na wala sio wewe uliyehukumiwa kunyongwa.

Kufa sio jambo rahisi usirahisishe
 
Wasambaa wanaliogopa hilo gereza mpaka basi. Wengi wanaona bora wakizingua, basi wapelekwe gereza la Korogwe. Ila siyo Maweni.

Sijui lina changamoto gani hili gereza! Maana lipo barabarani, na siyo mbali kutoka Tanga mjini.

1. Maximum security

2. Ukiingia umeingia na sio rahisi kupata interaction na watu nje

3. Kazi zinakuwa ngumu kama kupasua mawe, kuponda kokoto n.k
 
Back
Top Bottom