Maisha ya Musa: Utata wa kifo, mazishi yake na ufanano wa viongozi wa kiharakati Karne ya 21

Maisha ya Musa: Utata wa kifo, mazishi yake na ufanano wa viongozi wa kiharakati Karne ya 21

mugah di matheo

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2018
Posts
6,307
Reaction score
12,410
Habari za muda huu jf.

Tuanze moja kwa moja,tutatumia bibilia as reference pindi itakapohitajika Kama msingi kwakuwa ndio kitabu nikisomacho.

Nabii Musa ni Nani?
Maisha yake yanaelezewa kwenye kitabu Cha kutoka katika bibilia Kama mtoto aliezaliwa na wazazi waebrania lakini alilelewa katika kasri la ufalme wa misri.
Baadae anageuka kuwa mwanaharakati wa kutetea waebrania hadi anajikuta kaingia kwenye matatizo yaliyopelekea kukimbia nchi Kama vile tundu Lissu anavyofanya saivi (kutoka 2:15)

Alivyorudi toka uhamishoni midiani akawa mwanaharakati zaidi hata ya Bobby wine ama Samora machielle wa Mozambique hadi kufikia hatua ya kumega idadi kubwa ya watu katika kile kinachoitwa "kutoka misri kwenda nchi ya ahadi"

Baada ya miaka 40 ya huku na huku jangwani ,Siku ya kifo Cha Musa ilifika na aliarifiwa akafanya mchakato wakumpata mrithi wake na kumkabidhi madaraka (demokrasia), akapanda hadi mlima nebo.

Utata unaanzia hapa
Alipanda hadi mlima nebo akafa akiwa mwili wake hujapungua Nguvu(kumbuk 34:7)
Akazikwa na bwana na hakuna anaejua kaburi lake (34:5-6)

Je kwanini mungu alimtenga Musa na watu wake kabla ya kifo chake? alitaka wasione Nini?
Wengine wanaamini Musa hakufa bali alipazwa kwenda mbinguni kwa kuwa Yesu aliwahi kutokewa na Musa na eliya ambapo tunatambua Eliya hakufa hivyo wanasema Musa nae hakufa ndio maana alimtokea yesu (Marko 9:4).

Wengine wanaamini alikufa Ila mwili wake ulilindwa Sana na mungu (yuda 1:9).

Maswali yangu kwenu wanajamvi.
Je kaburi la Musa liko wapi?
Je Kuna jitihada zozote za kulitafuta?
Je kwanin Mungu alilificha hilo kaburi?

Nyongeza :hatujui lilipo kaburi la Gadafi Wala Osama bin laden.

2.kutokuaminika kwa chanzo Cha vifo vya viongozi wa Afrika Kama Jiwe na Nkurunziza je Kuna uhusiano na kisa hiki Cha Musa?

Asanteni karibu kwenye mjadala.
 
Ushahidi wa kifo cha Musa upo hapa:
Yuda 1:9
[9]Lakini Mikaeli, malaika mkuu, aliposhindana na Ibilisi, na kuhojiana naye kwa ajili ya mwili wa Musa, hakuthubutu kumshitaki kwa kumlaumu, bali alisema, Bwana na akukemee.
_____________________________________

Mwili wa Musa maana yake ni Maiti ya Musa
 
Musa alitwaliwa na Mungu Mwenyewe ile chata nyingine kabisa !! baaasi na huyu yeye ni miongoni mwa wazee 24 waliokizungukakiti cha enzi!! na huyu kamwe usimlinganishe na

vichaa wa shetani km jiwe!!...kaburi lake si liko chato pale nenda kaliliepo hapo weee na weye uendemotoni! ni kawaida ya shetani huwa anajifanya eti kutwaa wateule wake km Mungu anavyo fanya! mwee!

jamaa hilo shetani kwa kuiga asee ni kiboko!......Mungu kamtoa mwanae wa pekee na yeye devil huyooo kamtoa mzungu wake wa pekeee! mrembooo! nywele mpaka mgongoni!!..eti yule abebe msalaba!! si utani huo??

Yesu alikuwa mzizi mkavu mgumu!! ajuaye sikitiko!!! ukisikia alibeba msalaba alibeba kweli si utani!
 
Habari za muda huu jf.

Tuanze moja kwa moja,tutatumia bibilia as reference pindi itakapohitajika Kama msingi kwakuwa ndio kitabu nikisomacho.

Nabii Musa ni Nani?
Maisha yake yanaelezewa kwenye kitabu Cha kutoka katika bibilia Kama mtoto aliezaliwa na wazazi waebrania lakini alilelewa katika kasri la ufalme wa misri.
Baadae anageuka kuwa mwanaharakati wa kutetea waebrania hadi anajikuta kaingia kwenye matatizo yaliyopelekea kukimbia nchi Kama vile tundu Lissu anavyofanya saivi (kutoka 2:15)

Alivyorudi toka uhamishoni midiani akawa mwanaharakati zaidi hata ya Bobby wine ama Samora machielle wa Mozambique hadi kufikia hatua ya kumega idadi kubwa ya watu katika kile kinachoitwa "kutoka misri kwenda nchi ya ahadi"

Baada ya miaka 40 ya huku na huku jangwani ,Siku ya kifo Cha Musa ilifika na aliarifiwa akafanya mchakato wakumpata mrithi wake na kumkabidhi madaraka (demokrasia), akapanda hadi mlima nebo.

Utata unaanzia hapa
Alipanda hadi mlima nebo akafa akiwa mwili wake hujapungua Nguvu(kumbuk 34:7)
Akazikwa na bwana na hakuna anaejua kaburi lake (34:5-6)

Je kwanini mungu alimtenga Musa na watu wake kabla ya kifo chake? alitaka wasione Nini?
Wengine wanaamini Musa hakufa bali alipazwa kwenda mbinguni kwa kuwa Yesu aliwahi kutokewa na Musa na eliya ambapo tunatambua Eliya hakufa hivyo wanasema Musa nae hakufa ndio maana alimtokea yesu (Marko 9:4).

Wengine wanaamini alikufa Ila mwili wake ulilindwa Sana na mungu (yuda 1:9).

Maswali yangu kwenu wanajamvi.
Je kaburi la Musa liko wapi?
Je Kuna jitihada zozote za kulitafuta?
Je kwanin Mungu alilificha hilo kaburi?

Nyongeza :hatujui lilipo kaburi la Gadafi Wala Osama bin laden.

2.kutokuaminika kwa chanzo Cha vifo vya viongozi wa Afrika Kama Jiwe na Nkurunziza je Kuna uhusiano na kisa hiki Cha Musa?

Asanteni karibu kwenye mjadala.
Kaburi la Ghadafi na Osama linajulikana maana hatma yao ilikuwa mikononi mwa wachache waliowakamata.
Hivyo huwezi kuwafananisha na Musa.

Musa alikozikwa anajua Mungu, Malaika na Shetani.

Nadharia nyingi zinaonyesha ilifanyika hivyo ili asijekuabudiwa. Maana watu wale wayahudi walikuwa wachanga Sana kiroho. Kama waliabudu ndama kumuabudu Musa ilikuwa Jambo ndogo.


Ni kweli alikutana na Eliya na Yesu mlimani maana Kitabu cha Yuda kilipokuwa kikielezea matukio yaliyopita kimetaja Musa kuja kuchukuliwa na Malaika (Mwili wake/Kufufuliwa).
Hivyo alifufuliwa
 
Back
Top Bottom