Maisha yamekuwa magumu sana huku uswahilini kwetu. Ninatamani hata kuuza hii Taxi bubu yangu (Chase Avante GX-100) nifungue walau pub ndogo


Nilifungua kibar kidogo Sana wateja wakasuasua , sasa nimeweka banana walau napata 5000 toka kreti mbili kwa siku.

Mitano Tena.
 
Bajaj ni bei ya gar mkuu inakaribia 8M kama una passo ukikutana na bajaj pak pemben apite maana anaendesha chombo ya gharama kuliko yako[emoji3]
Waaaaaaaaaaahhhhhhh[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2]
 
maisha yamekuwa mepesi na rahisi kuliko zama zote, kila unacho kitaka kwa kipindi hiki unakipata tena kwa bei nafuu kabisa, bei ya mazao safi kabisa, pembejeo bei ya punguzo,
kilimo kinalipa.
ukikaa bila kujishughulisha kweli utakufa kwa njaa lkn ukijishughulisha maisha rahisi kabisa kama unakunywa maji.
wanao lia hali ngumu ni wavivu wa kazi na watu wa madili
 
Da pole ndugu yangu, tax now days zinachangamoto sana. Utandawazi umerahisisha viusafiri vya haraka, tax inaonekana old school pia tax ni gharama ukilinganisha na bajaji na boda kwa sababu ya mafuta inayo consume.
Ina-consume mafuta mengi lakini zamani nilikuwa ninapata faida kwa kiasi fulani tofauti na sasa...
 
yani ununue babaji milioni 7 ili dereva akuletee sijui 20,000 kwa siku mpaka upate faida cjui lini hapo una-assume haijaharibika ,haijakamtwa,hujaibia spare,haijapata ajali ,mwendo wa presure tu
Asa Milioni saba si bora anunue Vitz..[emoji853]
 
Ni kweli mkuu mfano bodaboda wateja wao wakubwa ni wadada ,,Bajaj ni mchanganyiko hasa wamama wa sokoni,wanaume kama hana gari au pikipiki yake binafsi ni aidha atakuwa na baiskeli hasa wa mjini kufanya shanting za hapa na pale ila kupanda Bajaj ni kwa shingo upande
 
Uza nunua bajaji.

Lazima ujifunze kuishi baharini na nchi kavu. Na uwe unabadirika kulingana na mazingira kama kinyonga.
Sawa kaka mkubwa. Ninakushukuru sana kwa ushauri wako mwanana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…