Maisha yamekuwa magumu sana huku uswahilini kwetu. Ninatamani hata kuuza hii Taxi bubu yangu (Chase Avante GX-100) nifungue walau pub ndogo

Na bado huu ni mwanzo tu. Miaka hii mitano ijayo hali ya kiuchumi Nchini itakuwa mbaya sana kuliko wakati wowote tangu tupate uhuru na kama una vijisenti vyako benki viondoe maana yanaweza kuwekwa masharti ya kutoa pesa benki na hata baadhi ya benki zinaweza kufilisika. Akili mkichwa.
 
Mhhh
 
Hivi hii biashara ya taxi bado ipogo?
Uza hiyo,nunua bajaji moja na nyingine mfungulie mamaz ki streetshop
 
Hujawahi hata kufanya biashara ya mgahawa wewe. Hakuna biashara ngumu kama mgahawa.
 
Mkuu hili gari ni lako au la huyo jirani yako?
 
si umisema maisha uswazi ni magumu.. sasa hiyo PABU ukifungua utapata walevi wakati hawana kitu AROSTO
 
yani ununue babaji milioni 7 ili dereva akuletee sijui 20,000 kwa siku mpaka upate faida cjui lini hapo una-assume haijaharibika ,haijakamtwa,hujaibia spare,haijapata ajali ,mwendo wa presure tu
Hiyo 20,000 kwa siku ndiyo faida yenyewe, of course ukitoa gharama za uendeshaji. Million 7 ndiyo mtaji wenyew. Kwa maneno mengine faida inatengenezwa siku bajaj inaanza kuoperate, na siyo eti faida ni kurudisha million 7. Inaelekea hujawahi kufanya biashara.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…