Maisha yanaenda kasi sana

Cpwaa kafa lini mkuu[emoji3064][emoji102]
Rapper Ilunga Khalifa aka Cpwaa, alifariki dunia usiku wa kuamkia January 17, 2021 baada ya kulazwa katika hospitali ya taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam, ilikua siku ya Jumapili
 
RIP Babu yangu, nakumbuka kuna siku ulinitia mabanzi kisa nilikuja kula chakula nikiwa tumbo wazi ukasema '...ndio adabu gani hii unakulaje chakula ukiwa umekaa uchi? Nenda ndani kavae Shati haraka mabanzi mabanzi...'

Ulinitia mabanzi mbele ya bibi, kaka na dada zangu ila nikajikokota hivyo hivyo huku machozi yananilengalenga nikaenda chumban kuvaa Shati nikarudi kuja kuendelea kula pamoja nanyi na tangia hapo sijawahi tena kula chakula nikiwa tumbo wazi mpaka leo..

rest easy grandpa
 
Ramadhani "Banza Stone" Masanja "Jenerali, Mzee wa Euro", Pumzika Kwa Amani, huku bado tunaendelea kufarijika na burudani uliyotuachia.
 
Kweli Mzee Babu alikuwa very strictly. Mwenyezi Amrehemu.
 
Kandoro,kolimba,karugendo(mwandishi),Elvis musiba,et el.
Na Gwiji la Habari za Uchunguzi "Stan Katabalo " wa gazeti Mfanyakazi likitoka kila Jumamosi. Mmoja wa victim wa kwanza katika habari kutolewa kafara na Mafisadi waliotaka ufisadi wao ubaki sirini. Apumzike Kwa Amani.
 
Dah leo nimewakumbuka Mr. Ebbo (me mmasai bwana nasema mm mmasai), Mtoto wa Dandu, Said Mwamba Kizota, Ruge Mutahaba, God Mjelwa, Ephraim Kibonde na Mkewe. Waendelee lupumzika kwa aman
Hapo "God Mjelwa" ulimaanisha "John Mjema"!? RIP Steve 2K.
 
Daah!! Aisee, huyo alikuwa Mwamba kweli kweli. Mwenyezi Amrehemu. Alithibitisha ubaba ni sacrifice.
 
[emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]
Kila dakika na kila siku kuna watu hupata furaha na kuna watu hupata majonzi makubwa kwa kuwapoteza wapendwa wao ambao ni msaada kwenye maisha yao, watu hawa hulia kwa uchungu sana na kukosa tumaini, lakini tuwaombee heri ndugu, jamaa na marafiki zetu ambao waneshatangulia na hatupo nao tena katika hii dunia, tuzidi kuishi katika misingi bora na yenye uungwana tukifahamu kua duniani tunapita, na sisi hatutokuepo siku moja hivo tuache kumbukumbu njema.
 
Hiyo stori ya David sounds very interesting.
 
Zilikuwa ni sera mbovu tu, sidhani ni sahihi kusema kuwa alikuwa na maslahi yake binafsi hapo
Kwanini aliwatetea sana wakenya kuja kufanya kazi nchini wakati huo kazi hizo zinaweza kufanywa na watanzania
 
RIP Sebastian Kinyondo "mzee wa mitemba"
 
Katika hao wote ninayemlilia na kumkumbuka daima hadi nami dunia inichukue ni mwamba jembe aka jiwe, aliyewafanya walamba asali waufyate mkia kama mbwa koko.
 
Hapo "God Mjelwa" ulimaanisha "John Mjema"!? RIP Steve 2K.
Hapana aisee hiyo huyo, huyu God Mjelwa alikuwa graphics designer mmoja matata sana, yeye ndiyo alidesign ile nembo ya chui kwenye bia ya serengeti. Mabango mengi sana yale ya Fiesta za kipindi kile yeye ndiyo alikuwa akidesign. RIP mwamba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…