Zurie
JF-Expert Member
- Jul 6, 2014
- 2,012
- 5,571
Miili ya vichanga wawili wanaosadikiwa kuwa mapacha imekutwa kwenye Mto Nairobi Jijini Nairobi nchini Kenya katika zoezi la usafi
Watoto hao walikutwa wakiwa kwenye mifuko ya plastiki mmoja akiwa bado akipumua lakini alipoteza maisha muda mfupi baadaye. Walizikwa karibu na walipokutwa
Mamlaka zinaamini miili hiyo inatupwa kwenye mto huo na mahospitali baada ya utoaji mimba ambao ni kinyume cha sheria nchini Kenya
Gavana wa Nairobi, Mike Sonko ametoa wiki moja uchunguzi ufanyike maana hii ni mara ya nane tukio kama hili la kukutwa miili linatokea ndani ya miezi michache
Licha ya miili ya watoto nane, maiti za watu wazima wanne pia zimepatikana tangu zoezi la kusafisha mto lianze
Watoto hao walikutwa wakiwa kwenye mifuko ya plastiki mmoja akiwa bado akipumua lakini alipoteza maisha muda mfupi baadaye. Walizikwa karibu na walipokutwa
Mamlaka zinaamini miili hiyo inatupwa kwenye mto huo na mahospitali baada ya utoaji mimba ambao ni kinyume cha sheria nchini Kenya
Gavana wa Nairobi, Mike Sonko ametoa wiki moja uchunguzi ufanyike maana hii ni mara ya nane tukio kama hili la kukutwa miili linatokea ndani ya miezi michache
Licha ya miili ya watoto nane, maiti za watu wazima wanne pia zimepatikana tangu zoezi la kusafisha mto lianze