Majambazi 6 wauwawa biharamuro

Yona F. Maro

R I P
Joined
Nov 2, 2006
Posts
4,201
Reaction score
236
Habari zilizotufikia sasa hivi zinasema kuna majambazi 6 wameuwawa katika mapambano na askari huko buharamuro , majambazi hao walikutwa na silaha kadhaa za kivita inasemekana walikuwa wanajiandaa kuvamia mgodi mmoja wa madini katika eneo hilo .

Bado haijajulikana kama majambazi hao ni wan chi jirani au ni raia wa Tanzania , mpambano huo ulichukuwa dakika chini ya 40 kwa sababu askari hao walikataa amri ya kuwataka kujisalimisha kwa askari
Tutawafahamisha zaidi jinsi tutakavyokuwa tunapata habari zaidi

http://groups.google.com/group/wanabidii/t/2c9d8cd361d55f57?hl=sw
 
Kama ni habari ya kweli well done Polisi. Hawa sasa hivi ni kuwaua tu
 
hivi kwa nini wanashindwa kuwakamata? Maana kwa kuwkamata wakiwa hai itawasaidia polisi kupata information kutoka kwao na kuendeleza zaidi mapambano dhidi yao
 
hivi kwa nini wanashindwa kuwakamata? Maana kwa kuwkamata wakiwa hai itawasaidia polisi kupata information kutoka kwao na kuendeleza zaidi mapambano dhidi yao
Na wakishawakamata wakiwa hai, kwa sheria za nchi yetu watapewa dhamana, na wakishakuwa nje watawahonga polisi na mahakimu na baadae wanarudi kuishi nasi kuendeleza ujambazi wao!
 
Sheria za Tanzania zinakataza kabisa watu hata polisi kujichukulia sheria mkononi.

hakika polisi hawakupaswa kuwauwa walitakiwa wawakamate wakiwa wazima au hata majeruhi lakini sio kuuwa. Kwani hao walikuwa WATUHUMIA WA UJAMBAZI na wala SIO MAJAMBAZI.

Aliyekuwa na uwezo wa kusema hao ni majambazi ni uamuzi wa mahakama.

Polisi wanavunja sheria.
najiuliza hivi kwanini hata watu binafsi wakimkamata kibaka na kumuuwa polisi hao hao wanafanya uchunguzi na wakigundulika walioshiriki wanawafikishwa mahakamani kwa kosa la mauaji.

Au hata mwizi akija kuvamia nyumba yako na wewe ukamkamata na kumpiga hadi kumuuwa, unashitakiwa kwa kosa la mauaji. Kwanini polisi wasishitakiwe

lazima sheria iangaliwe ili wote wawe na haki sawa mbele ya sheria.
 


ni vyema wamewaua kabisaa je kama wangewahiwa wao hapo ungesema nini???
 
Bihalamuro na si Biharamuro! Kazi nzuri polisi, lakini na wale wezi wakubwa kama akina Jitu Patel na RA fanyeni hivyo hivyo
 
Majambazi!!! mtumeeeee!! wameanza tena, kulikuwa shwari kidogo hapa kati, well done polisi, hawa jamaa nikuwawahi tu wakikuwahi huna bahati.
 
Bihalamuro na si Biharamuro! Kazi nzuri polisi, lakini na wale wezi wakubwa kama akina Jitu Patel na RA fanyeni hivyo hivyo

huwa najiuliza kwa nini hawa akina RA, chenge, rashidi, patel, n.k. nao wasiuliwe na ikajulikana walikuwa wakikaidi kukamatwa?
 
wawe majambazi kweli basi#

kwa mujibu wa gazeti la mwananchi ni waliouawa ni 4 na wawili walifanikiwa kutoroka. Katika waliouawa yupo mmoja raia wa burundi na walikutwa na bunduki 4 aina ya SMG, risasi 607 ktk magazini 11 na magruneti 2.
 

Jamani polisi hawatakiwi kuuwa kwani wao hawako juu ya sheria, ni ajabu nchi hii kila siku polisi wanauwa wakiwa wanapambana na majambazi halafu baada ya hapo jalada linafungwa. Je DPP anajua kuwa kunahitajika katika mazingira hayo kaunzisha iquestchini ya inquest Acts??????

Kwa jinsi mitanzania tulivyo unaweza kukuta inquest ya mwisho ilifanyika mwa 1980 au 1982 na toka hapo hakuna inquest iliyofanyika pamoja na vifo vyote hivyo vya wazi ambavyo havichunguzwi. Unaweza kukuta kuwa pamoja na sheria kuwepo, practically hakuna coroners wa kufanya inguest hizo sababu kubwa ni kuwa hawajateuliwa. Mara ya mwisho nimeona ofisi ya coroner mwaka 1985 toka hapo sijaona tena ofisi kama hiyo mwenye kuweza kupata ofisi ya coroner hapa tanzania anitonye.

Kutokana na upungufu hup ndio maana polisi ni trigger happy, wanajua wakiuwa hawataulizwa, Haki za binadamu mko wapi jamani.....au mnangoja wazungu waseme.
 
Mimi nashawishika kuamini kuwa ipo haja ya serikali kupitia upya kile kinachofahamika kama hifadhi za taifa. majammbazi haya yamekuwa yakitumia mwanya huo huo wa serikali kuzuia baadhi ya misitu ambayo ukiiangalia kwa makini siyo productive. kwanini wasiruhusu baadhi ya maeneo watu wakaanza kuyatumia kwa kilimo? hii ni kwa sababu baadhi ya "hifadhi" kwa barabarani zinaonekana ni misitu , lakini kwa ndani ni uwazi mtupu. hawa ma bwana misitu wakifanya force field analysis wataweza kiusaidia nchi kuelewa msitu upi uachwe na upi utolewe kwa matumizi ya wnanchi badala ya kuwa achia polisi kupambana na majambazi hao ambao ni wa msimu. otherwise tumekwisha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…