Majanga kama hili la Moto Kariakoo yanazidi kutukumbusha umuhimu wa Sekta Binafsi kwenye Uchumi

Tatizo la taasisi za umma ni kufanya kazi kwa mazoea, pia sheria mbovu maana kuna taratibu za hovyo sn
 
Soko kama la Kariakoo kulitakiwa kuwe na gari za zima moto muda wote pale
 
Swali gani unauliza kwani Dunia kote wanaongozwa na ccm? Chama chchote chasisa kinaweza kuongoza nchi sio lazima ccm. Vipaumbele vya ccm ni kutawala Tanzania milele sio kulinda mali za wanyonge

Jibu hili swali kwanza mkuu 👇 halafu endelea na huo uchambuzi wako, Lijibu kwa jibu 1 Straight n Clear

Ukishaiondoa unamweka nani
 
Kwani miaka yote ya nyuma kabla ya awamu ya tano jiji la dar es salaam kila kona ulikuwa unakuta magari binafsi ya zimamoto ya night support, kulikuwa na shida?kwani hayafanyi kazi moja tu, ya kuzima moto, bali yanajishughulisha na majukumu mengi tu, mfano ulinzi, mwenda zake ndio akayaweka kwenye hali ngumu!!na tatizo la dar hata kuwepo na magari mengi ya kuzima moto , sio dawa, japo inaweza saidia kidogo, shida ni mfumo wa maji , hakuna sehemu nyingi za kuyachukua maji, na kuwahi sehemu ya tukio!!moto upo kariakoo maji yanafuatwa uwanja wa ndege huo si utani!!!
 
Umepotea mkuu, eti kwa sababu matukio ya majanga ni nadra basi ndo itakuwa ni upotevu?

Umewahi kujiuliza bajeti ambayo inaenda kwenye kikosi cha uokoaji na fire kila mwaka? Ni Billions of money mkuu, ambazo naona kama zinachezewa na huduma mbovu ambazo tunaziona kwa sasa
 
Mi nna uhakika ingekuwa ni Night Support ndo wana tenda ya kuzima ule moto, usinge last hata masaa matatu.

Hawa watu wa private wapo sharp sana
 
Ndo madhara ya kupata viongozi wenye maono radical kwenye kuendesha uchumi.

Uchumi unaendeshwa kwa sekta binafsi na sekta ya umma. Huwezi tu ukaamua kuua sekta binafsi kwa kutokuelewa mchango wake.

Niomeona hata hii mentality kwenye matokeo ya kidato cha sita, unakuta viongozi wa serikali wanaanza kujisifu kwamba shule za serikali zimeshinda shule za binafsi, huo ni ujinga ni as if shule za binafsi ni mashetani fulani hivi..

Mentality hii ibadilike kwa kweli, inatufelisha sanaaa
 
Hivi Knight support,ultimate huwa wanazimaga moto bure au

Ova
 
Mkuu embu nipe historia ya mission zozote ambazo zimamoto ambao ipo chini ya serikali wame accomplish.

Mi naona ifike wakati tuache kuishi kwa mazoea, lazima tufikiri nje ya box, kama unakuwa na shirika linapewa bajeti ya mabilioni kila mwaka halafu haliwezi kufanya kazi yake kikamilifu, ni kwanini uendelee kulikumbatia?
 
Soko kama la Kariakoo kulitakiwa kuwe na gari za zima moto muda wote pale
Kutoka pale Fire mpaka kariakoo ni mwendo wa dakika tatu tu ila jiulize soko linawaka zaidi ya masaa ya kutosha halafu fire wanakuja bila maji..

Unapaswa kuwa na roho ya chuma kuvumilia huu utendaji kazi wa hawa jamaa
 
Hivi Knight support,ultimate huwa wanazimaga moto bure au

Ova
Ni suala la cost benefit analysis. Tufanye utafiti wa bajeti inayotengwa kila mwaka kuhudumia kikosi cha zima moto. Halafu angalia na output wanayotoa kwa jamii... Yaani hakuna usawa gharama ni kubwa output zero.

Pia angalia kwa mfano kama ungekuwa na SLA na kampuni binafsi ya kuzima moto kama ingekuwepo, ndio watalipwa kila mwaka ila tegemea ufanisi, na hayo ndo matumizi ya pesa yanapaswa kuwa.
 
Hahaha sahau
Siwezi kusahau kirahisi hivyo..! Hii ni awamu nyingine mkuu..! Alafu tujue kuwa raisi wa kwanza kukalia kiti cha uraisi akiwa na umri mkubwa ni Raisi wa sasa. Hilo linamafanya awe bora kuliko watangulizi wake....
 
Umewahi kufikiria Kama kungelikuwepo na kitu Kama hiko Kisha kutokee hakuna kazi hizo taasisi zingekua zinajiendeshaje?
Kazi ya zimamoto sio kuzima ajali za moto kuna zile compliance standards za viwanda ili kuepuka ajali za moto wakija kufunga vifaa hivyo au kutoa consultancy wanaingiza mamilion, kuuza fire safety equipments, kutoa training kwa taasisi mbalimbali, n.k kote huko wanaingiza pesa bila kuzima moto.

Private sector ni ubunifu maana mfanyakazi mzembe anatimuliwa ama management inang'olewa. Ila kiserikali ni kma haina mmiliki so kila mtu hawi accountable popote unless mwanasiasa aseme kwanza.
 
Mkuu wanaweza bado kulipwa na serikali au kupewa ruzuku ili cost zishuke. Uzuri ni tender na unaweka conditions zisipofikiwa mkataba unavunjwa. Trust me ufanisi ni 90% ila hawa wenye job security hawana KPI za kubanwa kila mwaka wa fedha ukiisha ufanisi hauwezi panda.

Nitajie tu ni sekta ipi ambayo serikali imeizidi private sector hapa Tanzania? Hta JPM aliwahi kiri CEOs na MDs wa private companies wana akili na mipango kuliko wa serikalini waliofeli kuleta magawio tokea anaingia madarakani.
 
Kikosi cha zima moto ni kama kime sahulika

Ova
 
Mkuu hata mimi nimefikiri hili la kuliupwa na serikali ila nikaona ni ghali kuliko serikali kushughulikia yenyewe. Wakiwepo watu private wa kulipwa lazima gharama zake zitakuwa kubwa. Sana sana serikali itaagiza wananchi kila nyumba itoe mchango kila mwezi wa zimamoto jambo ambalo litaongeza gharama kwa wananchi. Kitu ambacho kinatufanya tusifanikiwe ni uzembe tu. Mimi nasema tunaweza kwa sababu nchi nyingine wameweza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…