Majaribio ya Makombora Korea Kaskazini

Majaribio ya Makombora Korea Kaskazini

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
1643617613048.png

Vyombo vya Habari vya serikali nchini Korea Kaskazini vimetoa picha zinazosema kuwa zilichukuliwa kutokana na majaribio ya kombora lake kubwa zaidi kutoka mwaka 2017.

Picha hizo zinaonesha sehemu za rasi ya Korea na maeneo yaliyo karibu yakionekana kutoka angani.

Korea Kaskazini ilisema kuwa kombora hilo lilikuwa la masafa ya kati ya Hwasong-12.

Korea Kusini na Japan zilisema lilifikia umbali wa kilomita 2,000 (maili 1,242) kabla ya kuanguka kwenye maji kutoka Japan. Nchi zote mbili zimeshutumu jaribio hilo, ambalo ni la saba mwezi huu.

Picha hizo, zilizotolewa na shirika la kitaifa la habari la Korea Kaskazini, KCNA, ziliripotiwa kupigwa kwa kutumia kamera zilizowekwa kwenye kichwa cha kombora lililofanyiwa majaribio.

Picha mbili za kurusha kombora la Korea Kaskazini na mbili za Dunia zilizochukuliwa kutoka kwenye kombora hilo angani ambazo zinaonyesha wakati wa kurushwa na nyingine inaonyesha kombora likiwa katikati ya safari, iliyopigwa kutoka juu.

Maafisa wa Japan na Korea Kusini wanakadiria kuwa kombora hilo lilipaa kwa dakika 30 kwa umbali wa kilomita 800.

Credit: Star TV
 
Umbali wa kilomita 2000 au kilomita 800?

Umbali ni 'distance' ambayo kwa mujibu wa taarifa ni kilomita 800. Hiyo 2000 sio umbali bali ni kimo au urefu (height/apogee).

By the way, hizo picha za 'dunia' zinaweza kuleta mgogoro kidogo na watu fulani hivi!
 
Umbali wa kilomita 2000 au kilomita 800?

Umbali ni 'distance' ambayo kwa mujibu wa taarifa ni kilomita 800. Hiyo 2000 sio umbali bali ni kimo au urefu (height/apogee).

By the way, hizo picha za 'dunia' zinaweza kuleta mgogoro kidogo na watu fulani hivi!
Watu gani hao fafanua bana
 
Hana jipya USA alishamwambia Kama unaweza rusha hata jiwe kwenye maslahi yoyote ya USA alafu ndo utajua kwanini maharage mboga au futari[emoji3166]
 
Hana jipya USA alishamwambia Kama unaweza rusha hata jiwe kwenye maslahi yoyote ya USA alafu ndo utajua kwanini maharage mboga au futari[emoji3166]
Ajabu ni kwamba Kim yuko kwake anatengeneza vyombo vya kuilinda nchi yake na raia wake, lakini US analalama na kuomba wazungumze aachane na hayo makombora. Wakati huo huo US anayo makombora hayo

 
Ajabu ni kwamba Kim yuko kwake anatengeneza vyombo vya kuilinda nchi yake na raia wake, lakini US analalama na kuomba wazungumze aachane na hayo makombora. Wakati huo huo US anayo makombora hayo

US zana anazo lakn hatak wenzake wawenazo ili yy abakie kuwa super power.
 
Ajabu ni kwamba Kim yuko kwake anatengeneza vyombo vya kuilinda nchi yake na raia wake, lakini US analalama na kuomba wazungumze aachane na hayo makombora. Wakati huo huo US anayo makombora hayo

Anayetaka North Korea iachane na makombora si US pekee bali ni nchi takribani zote za UNSC zikiwemo China na Urusi. Pitia maazimio yote ya UNSC kuhusu North Korea na makombora yake!
 
Anayetaka North Korea iachane na makombora si US pekee bali ni nchi takribani zote za UNSC zikiwemo China na Urusi. Pitia maazimio yote ya UNSC kuhusu North Korea na makombora yake!
Niwekee hapa link ya habari yoyote inayoelezea China kama China au Russia kama Russia inaitaka North Korea kuachana na silaha za nyuklia.

Au weka link ya habari yoyote inayoelezea kuwa China au Russia wanaogopa majaribio ya silaha za nyuklia yafanywayo na North Korea/ au North Korea kuwa na nyuklia.

Ajabu ni kuwa wa mbali (US) pamoja na vibrant wake ndio wanaogopa na kubweka zaidi, wakati waliokaribu na North Korea (Russia na China) wanaona kawaida tu.
 
Niwekee hapa link ya habari yoyote inayoelezea China kama China au Russia kama Russia inaitaka North Korea kuachana na silaha za nyuklia...
Ukitaka kufahamu kuhusu misimamo ya China na Urusi kuhusu silaha za nyuklia za North Korea, fuatilia majadiliano na maazimio mbalimbali ya kimataifa kuhusiana na nchi hiyo. Usiishie tu kusikiliza kauli za kisiasa za kwenye media.

Anza kwanza kwa kusoma kuhusu The Six Party Talks! Hili lilikuwa ni azimio la amani dhidi ya mpango wa Korea Kaskazini wa silaha za nyuklia. Azimio lilihusisha nchi sita. Urusi na China zilihusika!

Pitia mlolongo wote wa mazungumzo kuanzia mwaka 2003:



Ukimaliza hilo, hamia kwenye maazimio mbalimbali ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa (UNSC), vikiwemo vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini kuhusiana na masuala yake ya nyuklia, ikiwemo kujiondoa kwake katika mazungumzo. Urusi na China pia zimehusika sababu ni nchi wanachama wa baraza hilo!



Ukihitaji link ya Wikipedia utiririke nayo, hii hapa chini:

 
Wanaobweka kila wakati wanajulikana
Kuna msemo unasema: Actions speak louder than words!

Hao "wanaobweka" mimi sina shida nao. Kauli yenye nguvu zaidi ni ya wale wanaokaa katika vyombo vya kimataifa na kufanya maamuzi kuhusu masuala mbalimbali ya dunia kwa vitendo.
 
Ukitaka kufahamu kuhusu misimamo ya China na Urusi kuhusu silaha za nyuklia za North Korea, fuatilia majadiliano na maazimio mbalimbali ya kimataifa kuhusiana na nchi hiyo. Usiishie tu kusikiliza kauli za kisiasa za kwenye media...
Usilete story za kale (zaidi ya muongo 'decade' muongo mmoja umepia) kwenye vikao vya umoja wa mataifa, nimekueleza lete link za habari toka popote ujuapo ambapo China kama China, Russia kama Russia walaani au kubweka (kama afanyavyo Marekani na vibaraka wake) mpango wa silaha za nyuklia wa North Korea
 
Usilete story za kale (zaidi ya muongo 'decade' muongo mmoja umepia) kwenye vikao vya umoja wa mataifa, nimekueleza lete link za habari toka popote ujuapo ambapo China kama China, Russia kama Russia walaani au kubweka (kama afanyavyo Marekani na vibaraka wake) mpango wa silaha za nyuklia wa North Korea
Umeomba link, umepewa link. Nenda kwanza kasome!

Story za kale?! Kwani mpango wao wa nyuklia umeanza leo? Soma kwanza ulichokiomba, ndio urudi kwenye mjadala!
 
Back
Top Bottom