Maji ya mvua ni salama kwa kunywa?

Maji ya mvua ni salama kwa kunywa?

Water guard haitakusaidia chochote kwani asilimia kubwa ya maji hayo hayana vimelea lakini yanaweza kuwa na dusts. Asilimia kubwa ya matatizo ya Rain water ni toxic chemicals, coat ya Carbon, Impurities za kutu zilizotoka kwenye mabati n.k. Sidhani kama kuchemsha maji au WaterGuard itasaidia kwenye Acidic Rain au Toxic rains. Nop
 
Maji ya kuchemsha hayana ladha. Sithubu kabisa kuchemsha kwasababu ukichemsha unaua vile vijidudu, alafu vikifa si vinakuwa marehemu?!! Vikioza sasa!!! Bora kuvinywa vizima na utamu wake.
Hahaha umenichekesha mkuu
 
Dah! Mimi niliyakinga kwenye mvua ya juzi. Nimejaribu kuyanywa hayapiti kooni. Sijui hawa wakina Bakresa wametuwekea nini kwenye maji yao... Ngoja tu tuendelee kuwaunga mkono...
 
Nimeikuta nikaona si mbaya tukishare

Kwa ufupi
Kwa asili yake maji ya mvua kabla hayajafika katika anga letu huwa ni safi na salama kwa kunywa. Hata hivyo, maji hayo lazima yapite katika anga na ndipo yafike ardhini kama mvua.

Maji ya mvua ni salama kwa kunywa?
 
Maji ya Mvua, Maji ya kwenye mito, Maji yanayotiririka kwenye milima ( water falls) ... Ni dawa kubwa sana.

Pendelea kuoga na kunywa maji Haya.

Ni mazuri pia kwa kukuweka kuwa karibu na Mungu.

Kama wewe ni muislam au mkristo, pendelea kutumia maji haya kwa sala, toba , kutawaza n.k

Ni salama sana. Hayana madhara.

Maji ya kuchemsha hayana dawa!
 
Wanageo science na wabobezi wa geography na yeyote mwenye elimu ya afya kuhusu maji ya mvua ni salama ukiyanywa bila kuchemshwa. Naomba ushauri nimekuwa nikiyakusanya kwenye matank hapa kwangu na kuyatumia kunywa na kazi zingine.


Je maji ya mvua bila kuchemshwa ni salama?
Nawakilisha
Inategemea mazingira ya maji hayo. Kwa mfano maji ya mvua inayonyesha maeneo kama mijini ambako kuna uchafuzi mkubwa wa mazingira si salama. Pili, yanaweza yakawa maji ya mvua ambayo ni salama lakini ukayatunza katika chombo (Tank) ambayo ni chafu. Maji hayo yatakuwa si salama tena. Usalama wa chakula cha aina yoyote ikiwemo maji inategemea mambo mengi sana ikiwa ni pamoja na wewe binasi unavyohandle hicho chakula.
 
Kinga maji ya mvua kwenye chombo kisafi, hakikisha bati halina kutu, yachemshe hapo unaweza kuyatumia kwa kunywa. Hakikisha hutumii maji ya mvua ya kwanza ya msimu hayo sio salama kwa kiasi kikubwa.

Duc In Altum.
 
Maji hayo uliyoyaka kwenye tanki si salama kama utayatumia kwa kunywa moja kwa moja bila kuchemsha au pasipo kuyatibu kwa dawa ya chlorine ama water guide.
maju ya tanki yanapokaa kwa muda mrefu wadudu huzaliana katika maji hayo na hivyo endapo utayatumia moja kwa moja badi utakuea katika hatari ya kuapta magonjwa.

Pia kuwa na utaratibu wa kusafisha tanki kila matmra ba kuondoa uchafu unaotuama hii itasaidia maji hayo kuwa na usalama zaidi.
pia mvua inapo acha kunyesha kwa muda mrefu Bati huchafuka kwa vumbi, kunyesi cha ndege na mambo kama hayo. hivyo maji ya kwanza usiruhusu yaingie moja kwa moja kwenye tanki lako acha maji hayo yamwagike chini hadi uone badi limekuwa safi ama maji yameanza kuwa safi ndio uruhusu maji hayo kuingia katika tanki.
nakushauri pia kila baada ya muda fulan basi uwe unaweka chumvi katika tanki hilo la maji pia usisahau kuwa unayatibu kwa water guide.
maji hayo yatakuwa salama kwa matumizi ya nyumbani kwako.

Chumvi inasaidia nini?
 
Back
Top Bottom