KERO Maji yanatoka Mbezi Beach lakini presha ni ndogo sana hata kama una tenki la akiba ni kazi bure, maeneo mengine Dar hali ikoje?

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Precious Diamond

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2023
Posts
593
Reaction score
1,376
Wakuu kwema,

Nilikuja na uzi hapa baada ya kukosa maji karibu siku 5 bila taarifa yoyote, baada ya malalamiko kupelekwa Insta maji yakaanza kutoka, lakini toka yaanze kutoka presha ni ile ile, ndogo sana.

Mpaka leo hii maji yanatoka kidogo kidogo sana kiasi kwamba hata kama mtu una tenki la akiba ni kazi bure maana presha haitoshi kupandisha maji.

Wakuu maeneo mengine kwa Dar hali ikoje, isije ikawa ni huku Mbezi tu walikozoea kutuonea kila mara?

Wizara ya Maji na DAWASA nini kinaendelea? Maji yasipotoka basi tunakomolewa presha inakuwa ndogo!😒😒

Pia soma: Hatimaye maji yameanza kutoka Mbezi Beach kwa Zena, JF mbarikiwe
 
Nunua pump, vuta hayo maji kwenye tanki lako,

Mkuu, ata ukiwashwa utakuja kutuomba ushauri, jikune au kakunwe
 
Kwetu yanatoka hadi yanapasua mabomba. Tabata Bonyokwa
 
Hata Ukonga hivyo yalitoka alhamis mpaka Jmosi
 
Nunua pump, vuta hayo maji kwenye tanki lako,

Mkuu, ata ukiwashwa utakuja kutuomba ushauri, jikune au kakunwe
Comment ya pili haikuwa necessary, huduma hizi ni haki yetu tena si huduma tu, huduma bora, kama maji hayana presha wanatakiwa kuhakikisha tunapata maji kwa presha stahiki, hatufanyiwi hisani, tunazilipia, ni HAKI yetu
 
Kama yanatoka shukuru,Goba ni hatarii tunapishana na maboza tuu
 
Mtaani kwangu yanachagua Mtaa Kuna maeneo Ni mwaka na mwezi Sasa hayajatoka.
Ajabu Jamaa kila wakija wanakuja na mpya Mara Tunaongeza Bomba presha iwe kubwa Mara Tunaongeza pump.

Juzi wamekula kipondo jioni ..asubuhi maji yametoka.
 
Mtaani kwangu yanachagua Mtaa Kuna maeneo Ni mwaka na mwezi Sasa hayajatoka.
Ajabu Jamaa kila wakija wanakuja na mpya Mara Tunaongeza Bomba presha iwe kubwa Mara Tunaongeza pump.

Juzi wamekula kipondo jioni ..asubuhi maji yametoka.
Hapo ndio unajua kuna watu mahala wanafanya yao wale kwa urefu wa kamba
 
Hapo ndio unajua kuna watu mahala wanafanya yao wale kwa urefu wa kamba
Mwenyekiti was eneo ndio kinara was kula njama na wauza maji was Magari na Hawa wanaosambaza mabomba ya maji ya visima binafsi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…