Majibu ya Juma Mgunda kuhusu kipa Aishi Manula 'very unprofessional'

Shida vitambi vya madafu na malimao. Hovyo kabisa yule kocha
 
Juma mbunda naye hovyo! Anaonesha yuko kishoga tu! Hata hakumbuki kuheshimu umri na umbo lake!
 
Mgunda hakutumia weledi kujibu swali la mwandishi. Kiukweli Manula ni mmojawapo wa makipa wazuri sana lakini mapungufu yake ya kucheza mipira ya kona na krosi kwa ufasaha na ile tabia yake ya kusogea mbele kidogo ya goli wakati mchezo unaendelea ndio vinamshusha thamani ukimlinganisha na Kaseja. Ukweli huu mchungu ndio mashabilki wa Manula hawapendi kuukubali lakini mwisho wa siku ndio ukweli wenyewe.

Mgunda angejibu tu kistaarabu kuwa makipa waliopo sasa hivi wamefanya vizuri ndio maana wameitwa na yeye Manula akifanya vizuri ataitwa maana timu ya taifa ni ya watanzania wote wakiwepo Manula pamoja na akina Kaseja na Metacha. Basi ingetosha kumtoa Manula kwenye reli na mashabiki wa Manula wangetulia kuliko alivyojibu maana sasa inatafutwa timu ya taifa ifungwe na makosa yawe ya golikipa hapo Mgunda atatafuta pakutokea na asipaone.
 
Kiukweli Manura hafai basi tu
Kwa hapa nchini ndio kipa namba moja kwa sasa, kwa wazawa na wageni wote wanaocheza ligi zote za nchini, na ameteuliwa na makocha kuwa kipa bora katika misimu yote aliyokuwapo Simba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…