Majibu ya madaktari yamegongana nifanyeje?

Majibu ya madaktari yamegongana nifanyeje?

Inaelekea figo kweli ni nzima ila sasa hiyo Calcification ndio inaweza kuwa imesababisha yote haya, endelea na uchunguzi hasa ni vizuri kama watachukua Biopsy kutoka kwenye hiyo Calcification na majibu yake yatatoa mwanga wa matibabu, KCMC na Muhimbili ni wazuri sana kwa magonjwa kama haya ..Au kamwone Dr Mbwambo private Hospital (Moshi) na ni mzuri sana kwa mikojomikojo

Kwa Dar Ni Dokta Gani?
 
Mzee wangu anatibiwa katika hospital moja jina naomba nisilitaje kwa usalama wa mgonjwa.kapiga CT I.V.U Majibu Yakatoka Tukayapeleka Kwa Specialist Wa Matatizo Ya Figo.Huyu Akasema Kwenye Figo Hakuna Tatizo Ila Kwenye Ureta Ya Mkojo Kuna kauvimbe,akasema Tumuone Specialist Wa Vibofu Vya Mkojo.

Tukamuona Huyo Wa Vibofu,majibu Ya Mtaalam Wa Vibofu Kasema Figo Imekufa.Sasa Dr Wa Figo Yeye Kasema Figo Inafanya Kazi Na Akasema Tatizo Hl Halimhusu,akatuelekeza Kwa Daktari Wa Vibofu Na Mfumo Wa Ukojoaj,majibu Ya Huyu Kasema Figo Imekufa Na Iondolewe.

Na Wote Ni Madaktari Wapo Hosp Moja.Na Wote Ni Madaktar Bingwa,SASA NIFANYEJE? Ni Figo Imekufa Au Ni Uvimbe Wa Kwenye Ureta? Figo Yenyewe Imejaa Maji.Kwa Mujibu Wa Dk Wa Figo.

Naombeni Ushauri.

Hii kidogo ifanane na doctor shopping au double doctoring. Ushauri: Ulizia madaktari waliobobea katika fani hiyo. Pili usifuate ushauri wa daktari aliyesoma kipimo, yaani radiologist, ila fuata ushauri wa daktari anayekutuma kufanya hicho kipimo. Usizunguke kwa madaktari wengi, maana utachanganywa zaidi.
 
hao madokta nadhani wangekutana wadiskass kwa pamoja kujua tatizo ,au kama vipi nenda hospitali ingine
 
Back
Top Bottom