Majina Ya Viumbe Hai: wadudu, wanyama, ndege, mimea n.k.

Majina Ya Viumbe Hai: wadudu, wanyama, ndege, mimea n.k.

Ni siku za karibuni tu nimebahatika kufahamu kuwa matopetope yanajulikana kama custard apple, jina lake la kisayansi silijui.

Napenda kuulizia majina ya: mastafeli na Mafenesi. Jina la kiingereza au kilatini. Ahsanteni.
 
Katika pitapita yangu kwenye mtandao (nadhani kwa michuzi - sina hakika) nilikutana na kitu ambacho sijawahi kufiri kinaliwa.
Kuna 'maua' ya migomba (ambayo hutoa ndizi), kwamba yanauzwa (Ulaya?) na kutumika kama chakula .
Hivi yanaitwaje (Kiswahili) na yanatumikaje kwa msosi (sababu kwetu sisi yale ni chakula cha ng'ombe/mbuzi)?

attachment.php
 
Dragonfly wanaitwa 'Kereng'ende' kwa kiswahili
Jioni njema.

Mimi nadhani dragonfly kwa kiswahili anaitwa helikopta

na praying mantis ni nabii anayesali kwa sababu mantis means prophet
 
Ni siku za karibuni tu nimebahatika kufahamu kuwa matopetope yanajulikana kama custard apple, jina lake la kisayansi silijui.

Napenda kuulizia majina ya: mastafeli na Mafenesi. Jina la kiingereza au kilatini. Ahsanteni.

Soursop or soncoya
Latin Name: Annona muricata or Annona purpurea

Kuna matunda yanaitwa mbilimbi, na kwa kiingereza ni Bilimbi. Kilatini ni Averrhoa bilimbi. Ni katika jamii ya Avverhoa carambola or Star Fruit.

Pilipili mbuzi Orange, wrinkled pepper,

Pilpili kichaa Wild pepper, Capsicum eximium.

Zambarau: Water Berry kwa Kilatin: Syzygium cordatum
 
Last edited:
Katika pitapita yangu kwenye mtandao (nadhani kwa michuzi - sina hakika) nilikutana na kitu ambacho sijawahi kufiri kinaliwa.
Kuna 'maua' ya migomba (ambayo hutoa ndizi), kwamba yanauzwa (Ulaya?) na kutumika kama chakula .
Hivi yanaitwaje (Kiswahili) na yanatumikaje kwa msosi (sababu kwetu sisi yale ni chakula cha ng'ombe/mbuzi)?

attachment.php

Mkuu itabidi nimpigie shangazi yangu mmoja simu anatokea Bukoba na amekaa sana Mbeya, yawezekana anajua. Kwasababu jina linaonekana kushindikana kupatikana, tunaweza kabisa kulinyambulisha kutoka kwa wale wa Moshi/Arusha, wa Mbeya na wa Bukoba ili kupata jina moja la Kiswahili litakolokuwa la wastani kwa wote.

By the way WanaJF, hivi mizaituni kama inavyopatikana kule Mashariki ya Kati inaitwa nini katika Kiingereza, na scientific name yake ni nini?! Natanguliza shukrani.
 
koboko ni kiswahili cha nyoka aina ya Black Mamba au Green mamba. Ni nyoka mwenye sumu kali na mkali sana. King Cobra ni Mfalme Swila anayepatikana zaidi Asia
 
Huwa nasilia watoto wengi wakimwita "kombamwiko" huyo praying mantis. Sina hakika kama ni kiswahili fasihi au msimu tu.
 
Huwa nasilia watoto wengi wakimwita "kombamwiko" huyo praying mantis. Sina hakika kama ni kiswahili fasihi au msimu tu.

Kombamwiko ni jamii ya MENDE... ila wana maumbo madogo kuliko Mende tulio wazoea.
 
Zamani watu walikua wanajadilina vizuri....
Hongereni wahenga wa jf sijui mko wapi kwa sasa japo Mzee Mwanakijiji yupo sana siasani....
 
Katika pitapita yangu kwenye mtandao (nadhani kwa michuzi - sina hakika) nilikutana na kitu ambacho sijawahi kufiri kinaliwa.
Kuna 'maua' ya migomba (ambayo hutoa ndizi), kwamba yanauzwa (Ulaya?) na kutumika kama chakula .
Hivi yanaitwaje (Kiswahili) na yanatumikaje kwa msosi (sababu kwetu sisi yale ni chakula cha ng'ombe/mbuzi)?

attachment.php
Arusha yanapikwa kabisa.
 
  • Thanks
Reactions: RR
Back
Top Bottom