Majina ya watu ya Asili kama vile ya kikabila na ya kiswahili uenda yakatoweka

Majina ya watu ya Asili kama vile ya kikabila na ya kiswahili uenda yakatoweka

Mhaya

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2023
Posts
1,831
Reaction score
5,489
Ukifanya utafiti utagundua siku hizi watu wengi hawawapi watoto wao majina ya Kiasili kama vile ya kikabila au ya kiswahili.

Siku hizi majina mengi yanabaki kuwa ya kizungu kwa wakristo au ya kiarabu kwa waislamu.

Zama za kale watu walipewa majina kulingana na vitu mbalimbali au matukio mbalimbali, ambayo kwa hivi sasa watu wengi kwao yamebaki kama majina ya ukoo tu, ila jina la kwanza linakuwa la kiarabu au kizungu.

Hii ni hali ya hatari kwa majina yetu ya asili au kiswahili. Familia muangalie sana kuepuka kuwapa watoto wenu majina ya kimagharibi au kiarabu, badala ya jina la kiswahili au kikabila.

Unakuta mtu anamwita mtoto wake "Hope" badala ya "Tumaini", au "Jamal" badala ya "Tumaini"... Sasa unakuta mtu anakimbilia kumuita jina la kiarabu au kizungu ambalo linamaana sawa na jina la ambalo lipo kwenye kabila analotoka au lipo kwenye kiswahili, mpaka unajiuliza kwa nini hasingemuita tu lile la kikabila au kiswahili.

Siwapangii majina ya kuwaita watoti wenu, ila tupende vyetu
 
Ukifanya utafiti utagundua siku hizi watu wengi hawawapi watoto wao majina ya Kiasili kama vile ya kikabila au ya kiswahili.

Siku hizi majina mengi yanabaki kuwa ya kizungu kwa wakristo au ya kiarabu kwa waislamu...
Issue of Internationalisation
 
Huku kwetu majina ya kiasili yalikuwa hayaandikiki, ilibidi walimu wawarudishe wanafunzi nyumbani waje na majina ya kanisani/msikitini.
 
Kuna mkoloni mmoja huko rhodesia yeye aliitwa whitehead, kuna yule mchezaji ligi ya epl anaitwa drinkwater. Hata huku kwetu watu waliitwa majina kama hayo ila ya kiasili. Unakuta mtu anaitwa ng'imba, yaani simba, ndoghwe yaani punda, njiku, nkhambaku, mwang'ombe na mengine chungu nzima ila kwa sasa watoto hawaitwi majina hayo
 
Ndy maana ikaitwa ZAMANI, saizi kisasa.

Mwanangu anaitwa Genesis, ila mtaani wanamuita MWANZO
 
Huku kwetu majina ya kiasili yalikuwa hayaandikiki, ilibidi walimu wawarudishe wanafunzi nyumbani waje na majina ya kanisani/msikitini.
Ngh'wizukulu? Mbona linàandikika au wàlimu wálikuwa UPE?
 
Mimi kijijini kwetu naitwa MARWA MAHENDE ila hapa mjini jina langu ni EMMANUEL JOHN.
 
Mimi naangalia maana ya jina na siyo mambo sijui ya asili na upuuzi mwingine.

Siwezi waita watoto wangu (Shida, Masumbuko, Tabu) ety kwa sababu ya asili au lugha ya Kiswahili inanitaka kufanya hivyo,, ni ukichaa huo 😎🤏
 
Ndiomaana mitoto ya sasa imekuwa kama ina laana, unakuta toto halisikii, pamoja na kulisomesha shule/hizo dini lkn bado linaibuka na tabia chafu ambazo ktk UKOO hazipo, ukifuatilia kwa umakini unagundua shida ni hayo majina mnayowapa watoto yanwaambukiza tabia na asili za wale wahusika/wamilliki wa hayo majina.

Mitoto misomi lkn mijizi, mijuaji, misagaji&mishoga, na ushenzi wa kila aina yaani haisikii wala haina adabu, asili ya kiafrika imekufa imezaliwa asili mpya mbovu ya wazungu/waarabu.

Si serikali wala jamii, iko kimya hakuna anaekemea wala kulalamika kuunusuru utamaduni&uhalisia wa muafrika, watu wote tumechanganyikiwa na kulewa utumwa wa akili za watu weupe, ndiomaana wanatutawala na kutucontrol watakavyo sababu wameshikilia fahamu zetu na tunawaona wao ni kila kitu.

Rudini ktk asili zenu, hayo majina ya wazungu/waarabu sio fashion mnaharibu uzao wenu na taifa kiujumla, mwishoe mnaleta laana kwa Taifa na Afrika nzima, tunabaki nyuma kwa kila jambo, yaani Afrika hata ktk mambo ya kipuuzi tuko nyuma shida kubwa ni hii ya kuwaabudu hao watu weupe na takataka zao.
 
Back
Top Bottom