Majina ya watu ya Asili kama vile ya kikabila na ya kiswahili uenda yakatoweka

Majina ya watu ya Asili kama vile ya kikabila na ya kiswahili uenda yakatoweka

Mimi naangalia maana ya jina na siyo mambo sijui ya asili na upuuzi mwingine.

Siwezi waita watoto wangu (Shida, Masumbuko, Tabu) ety kwa sababu ya asili au lugha ya Kiswahili inanitaka kufanya hivyo,, ni ukichaa huo 😎🤏
Mbona yapo majina ya kiswahili au ya kilugha yenye maana nzuri... Furaha, neema, rehema, Akili, Fikiri, na majina yote mazuri ya kiswahili, au ya kilugha

Wewe majina ya kiswahili umeona tu Shida, Masumbuko, Tabu... Au ndio ufinyu wa kufikiri, mtoto unaenda kumuita Happiness, je ungemuita Furaha ungekosa nini
 
Sidhani kama hiyo zama za kale ulikuwepo.
 
Ukifanya utafiti utagundua siku hizi watu wengi hawawapi watoto wao majina ya Kiasili kama vile ya kikabila au ya kiswahili.

Siku hizi majina mengi yanabaki kuwa ya kizungu kwa wakristo au ya kiarabu kwa waislamu.

Zama za kale watu walipewa majina kulingana na vitu mbalimbali au matukio mbalimbali, ambayo kwa hivi sasa watu wengi kwao yamebaki kama majina ya ukoo tu, ila jina la kwanza linakuwa la kiarabu au kizungu.

Hii ni hali ya hatari kwa majina yetu ya asili au kiswahili. Familia muangalie sana kuepuka kuwapa watoto wenu majina ya kimagharibi au kiarabu, badala ya jina la kiswahili au kikabila.

Unakuta mtu anamwita mtoto wake "Hope" badala ya "Tumaini", au "Jamal" badala ya "Tumaini"... Sasa unakuta mtu anakimbilia kumuita jina la kiarabu au kizungu ambalo linamaana sawa na jina la ambalo lipo kwenye kabila analotoka au lipo kwenye kiswahili, mpaka unajiuliza kwa nini hasingemuita tu lile la kikabila au kiswahili.

Siwapangii majina ya kuwaita watoti wenu, ila tupende vyetu
Kwenye kabila langu hakuna neno Tumaini. Je tupende vyetu kama kabila au tupende vyetu kama nchi au tupende vyetu kama bara au labda tuoende vyetu kama dunia?
Kuna watu ukisema vyetu watanaanisha vya Kizungu au vya Kiarabu kulingana na imani zao, je wapi mtu anaona ndiyo nyumbani. Dini au kabila?
All in all jina ni jina tu, mimi huwa nawapa watoto wangu majina kwa sababu zangu binafsi.
 
Usipangie watu mkuu, ita wa kwako inatosha
Kuna sehemu nimesema napangia watu, au wewe nimekupangai?

Jua kuelewa utofauti wa mtu kutoa mtazamo wa maoni na mtu kumpangia mtu mwingine
 
Ulimbukeni ni tatizo kubwa kwa jamii ya waafrika. Nina watoto 4 majina yao ni
1. Baraka
2. Upendo
3. Maseko ( Mavuno)
4. Kisaka ( Dunia)
 
Back
Top Bottom