Majivuno ya CEO Barbara Yanairudisha nyuma Simba kimaendeleo

Majivuno ya CEO Barbara Yanairudisha nyuma Simba kimaendeleo

Hayawahusu..huyu mwanamke anaaasumbua sana vichwa vya watu..alipoondoka manara akalia lia akajua atabembelezwa akamsema wee lakini dada yuko ngangari. Na Kupitia huyu dada Simba inaendelea kupata mafanikio kama club.
Nyie ni mabwege kweli yani, mtu gani unagombana na kila MTU, kila mtu akulalamikie wewe tu hii sio sawa uyu mdada Ana matatizo binafsi wamuangalie kwa jicho la 3, vinginevyo atawadumbukiza shimoni taratibu na wajinga wajinga Kama wewe ndio mtaendelea kumpigia makofi, na sakata hili la Morrison ndo linazidi kumuanika ujinga wake
 
BARBARA HAKUWAHI KUMUONDOA MORISON KAMBINI.

Mbinu zile zile alizotumia Manara kuwalaghai wapenzi wa Simba kwamba anaonewa na mtesi wake mkuu ni Babra ndio mbinu hizo hizo zinatumika na Morison. Tofauti tu ni kwamba Morison bado hajalia na kutoa machozi ya kinafiki hadharani.
Umewahi kujiuliza kwa nini mbinu ni zile zile na zinafanana? Uongo hudumu kwa muda mfupi ila ukweli utadumu milele.

Aliyemfukuza kambini Morison ni meneja wa timu Patrick Rweymamu baada ya Morison kutoroka kambini na kurudi asubuhi. Morison alikuwa akiishi chumba kimoja na Inonga. Akijua Wawa ni mgonjwa na amekunywa dawa za usingizi alimuaga Inonga yupo chumbani kwa Wawa. Patrick ana kawaida ya kukagua kambi kwa kushtukiza usiku. Ilipofika siku ya tukio saa sita usiku Patrick alivamia kambi na alipofika chumbani alimkuta Inonga peke yake. Alipomuuliza alipo Morison alijibu yupo chumbani kwa Wawa. Patrick alipofika chumbani kwa Wawa hakumkuta Morison na alikuta Wawa amelala. Patrick aliondoka na kurudi tena saa 12 alfajiri na akakuta Morison bado hayupo. Ndipo akamuuliza Wawa Morison yupo wapi? Wawa akajibu alikuwepo pale ila yeye alipopitiwa na usingizi Morison alitoweka.

Patrick aliendelea kuwepo pale kambini mpaka saa mbili asubuhi ndipo akamuona Morison akirejea kwa kuruka ukuta. Patrick akamuamrisha asiruke ukuta bali akapite getini. Na Morison alitii. Alipoingia getini Patrick alimgomea na kumuamuru arudi alikotoka. Morison alinza kumtukana Patrick na kumwambia hana uwezo wa kumuondoa kambini yeye ni mtu mdogo sana. Ndipo Patrick akamgomea kuingia kambini na ukatokea mzozo kati yao wawili. Ndipo Patrick akawaomba wanajeshi ambao ni walinzi pale wamtoe nje na akatolewa nje ya geti kwa nguvu na walinzi ambao ni wanajeshi.

Alipofika nje akapiga simu ya vitisho kwa Babra na kumwambia nafukuzwa kambini na mimi nitachukua hatua na mtanilipa fedha nyingi mno. Ndipo Babra akapiga simu kwa Patrick kumuomba amruhusu Morison aingie kambini na viongozi watakuja kuyazungumza. Kutokana na matusi, kiburi na jeuri aliyokuwa Morison amemuonyesha Patrick. Patrick aligoma na kumwambia Babra kama huyu anaingia kambini natoka mimi. Siwezi kuwa na mchezaji kambini ambaye hana maadili na anajiona yeye ni mkubwa kuliko wengine wote kambini. Ndipo Babra akarudi kwa Morison na kumwambia nenda nyumbani tutakuita tuyazungumze.

Babara aliitisha kikao na Patrick alieleza vitendo vingi vya utovu wa nidhamu vya Morison tena kwa ushahidi na jinsi alivyomvumilia na kumfichia siri. Morison akalia machozi na kukiri huku akionyesha kutokuwa tayari kuomba radhi.
Hiki ndio kilikuwa chanzo cha sakata la Morison.

Cha kujiuliza kwa nini Meneja wa timu hatajwi anatajwa Babra? Ni wazi kuna kitu kinafichwa na kuna kitu kinatafutwa.
Watu wale wale wanataka kutuaminisha Babra ni chanzo cha matatizo Simba ndio hao hao wanatengeneza hii sinema.

Kisa hiki nimesimuliwa na mchezaji mmoja wa Simba ambaye hakutaka jina lake liwekwe wazi.
( Jicho la tatu la Mgalilaya).

Ulichokiandika ni tofauti na alichokisema yeye kwa mdomo wake.

[emoji3][emoji3]
 
Huo mkataba wa Morisson aliopewa wa mil 7 hebu tuwekee hapa tuuone.

Vinginevyo nawe utakuwa na katabia cha umbea tu.

Barbra anawaumiza kwasababu mmezoea kuishi kiswahili, kuchekeana, kuvunja sheria, na kuishi kwa mazoea, na majungu.

Badilikeni hivyo vitabia vyenu vya hovyo mtamuona Barbra mtu flani poa sana, na Simba SC haondoki.
kabla ya kuuona huo mkataba, hebu twambie ni mkataba gani na wa mchezaji ganj ushawahi kuuona wazi?

Sent from my Infinix X683 using JamiiForums mobile app
 
Sikiliza Mtani.

Masikhara tuyaweke pembeni, ila kuhusu huyu mwanadada nakushauri apewe rikizo ndefu tena isiyo na maelezo ya atarudi lini. Niliwahi kuzungumza hapa jukwaani.

katika dunia ya sasa utapigiwa makofi lukuki pale utakapo jaribu kuzingatia sana usawa wa kijinsia pasipo kuweka kipaumbele malengo yako. Binafsi sina shaka na uwezo wake, lakini katika ile nafasi anahitajika kiongozi wa kiume ambaye atakuwa na busara, weledi, uzoefu na akili ya namna ya kutimiza majukumu ya msingi.

Huyu binti Barbra amejaa na wivu, kiburi, majivuni na hasira. Hizo zote ni emotional characteristics za mwanamke. Hivyo basi katika maamuzi mengi atakayo paswa kufanya hato weza kuyafanya ipasavyo kwa sababu atakuwa akisukumwa na hisia zaidi kuliko Logic.

Ona kwa mfano alivyo handle suala lenu la Morrison.

Mchezaji amefikia ukingoni mwa mkataba na klabu. Unapomuita ili kujadiri suala la mkataba mpya ni wazi kuwa kuna improvements za kimkataba atazihitaji. Kutokana na kukosa uzoefu na kuwa mtu mwenye mihemko akaamua kutengeneza mkataba ambao ndani yake umepunguza mshahara na signing fee ya mchezaji.

Mchezaji ulikuwa ukimlipa mil 11 kwa mwezi, kwenye mkataba mpya umeandika atalipwa mil 7. Iweje mchezaji mkubw akama yeye signing fee yake iwe mil 50 kweli?

Hiyo ndio sababu mchezaji akagoma kuongeza mkataba akitaka maboresho na maslahi mazuri kwasababu mpira ndio kazi yake.

Baada ya mchezaji kugoma. Barbra akaanza kumuanzishia zengwe. Mara anamwambia mchezaji hana nidhamu, mara anamwambia akae mbali na timu. Badala ya kukaa chini na kutafuta namna njema anatumia nguvu.

Sawa alikorofishana na Manara, tukasema Manara ni mkorofi.

Hivi sasa yuko na bifu na Morrison, kwa mazoea yetu tunasema bernard ni mkorofi.

Kibaya zaidi amepewa maamuzi yeye ya kupanga mshahara wa mchezaji, sakata lote hili hata MO alikuwa halifahamu vyema. Amekuja kupea habari juzi tu hapa.

Haya mambo ndio yaliyompelekea Bernard Morrison kuanza mazungumzo na Yanga SC tangu tarehe 7 May, 2022.

Hivi sasa/leo Mo amekuwa na mazungumzo na Morrison ofisini kwake kuhusu kusalia Msimbazi msimu ujao lakini anapatwa kigugumizi ni namna gani Morrison na Barbra wataishi pamoja.

NOTE:-
Benard MOrrison bado hajasaini Yanga SC ila Yanga wamekwisha muwekea mkataba mezani wenye offer nzuri aidi ya Barbra. Amepewa mpaka tarehe 10 ya mwezi wa 7, baada ya hapo Yanga SC nao watafunga mlango wao na kuangalia chaguo lingine ambalo wameliweka pending kwa sasa.

View attachment 2277551
Kipi hupandisha na kushusha thamani ya mchezaji?


Ukielewa hilo wala usingeandika hayo uliyoandika.

Suala la Mo kujadili na Morison huo ni utaratibu wao wa namna ya kuendesha mazungumzo
 
Ivi unayajua majivuno ya PEREZ wewe uto PEREZ uwa anawachana wanahabari na hapindishi maneno sasa Madam CEO aliwai kujivuna wapi??lini?? Zaidi ya kuchapa kazi tu tazama alivyoibua mjadala wa Udhamini wa GSM kwenye ligi kuu kina senzo wote walitoa jasho,,,Kesi ya Morrisom CAF na FIFA kina Injinia nusu watoe chozi...Kufukuza Virusi kama Manara,BM3 yaani kifupi anapiga kazi
 
Kwa mchezaji gani wa kugombania tatizo wa bongo limbukeni sana aende huko akakutane na ambundo waanze kukesha bar.
 
Ivi unayajua majivuno ya PEREZ wewe uto PEREZ uwa anawachana wanahabari na hapindishi maneno sasa Madam CEO aliwai kujivuna wapi??lini?? Zaidi ya kuchapa kazi tu tazama alivyoibua mjadala wa Udhamini wa GSM kwenye ligi kuu kina senzo wote walitoa jasho,,,Kesi ya Morrisom CAF na FIFA kina Injinia nusu watoe chozi...Kufukuza Virusi kama Manara,BM3 yaani kifupi anapiga kazi
Ata mm nashangaa sana nashindwa kuelewa maana ya kusema babra ana wivu ,,kivip yan ,suhala la Morrison ata kama mm ningekua kiongoz wa simba ningekua na machaguo mawili kumuacha au kupunguza baadhi ya maslai kinachopandisha maslai ya mchezaji ni kiwango sasa Morrison misimu yote miwil ana kiwango gani ch kupandisha thaman yake , tunalaumu tu kwa chuki au mapenzi mchezaji akiwa na kiwango kikubwa aboreshewe maslai ata akiwa na kiwango cha kushuka au kupanda iwe ivyo ivyo nani anaweza ,yani leo hii yule mugalu au lwanga ili abak uwaboreshee maslai ,kwa wachezaji aina ya Morrison machaguo yanakua mawil au matatu maslai yabak vile vile ,yapungue au aangalie pengine
 
Mwanamke ni mwanamke tu maamuzi ya kike kike...Simba Kwa huyu dada N0 kubwa..
wewe achana na uwezo mzuri wa kazi aliouonesha barbara Gonza!Simba msimfanye huyu dada ndiye chanzo cha kufungwa na Yanga ila jaribuni kusuka timu nzuri ili muwe wa shindani azizi wa Yanga.

tokea timu ifungwe na Yanga maneno mabaya ya majungu na fitina yanatungwa kila kukicha kumchafua Mama Gonzalel.Yanga angefungwa majuzi na simba kuingia fainali ya ASAF leo hii haya yote maneno ya kitoto yasingetokea. simba kueni na kujua hata madrid kafungwa nne bila na bacelona msimu huu lakini klabu imetulia na kuchukua ubingwa wa UEFA

. sasa na nyinyi tulieni tuu makombe yapo mengi sana mkikosa ya nyumbani hata ya CAF mna haki ya kubeba. Yanga mwakani inaingia CAF kwenda kulibeba kombe na wakibeba tuu ndoo ya CAF sisi mashabiki tutauomba uongozi uiombe serikali public holiday ili shangilia yetu iwe zaidi ya ile ya the Roco blanco(real mabrid nick name) nyie mtabaki kumchafua mama Gonzalel huku timu ikikanyaga kimba! kueni sasa yanga kila siku YASC ni daima mbele nyuma mwiko! you guys grow up, wise up, get ma point?
 
Kwa mchezaji gani wa kugombania tatizo wa bongo limbukeni sana aende huko akakutane na ambundo waanze kukesha bar.
kua umri wako vizuri la sivyo barbara ni kiongozi madhubuti jana na leo. kumbuka kusuka timu na sio kusuka matusi kwa dada yetu Gonza!
 
Mwanamke mpe kazi ya wizara ya mambo ya ndani na watoto, uku kwingine ni kuleta matatizo yasiyo na ulazima
uchungu wa goli la feisal toto usiwe nongwa kwenu kumtukana mama Gonzalel. Yanga ikiwafunga tuu kila siku lazima mufukuza kocha na kutafuta the scape goats klabuni.
 
Sikiliza Mtani.

Masikhara tuyaweke pembeni, ila kuhusu huyu mwanadada nakushauri apewe rikizo ndefu tena isiyo na maelezo ya atarudi lini. Niliwahi kuzungumza hapa jukwaani.

katika dunia ya sasa utapigiwa makofi lukuki pale utakapo jaribu kuzingatia sana usawa wa kijinsia pasipo kuweka kipaumbele malengo yako. Binafsi sina shaka na uwezo wake, lakini katika ile nafasi anahitajika kiongozi wa kiume ambaye atakuwa na busara, weledi, uzoefu na akili ya namna ya kutimiza majukumu ya msingi.

Huyu binti Barbra amejaa na wivu, kiburi, majivuni na hasira. Hizo zote ni emotional characteristics za mwanamke. Hivyo basi katika maamuzi mengi atakayo paswa kufanya hato weza kuyafanya ipasavyo kwa sababu atakuwa akisukumwa na hisia zaidi kuliko Logic.

Ona kwa mfano alivyo handle suala lenu la Morrison.

Mchezaji amefikia ukingoni mwa mkataba na klabu. Unapomuita ili kujadiri suala la mkataba mpya ni wazi kuwa kuna improvements za kimkataba atazihitaji. Kutokana na kukosa uzoefu na kuwa mtu mwenye mihemko akaamua kutengeneza mkataba ambao ndani yake umepunguza mshahara na signing fee ya mchezaji.

Mchezaji ulikuwa ukimlipa mil 11 kwa mwezi, kwenye mkataba mpya umeandika atalipwa mil 7. Iweje mchezaji mkubw akama yeye signing fee yake iwe mil 50 kweli?

Hiyo ndio sababu mchezaji akagoma kuongeza mkataba akitaka maboresho na maslahi mazuri kwasababu mpira ndio kazi yake.

Baada ya mchezaji kugoma. Barbra akaanza kumuanzishia zengwe. Mara anamwambia mchezaji hana nidhamu, mara anamwambia akae mbali na timu. Badala ya kukaa chini na kutafuta namna njema anatumia nguvu.

Sawa alikorofishana na Manara, tukasema Manara ni mkorofi.

Hivi sasa yuko na bifu na Morrison, kwa mazoea yetu tunasema bernard ni mkorofi.

Kibaya zaidi amepewa maamuzi yeye ya kupanga mshahara wa mchezaji, sakata lote hili hata MO alikuwa halifahamu vyema. Amekuja kupea habari juzi tu hapa.

Haya mambo ndio yaliyompelekea Bernard Morrison kuanza mazungumzo na Yanga SC tangu tarehe 7 May, 2022.

Hivi sasa/leo Mo amekuwa na mazungumzo na Morrison ofisini kwake kuhusu kusalia Msimbazi msimu ujao lakini anapatwa kigugumizi ni namna gani Morrison na Barbra wataishi pamoja.

NOTE:-
Benard MOrrison bado hajasaini Yanga SC ila Yanga wamekwisha muwekea mkataba mezani wenye offer nzuri aidi ya Barbra. Amepewa mpaka tarehe 10 ya mwezi wa 7, baada ya hapo Yanga SC nao watafunga mlango wao na kuangalia chaguo lingine ambalo wameliweka pending kwa sasa.

View attachment 2277551
.
FB_IMG_1611660294488.jpg
 
Back
Top Bottom