Majizzo ataja Playlist ya nyimbo zake bora mwaka 2024, Komasava namba moja Bongo

Majizzo ataja Playlist ya nyimbo zake bora mwaka 2024, Komasava namba moja Bongo

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Mmiliki na Mkurugenzi wa EFM na TVE Francis "Majizzo" Ciza ametaja Playlist ya ngoma zake 20 bora kwa mwaka 2024 na ameiweka Komasava ya Diamond namba moja na katika orodha hiyo Marioo ndio jina la msanii lililotokea mara nyingi zaidi.

Soma, Pia: Diamond Platnumz namba moja kwa kutazamwa YouTube Kenya
IMG_2158.jpeg

Kabla ya kufunga mwaka Playlist yako ni ipi??
 
ukitaka kujua kila mtu ana miziki yake ati hapo kuna miziki hata siijui..!😅
😂😂 kila mtu na vibe yake mkuu, tupe na wewe list yako tuishi nayo leo tukisubiri mwaka mpya 2025
 
😂😂 kila mtu na vibe yake mkuu, tupe na wewe list yako tuishi nayo leo tukisubiri mwaka mpya 2025
mi utanionea bure mi kwenye muziki nipo tofauti sana!, yani sieleweki naweza hata kupenda nyimbo za mwaka 2000 huko nakuziona kama zimetoka leo!.
mfano sasahivi napenda sana nyimbo za aaliyyah yule mwanadada mmarekani aliefariki kitambo!, naweza sema mwaka huu yeye ndio nimesikiliza nyimbo zake zaidi kushinda msanii yoyote kwa mwaka huu!.
wimbo kama huu nani atakuelewa kwamba ni wimbo mzuri!, lakini kaka wa watu ndo inanilaza hiyo!..🤣
tena kama hii ndo inanifanya naota kabisa!


Kwa hapa bongo labda nitoe list ya nyimbo tano kwa ngoma zilizotoka mwaka huu nazozikubali.

Mario - yule remix
Mario - hakuna matata
mapozi remix
mkuu naishia hizo kwanza mpk nikaangalizie...🤣
 
U

Utaziweza nyimbo za hawa vijana?

Yani sikuhizi hata vile viwanja classic wanapiga nyimbo za kipuuzi tu mpaka unajutia muda na hela yako
nafikiri ni akili ya mtu tu, maana mi mwenyewe kijana lkn napenda zaidi nyimbo za zamani!
 
Ngoma iliyosumbua 2024 ni moja yani utake usitake, upende usiipende utakuwa umeisikia hasa mitaa ya jiji.

DJ Mushizo Ft Jay Combat X Baddest 47 – Wivu​

 
mi utanionea bure mi kwenye muziki nipo tofauti sana!, yani sieleweki naweza hata kupenda nyimbo za mwaka 2000 huko nakuziona kama zimetoka leo!.
mfano sasahivi napenda sana nyimbo za aaliyyah yule mwanadada mmarekani aliefariki kitambo!, naweza sema mwaka huu yeye ndio nimesikiliza nyimbo zake zaidi kushinda msanii yoyote kwa mwaka huu!.
View attachment 3189361 wimbo kama huu nani atakuelewa kwamba ni wimbo mzuri!, lakini kaka wa watu ndo inanilaza hiyo!..🤣
tena kama hii ndo inanifanya naota kabisa!
View attachment 3189364

Kwa hapa bongo labda nitoe list ya nyimbo tano kwa ngoma zilizotoka mwaka huu nazozikubali.

Mario - yule remix
Mario - hakuna matata
mapozi remix
mkuu naishia hizo kwanza mpk nikaangalizie...🤣
😂 sio mbaya mkuu, hizi pia zinaturudisha kwenye kumbukizi ya miaka ya nyuma.
 
Huu mwaka msanii bora kwangu ni Mbosso, amekiwasha sana.
Mbosso anaandika na kuimba, anajua.
Yaah huyu dogo anaandika sana aiseee.
Kwa mtu anaependa kusikiliza basi mboso ni chaguo sahihi. Hapigi kelele na kurudia maneno wimbo mzima.
 
Kuna wimbo katoa msanii mkubwa WAKAZI. Ule wimbo utasumbua sana kwenye chati za kimataifa.
 
Yaah huyu dogo anaandika sana aiseee.
Kwa mtu anaependa kusikiliza basi mboso ni chaguo sahihi. Hapigi kelele na kurudia maneno wimbo mzima.
Mbosso anaandika mno, na kuimba live anajua kuliko yeyote pale Wasafi.

Itoshe kusema Mbosso ni mwanamuziki, full package.
 
Back
Top Bottom