Majukumu ya waziri mwandamizi yanahitaji chombo (ibara 100)

Majukumu ya waziri mwandamizi yanahitaji chombo (ibara 100)

ego

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2013
Posts
1,620
Reaction score
1,407
siku zote tunasema waziri mwandamizi (rasimu) waziri mkuu (katiba) atakuwa na wajibu wa kudhibiti na usimamizi wa shughuli za kila siku.

lipo tatizo la sisi kutokuwa na mfumo wa kitaifa unaoeleweka wa ni jinsi gani kiongozi huyu anaweza kutimiza majukumu yake.

ni jambo la busara sana kama tutaanzisha taasisi ya kupanga na kudhibiti uchumi hapa na hiki ndicho chombo cha kumsaidia waziri huyu kutimiza majukumu yake.

hapa tunatakiwa kuunda chombo kikubwa cha kitaifa ambacho kinapanga mipango ya uchumi na kudhibiti uchumi wetu.

waziri mkuu au waziri mwandamizi hawezi kutimiza majukumu yake kama hana chombo ambacho kinajihusisha katika sekita zote kikiangalia mwenendo wa nchi na kutoa dira ya utekelezaji wa shughuli za serikali, kufuatilia utekelezaji na kutoa maagizo.

ki msingi waziri hapa anakuwa msemaji wa chombo hiki lakini lazima kuwe na chombo kinachofanya kazi hiyo.

kuchelewa kwetu kuunda chombo hiki au kutokuunda chombo hiki kumemfanya waziri mkuu au kutamfanya waziri mwandamizi kushindwa kutimiza wajibu wake na atakuwepo tu.

kimsingi mipango ya nchi inatakiwa kuanzia katika chombo kimoja cha kitaifa ambacho kinaangalia tuna nini, kinaangalia ili tuweze kupata mafanikio ya haraka tupitie njia ipi ambayo ni fast katika kupata best result.

bila chombo hiki taifa litaendelea kubahatisha na katika kubahatisha hatuwezi kupata maendeleo.

hebu angalia mfano mdogo tu wa tatizo la foleni za dar es salaam.

hili ni tatizo ambalo linatakiwa kutatuliwa na mchumi na sio engineer.

mchumi hapa anaangalia tatizo la foleni limetokana na nini? je tuna magari mengi kuliko uwezo wetu? au tuna barabara kidogo kuliko magari tunayohitaji?

hapa yawezekana tumeshindwa kudhibiti sekita ya magari na watanzania wananunua magari mengi kuliko uchumi wa nchi unavyoweza kuhimili. kumbuka magari yanachota fedha zetu kupeleka kwa watengeneza magari na vipuri vyake, magari haya yanachota fedha zetu kupeleka kwa wachimba mafuta lakini magari haya tunayahitaji ili kutusaidia katika usafiri.

hapa tunahitaji kudhibiti magari haya kiuchumi ili tusinunue magari mengi kupita tunavyohitaji na kuathiri uchumi wetu lakini vilevile tusiwe na magari kidogo kuliko tunavyohitaji na kuathiri uchumi wetu.

hapa tunahitaji taasisi ya kukaa chini ikaangalia jiji la dar es salaam linahitaji magari ya aina gani na kwa kiwango gani ili kuondoa tatizo la usafiri.

chombo hiki kitaangalia barabara ya gongo la mboto kuja mjini mfano tukiwa na mabasi mengi ya kubeba ya kubeba abiria kuanzia 45 na kuendelea barabarani kuelekea maeneo tofauti ya jiji na magari kidogo ya binafsi ambayo yamebeba wastani wa abiria 2 je kiuchumi imekaaje kwa maana ya foleni au mda wa abiria kutoka gongo la mboto kwenda mjini, kwa maana mfumo huu una impact gani kifedha kwa maana kwa mwaka tutapoteza fedha kiasi gani kwenda kwa watengeneza magari na wazalisha mafuta.

alafu kinaangalia mfumo mwingine wa kuwa na magari madogo ya binafsi ya wastani abiria 2 mengi na mabasi ya kati na makubwa kidogo kinaangalia impact yake kiuchumi na kinaangalia scenario nyingi.

alafu kinaangalia utekelezaji wake kwa maana
kwa kuangalia kila chombo kinachohusika jinsi kinavyochangia katika sekita hiyo.

mchango wa serikali kuu na vyombo vyake kuanzia mipango, sheria za kodi, mamlaka za udhibiti na mengine, sekita binafsi.

alafu kinatoa dira ya mpango wa kukabiliana na tatizo hilo na hilo anapewa waziri mkuu na yeye sasa ndipo anaagiza wizara husika kila moja jambo la kufanya katika kutatua tatizo hilo na kuwapa time frame huku yeye akiwa amekwishapanga vipaumbele kifedha kutokana na picha ya sekita zote kitaifa inayoandaliwa na chombo hiki.

yawezekana matatizo ya sekita ya usafirishaji dar kwa sasa ni ugonjwa wa presha kiuchumi ambao unatokana na ununuzi holela wa magari ya binafsi na hivyo suluhisho ni serikali kudhibiti ununuzi wa magari ya binafsi kupitia kodi na tozo mbalimbali, kuhamasisha ununuzi wa magari ya jamii kwa kupunguza ushuru na gharama za uendeshaji.

lakini ukimueleza mhandisi au wizara ya ujenzi kutatua tatizo hilo yeye anaangalia foleni na kuona suluhisho ni kuongeza ukubwa wa barabara ili magari yapite mengi zaidi. hii yawezekana na kuwa ni sawa na kuumwa na ukaenda kwa maabara ukaambiwa tatizo una mafuta mengi mwili na ukienda kutafuta suluhisho lake kutoka kwa mwanamahesabu na sio dakitari anaweza kukushauri kuongeza uzito wa mwili ili ratio ya mafuta na mwili vikae katika uwiano mzuri kumbe ndio utakuwa unaongeza tatizo zaidi.

mfumo wa kodi unaweza kudhibiti tatizo la foleni pengine bila kuhitaji kupanua barabara. kupanua barabara ni jambo zuri lakini lazima tuelewe kuwa kuwa na wafanyakazi mfano laki tano katika jiji la dar ambao kila siku wanachoma mafuta ya 15,000 kwenda kazini na kurudi, wakitumia magari yanayohitaji mainteance ni hasara kwa taifa kuliko kama tuaweza kuwapunguza hawa na kubakiza laki moja tu na hawa laki nne wakapanda usafiri wa umma na kulipa jumla pengine 2000 tu.

tutaokoa fedha nyingi isiende kwa wazalisha mafuta, tutaondoa magari mengi barabarani hivyo barabara zetu zinaweza kutosha, tutaokoa fedha nyingi isiende kwa watengeneza magari.

kwa mfumo wetu wa sasa sioni jinsi waziri mkuu anavyoweza kudhibiti jambo hilo bali yeye atasubiri wizara ya ujenzi waseme tupanue barabara zetu, atasubiri wizara ya fedha ifanye mipango ya kupata fedha za kupanua barabara. hapa sioni waziri mkuu akidhibiti bali kusimamia yale wizara zimependekeza.

lakini ili yeye waziri mkuu aweze kudhibiti lazima tatizo hilo lianzie kwake na yeye kwa kuwa yuko katika wizara zote ndiye wa kuangalia tatizo hili tunalitatua kupitia njia au nyanja ipi na anatoa maagizo kama ni tra rekebisha mfumo wa kodi tunataka kupunguza magari ya binafsi, sumatra tunataka jiji la dar liwe na mabasi idadi kadhaa na kabla ya mtu kuagiza gari la abiria anangalia takwimu pengine ni njia gani zenye mapungufu na ni mabasi ya aina gani kama ni madogo, au makubwa au ya kati maana bila kuyadhibiti hayo pia yanaweza kununuliwa zaidi pale itakapoonekana ni biashara nzuri na hapo tunakuwa hatujafanya kitu katika fedha zinazokwenda kwa watengeneza magari.

takukuru na polisi wanaagizwa nini ili taasisi hizi ambazo zinaagizwa kudhibiti uchumi zisitumie hali ya mabadiliko yatayojitokeza ambayo kwa wananchi kabla ya kuizoe wataona kama ni crisis na inaweza kuchochea vitendo vya rushwa katika taasisi zinahusika katika mpango moja kwa moja na kuharibu mipango.

na baada ya mda anaangalia utekelezaji wa mipango.

kwa njia hii waziri mkuu kweli atakuwa anatimiza wajibu wake.

si vyema kuacha maelezo haya mafupi ya kwenye katiba kila mmoja atakayeshika madaraka atekeleze yeye anavyotaka. tutakuja kuwa na hali ya kiuchumi kama mipangilio ya miji yetu kwa maana huyu anaweza kulitia mkazo jambo hili na yule ana la kwake.

tunayo nafasi kubwa sana ya kufanya vizuri kiuchumi lakini kupitia mipango, bila ya kuweka dira hasa kwa kuunda chombo tutayumbishwa sana kwa kila serikali inayoingia inataka kufanya inavyotaka yenyewe. huyu anakuta miradi fulani ilikuwa imeanza anaitelekeza na kuanzisha ya kwake, kila mmoja anawaza sekita fulani ndio niipe kipaumbele bila wachumi wa nchi kutathmini mpango na kumueleza mweshimiwa kuwa matokeo ya mpango wako ni hivi lakini kuna mpango mwingine matokeo yake ni haya.

ni vema tuunde chombo cha kudhibiti na kusimamia uchumi kikatiba na chombo hiki ndio chombo cha kumsaidia waziri mkuu kutimiza wajibu wake kwa mujibu wa ibara ya 100 rasimu.
 
siku zote tunasema waziri mwandamizi (rasimu) waziri mkuu (katiba) atakuwa na wajibu wa kudhibiti na usimamizi wa shughuli za kila siku.

lipo tatizo la sisi kutokuwa na mfumo wa kitaifa unaoeleweka wa ni jinsi gani kiongozi huyu anaweza kutimiza majukumu yake.

ni jambo la busara sana kama tutaanzisha taasisi ya kupanga na kudhibiti uchumi hapa na hiki ndicho chombo cha kumsaidia waziri huyu kutimiza majukumu yake.

hapa tunatakiwa kuunda chombo kikubwa cha kitaifa ambacho kinapanga mipango ya uchumi na kudhibiti uchumi wetu.

waziri mkuu au waziri mwandamizi hawezi kutimiza majukumu yake kama hana chombo ambacho kinajihusisha katika sekita zote kikiangalia mwenendo wa nchi na kutoa dira ya utekelezaji wa shughuli za serikali, kufuatilia utekelezaji na kutoa maagizo.

ki msingi waziri hapa anakuwa msemaji wa chombo hiki lakini lazima kuwe na chombo kinachofanya kazi hiyo.

kuchelewa kwetu kuunda chombo hiki au kutokuunda chombo hiki kumemfanya waziri mkuu au kutamfanya waziri mwandamizi kushindwa kutimiza wajibu wake na atakuwepo tu.

kimsingi mipango ya nchi inatakiwa kuanzia katika chombo kimoja cha kitaifa ambacho kinaangalia tuna nini, kinaangalia ili tuweze kupata mafanikio ya haraka tupitie njia ipi ambayo ni fast katika kupata best result.

bila chombo hiki taifa litaendelea kubahatisha na katika kubahatisha hatuwezi kupata maendeleo.

hebu angalia mfano mdogo tu wa tatizo la foleni za dar es salaam.

hili ni tatizo ambalo linatakiwa kutatuliwa na mchumi na sio engineer.

mchumi hapa anaangalia tatizo la foleni limetokana na nini? je tuna magari mengi kuliko uwezo wetu? au tuna barabara kidogo kuliko magari tunayohitaji?

hapa yawezekana tumeshindwa kudhibiti sekita ya magari na watanzania wananunua magari mengi kuliko uchumi wa nchi unavyoweza kuhimili. kumbuka magari yanachota fedha zetu kupeleka kwa watengeneza magari na vipuri vyake, magari haya yanachota fedha zetu kupeleka kwa wachimba mafuta lakini magari haya tunayahitaji ili kutusaidia katika usafiri.

hapa tunahitaji kudhibiti magari haya kiuchumi ili tusinunue magari mengi kupita tunavyohitaji na kuathiri uchumi wetu lakini vilevile tusiwe na magari kidogo kuliko tunavyohitaji na kuathiri uchumi wetu.

hapa tunahitaji taasisi ya kukaa chini ikaangalia jiji la dar es salaam linahitaji magari ya aina gani na kwa kiwango gani ili kuondoa tatizo la usafiri.

chombo hiki kitaangalia barabara ya gongo la mboto kuja mjini mfano tukiwa na mabasi mengi ya kubeba ya kubeba abiria kuanzia 45 na kuendelea barabarani kuelekea maeneo tofauti ya jiji na magari kidogo ya binafsi ambayo yamebeba wastani wa abiria 2 je kiuchumi imekaaje kwa maana ya foleni au mda wa abiria kutoka gongo la mboto kwenda mjini, kwa maana mfumo huu una impact gani kifedha kwa maana kwa mwaka tutapoteza fedha kiasi gani kwenda kwa watengeneza magari na wazalisha mafuta.

alafu kinaangalia mfumo mwingine wa kuwa na magari madogo ya binafsi ya wastani abiria 2 mengi na mabasi ya kati na makubwa kidogo kinaangalia impact yake kiuchumi na kinaangalia scenario nyingi.

alafu kinaangalia utekelezaji wake kwa maana
kwa kuangalia kila chombo kinachohusika jinsi kinavyochangia katika sekita hiyo.

mchango wa serikali kuu na vyombo vyake kuanzia mipango, sheria za kodi, mamlaka za udhibiti na mengine, sekita binafsi.

alafu kinatoa dira ya mpango wa kukabiliana na tatizo hilo na hilo anapewa waziri mkuu na yeye sasa ndipo anaagiza wizara husika kila moja jambo la kufanya katika kutatua tatizo hilo na kuwapa time frame huku yeye akiwa amekwishapanga vipaumbele kifedha kutokana na picha ya sekita zote kitaifa inayoandaliwa na chombo hiki.

yawezekana matatizo ya sekita ya usafirishaji dar kwa sasa ni ugonjwa wa presha kiuchumi ambao unatokana na ununuzi holela wa magari ya binafsi na hivyo suluhisho ni serikali kudhibiti ununuzi wa magari ya binafsi kupitia kodi na tozo mbalimbali, kuhamasisha ununuzi wa magari ya jamii kwa kupunguza ushuru na gharama za uendeshaji.

lakini ukimueleza mhandisi au wizara ya ujenzi kutatua tatizo hilo yeye anaangalia foleni na kuona suluhisho ni kuongeza ukubwa wa barabara ili magari yapite mengi zaidi. hii yawezekana na kuwa ni sawa na kuumwa na ukaenda kwa maabara ukaambiwa tatizo una mafuta mengi mwili na ukienda kutafuta suluhisho lake kutoka kwa mwanamahesabu na sio dakitari anaweza kukushauri kuongeza uzito wa mwili ili ratio ya mafuta na mwili vikae katika uwiano mzuri kumbe ndio utakuwa unaongeza tatizo zaidi.

mfumo wa kodi unaweza kudhibiti tatizo la foleni pengine bila kuhitaji kupanua barabara. kupanua barabara ni jambo zuri lakini lazima tuelewe kuwa kuwa na wafanyakazi mfano laki tano katika jiji la dar ambao kila siku wanachoma mafuta ya 15,000 kwenda kazini na kurudi, wakitumia magari yanayohitaji mainteance ni hasara kwa taifa kuliko kama tuaweza kuwapunguza hawa na kubakiza laki moja tu na hawa laki nne wakapanda usafiri wa umma na kulipa jumla pengine 2000 tu.

tutaokoa fedha nyingi isiende kwa wazalisha mafuta, tutaondoa magari mengi barabarani hivyo barabara zetu zinaweza kutosha, tutaokoa fedha nyingi isiende kwa watengeneza magari.

kwa mfumo wetu wa sasa sioni jinsi waziri mkuu anavyoweza kudhibiti jambo hilo bali yeye atasubiri wizara ya ujenzi waseme tupanue barabara zetu, atasubiri wizara ya fedha ifanye mipango ya kupata fedha za kupanua barabara. hapa sioni waziri mkuu akidhibiti bali kusimamia yale wizara zimependekeza.

lakini ili yeye waziri mkuu aweze kudhibiti lazima tatizo hilo lianzie kwake na yeye kwa kuwa yuko katika wizara zote ndiye wa kuangalia tatizo hili tunalitatua kupitia njia au nyanja ipi na anatoa maagizo kama ni tra rekebisha mfumo wa kodi tunataka kupunguza magari ya binafsi, sumatra tunataka jiji la dar liwe na mabasi idadi kadhaa na kabla ya mtu kuagiza gari la abiria anangalia takwimu pengine ni njia gani zenye mapungufu na ni mabasi ya aina gani kama ni madogo, au makubwa au ya kati maana bila kuyadhibiti hayo pia yanaweza kununuliwa zaidi pale itakapoonekana ni biashara nzuri na hapo tunakuwa hatujafanya kitu katika fedha zinazokwenda kwa watengeneza magari.

takukuru na polisi wanaagizwa nini ili taasisi hizi ambazo zinaagizwa kudhibiti uchumi zisitumie hali ya mabadiliko yatayojitokeza ambayo kwa wananchi kabla ya kuizoe wataona kama ni crisis na inaweza kuchochea vitendo vya rushwa katika taasisi zinahusika katika mpango moja kwa moja na kuharibu mipango.

na baada ya mda anaangalia utekelezaji wa mipango.

kwa njia hii waziri mkuu kweli atakuwa anatimiza wajibu wake.

si vyema kuacha maelezo haya mafupi ya kwenye katiba kila mmoja atakayeshika madaraka atekeleze yeye anavyotaka. tutakuja kuwa na hali ya kiuchumi kama mipangilio ya miji yetu kwa maana huyu anaweza kulitia mkazo jambo hili na yule ana la kwake.

tunayo nafasi kubwa sana ya kufanya vizuri kiuchumi lakini kupitia mipango, bila ya kuweka dira hasa kwa kuunda chombo tutayumbishwa sana kwa kila serikali inayoingia inataka kufanya inavyotaka yenyewe. huyu anakuta miradi fulani ilikuwa imeanza anaitelekeza na kuanzisha ya kwake, kila mmoja anawaza sekita fulani ndio niipe kipaumbele bila wachumi wa nchi kutathmini mpango na kumueleza mweshimiwa kuwa matokeo ya mpango wako ni hivi lakini kuna mpango mwingine matokeo yake ni haya.

ni vema tuunde chombo cha kudhibiti na kusimamia uchumi kikatiba na chombo hiki ndio chombo cha kumsaidia waziri mkuu kutimiza wajibu wake kwa mujibu wa ibara ya 100 rasimu.

So what should be done?
 
ni lazima tutambue kuwa waziri mwandamizi ni nafasi ambayo inabalansi uongozi wa nchi kwa maana waziri mkuu kazi yake ni kuweka mapendekezo au mipango ya raisi katika utaalamu.

raisi yeye kama mwanasiasa yeye anatoa maagizo mbalimbali kulingana na hali ilivyo, lakini waziri mkuu anatakiwa aingize maelekezo ya raisi katika utaalamu.

lakini pia yale majukumu yaliyo ya kila siku ya serikali hahitaji kuelekezwa na raisi bali kuyafanyia kazi.

hivyo vi vema tukarekebesha katiba yetu kuelekeza serikali kuunda chombo hiki. chombo hiki kinatakiwa kuwa chombo kipana sana kwani kinatakiwa kinaweza kuwa na vitengo vya kila sekita ambavyo kila kitengo kinajikita katika sekita husika lakini lazima kuwepo unit inyounganisha vitengo vyote.

si vema kuendelea na utaratibu wetu wa sasa ambao unamfanya waziri mkuu kuwa kama kiongozi wa kuchaguliwa na wananchi ambaye ni vigumu kumbana kwa utaalamu kutokana na mapenzi ya wananchi yanaweza yasikizi vigezo vya kitaalamau.

ni lazima kila jambo ambalo waziri mkuu anaagiza au anatolea uffanuzi liwe limefanyiwa kazi na chombo hiki na kuliweka kitaalamu na yeye anaagiza mapendekezo ya chombo.

raisi kwa nafasi yake anaweza kutoa maagizo ya kisiasa lakini maagizo hayo waziri mkuu anayatoa kitaalamu.

ni lazima chombo hiki kiwe pia kinafuatilia utekelezaji wa mipango na kumpa waziri mkuu reporti ili aweze kufahamu utekelezaji wa maagizo au mipango au kujua utendaji wa baraza la mawaziri.

hivyo ni vema tuagize kikatiba serikali kuunda chombo hiki na kuelekeza ni chombo cha aina gani kiundwe.

So what should be done?
 
Nikajua anakuja na complete structure ya chombo hicho kumbe na yeye anapiga porojo humu ndani ili apate wafuasi!Maelezo marefu as if unapresent paper afu huna anayekusikiliza!
 
hoja yako inaonyesha umuhimu wa chombo hicho.

wewe kwa nini unadhani hakuna anayesikiliza?

yaani mimi niandae kila kitu unadhani katiba ni yangu?

hii ni katiba ya watanzania na kama kuna mtu anadhani kuna watu watamfanyia yeye kila kitu na yeye kukaa kuwahukumu wengine lazima tutambue hilo halikubaliki kama sitopenda kutumia lugha kali ambayo inaweza kutuvuruga na sote tusipate katiba bora.

haya ni mawazo ambayo yanaweza kutusaidia watanzania lakini kuna watu wanajua ukweli juu ya jambo hili kwa maana wamekuwa wakilifanya kwa njia nyingine hivyo ni kwetu sote kupima kama linafaa ili tupime.

cha msingi tutengeneze katiba bora bila kuangalia nani anapendekeza nini.

na mimi nadhani mwenye busara huwa hatumii lugha ya kwako kama anaona jambo linafaa au halifai bali hujadili jambo ili tupate mwelekeo.

Nikajua anakuja na complete structure ya chombo hicho kumbe na yeye anapiga porojo humu ndani ili apate wafuasi!Maelezo marefu as if unapresent paper afu huna anayekusikiliza!
 
lakini kwa maelezo zaidi ni kuwa mijadala hii ni mijadala ya kisiasa, siasa kazi yake ni kutoa dira lakini siasa ikishatoa dira utaalamu ndio unafanyia kazi mapendekezo hayo.

maelezo marefu yanayowekwa hapa ni ili kumpa picha msomaji aweze kuelewa pendekezo lakini mambo haya ni lazima yafanyike kitaalamu.

kama wazo hili lina tija ni wajibu wetu kutumia utaalamu kutengeneza complete structure.

Nikajua anakuja na complete structure ya chombo hicho kumbe na yeye anapiga porojo humu ndani ili apate wafuasi!Maelezo marefu as if unapresent paper afu huna anayekusikiliza!
 
hoja yako inaonyesha umuhimu wa chombo hicho.wewe kwa nini unadhani hakuna anayesikiliza?yaani mimi niandae kila kitu unadhani katiba ni yangu? hii ni katiba ya watanzania na kama kuna mtu anadhani kuna watu watamfanyia yeye kila kitu na yeye kukaa kuwahukumu wengine lazima tutambue hilo halikubaliki kama sitopenda kutumia lugha kali ambayo inaweza kutuvuruga na sote tusipate katiba bora.haya ni mawazo ambayo yanaweza kutusaidia watanzania lakini kuna watu wanajua ukweli juu ya jambo hili kwa maana wamekuwa wakilifanya kwa njia nyingine hivyo ni kwetu sote kupima kama linafaa ili tupime.cha msingi tutengeneze katiba bora bila kuangalia nani anapendekeza nini.na mimi nadhani mwenye busara huwa hatumii lugha ya kwako kama anaona jambo linafaa au halifai bali hujadili jambo ili tupate mwelekeo.
Ndiyo jenga hoja inayoeleweka weka wazi mfumo unaouamini/structure yake strength and weakness pia tuambie hali ilivyokua mpaka umewaza hivyo kwa kina then tuambie katiba pendekezwa kwa vifungu vyake nini kinamis ili tukuelewe acha kuogelea juu juu as if umecopy na kupaste concept ya mtu ambayo huweI kuidefend,KWenye katiba pendekezwa IBara ya 110 imeweka wazi structure na position ya Waziri Mkuu pamoja na Baraza la mawaziri sioni tatizo lolote la structure iliyowekwa.
 
umuhimu wa chombo ninachokisema nimejaribu kukuonyesha kupitia mfano wa tatizo la foleni dar.

nikakuonyesha kuna tatizo hilo sasa jiulize tunaanzia wapi kulitatua.

hili moja kwa moja linatakiwa kufanyiwa utafiti na chombo ambacho kinaangalia sekita zote.

kwa nini? ni kwa sababu linaweza kuwa tatizo la mifumo ya barabara kwa maana kuangukia wizara ya ujenzi au kuwa ni tatizo linaloangukia wizara ya fedha kwa maana ya kurekebisha viwango vya kodi na tozo ili kudhibiti magari tu.

sasa je waziri mkuu atoe maagizo yapi na kwa nani?

na ni lazima utambue kuwa utekelezaji wa mpango wa maboresho unaweza kuhitaji kuhusisha wizara au taasisi nyingine.

sasa nani anatoa picha hii kujua ni kitu gani kinahitajika kufanyika na ni kwa jinsi gani? hapa utagundua haya ndio majukumu aliyopewa waziri mkuu kikatiba.

lakini bila kuunda chombo cha kufanya kazi hiyo waziri mkuu atabaki na yeye kutoa maagizo kama raisi ya kusimama kwenye majukwaa.

na bila ya utafiti wa kiuchumi tatizo hili linaonekana kama liko wizara ya ujenzi kutokana na kugusa barabara moja kwa moja hivyo ni rahisi sana kama hatutumii utaalamu kukimbilia kupanua barabara.

hapa ni lazima kutambua kuwa taifa ni kama mwanadamu, na kama unavyoona kuna wanadamu ambao akipata fedha anakimbilia starehe kushinda baa, kununua vitu vya kifahari, lakini haweki kitu chochote cha maendeleo. baada ya miaka kadhaa anakuwa kipato chake chote kimepotelea katika hasana tu.

bila kuwa na chombo cha kuliekeza taifa kuwa kipato hiki kinachoongezeka kitumikeje ni rahisi sana kwa taifa kupotea kwa kupoteza fedha zao zote kwenye vitu vya anasa tu au fedha kupotea katika bidhaa za kutoka nje ya nchi.

ni lazima kuwe na chombo kinachofanya kazi ya kuangalia kwa mapato kidogo tuliyonayo je tuwekeze katika sekita zipi na ili tufike wapi.

hivyo hiki chombo hakina lengo la kuondoa mawaziri bali ni chombo cha kufanya kazi ya kubadili sera kuwa katika mfumo wa kitaalamu wa utekelezaji.

hiki ni chombo cha kubadili changamoto zetu kuwa katika mfumo wa kitaalamu wa utekelezaji.

hiki ni chombo ambacho kikishatoa mkakati wa utekelezaji wa jambo fulani, waziri mkuu anatoa maagizo kwa wizara na taasisi husika kulingana na mkakati wa kitaalamu ulivyo pangwa.

baada ya utekelezaji kuanza chombo hiki kinafuatilia kujua utekelezaji ukoje na kinampa waziri mkuu taarifa na yeye anafanya maamuzi kulingana na taarifa.

kimsingi chombo hiki kinamsaidia waziri mkuu kutekeleza kazi majukumu yake.

tumeona mambo mengi yanatokea katika nchi hii lakini waziri mkuu hana taarifa na mpaka jambo limeibuliwa ndio viongozi wanaunda tume kuchunguza kujua kinachoendelea.

wengine wanasema jambo lililotendwa na waziri kuwa waziri mkuu hakuhusika lakini mpaka linaibuliwa na jamii yeye yuko kimya. sasa kwa kifungu hiki cha katiba waziri mkuu anakuwa accountable kwa kila kosa linalofanyika chini yake.

lakini sasa tujiulize je mfumo wa utendaji ulivyo unampa waziri mkuu nafasi ya kudhibiti na kusimamia kila kinachofanyika?

tujiulize je tuna utaratibu gani wa ambao unatuwezesha kutambua kwa kila changamoto inayotukabili ni wapi mahali sahihi pa kuanzia kulitatua, je tuna utaratibu gani wa kutuwezesha kujua kwa changamoto zetu nyingi tulizonazo je ni changamoto gani tuanze kuzishughulikia kwa mapato yetu kidogo lakini tukichukua kila sekita husika katika kila changamoto tunayoichukua ili kile tunachokiwekeza kiwe na tija?

au kwa kifupi ni kwa jinsi gani waziri mkuu anasimamia na kudhibiti shughuli za kila siku za serikali?

Ndiyo jenga hoja inayoeleweka weka wazi mfumo unaouamini/structure yake strength and weakness pia tuambie hali ilivyokua mpaka umewaza hivyo kwa kina then tuambie katiba pendekezwa kwa vifungu vyake nini kinamis ili tukuelewe acha kuogelea juu juu as if umecopy na kupaste concept ya mtu ambayo huweI kuidefend,KWenye katiba pendekezwa IBara ya 110 imeweka wazi structure na position ya Waziri Mkuu pamoja na Baraza la mawaziri sioni tatizo lolote la structure iliyowekwa.
 
umuhimu wa chombo ninachokisema nimejaribu kukuonyesha kupitia mfano wa tatizo la foleni dar.

nikakuonyesha kuna tatizo hilo sasa jiulize tunaanzia wapi kulitatua.

hili moja kwa moja linatakiwa kufanyiwa utafiti na chombo ambacho kinaangalia sekita zote.

kwa nini? ni kwa sababu linaweza kuwa tatizo la mifumo ya barabara kwa maana kuangukia wizara ya ujenzi au kuwa ni tatizo linaloangukia wizara ya fedha kwa maana ya kurekebisha viwango vya kodi na tozo ili kudhibiti magari tu.

sasa je waziri mkuu atoe maagizo yapi na kwa nani?

na ni lazima utambue kuwa utekelezaji wa mpango wa maboresho unaweza kuhitaji kuhusisha wizara au taasisi nyingine.

sasa nani anatoa picha hii kujua ni kitu gani kinahitajika kufanyika na ni kwa jinsi gani? hapa utagundua haya ndio majukumu aliyopewa waziri mkuu kikatiba.

lakini bila kuunda chombo cha kufanya kazi hiyo waziri mkuu atabaki na yeye kutoa maagizo kama raisi ya kusimama kwenye majukwaa.

na bila ya utafiti wa kiuchumi tatizo hili linaonekana kama liko wizara ya ujenzi kutokana na kugusa barabara moja kwa moja hivyo ni rahisi sana kama hatutumii utaalamu kukimbilia kupanua barabara.

hapa ni lazima kutambua kuwa taifa ni kama mwanadamu, na kama unavyoona kuna wanadamu ambao akipata fedha anakimbilia starehe kushinda baa, kununua vitu vya kifahari, lakini haweki kitu chochote cha maendeleo. baada ya miaka kadhaa anakuwa kipato chake chote kimepotelea katika hasana tu.

bila kuwa na chombo cha kuliekeza taifa kuwa kipato hiki kinachoongezeka kitumikeje ni rahisi sana kwa taifa kupotea kwa kupoteza fedha zao zote kwenye vitu vya anasa tu au fedha kupotea katika bidhaa za kutoka nje ya nchi.

ni lazima kuwe na chombo kinachofanya kazi ya kuangalia kwa mapato kidogo tuliyonayo je tuwekeze katika sekita zipi na ili tufike wapi.

hivyo hiki chombo hakina lengo la kuondoa mawaziri bali ni chombo cha kufanya kazi ya kubadili sera kuwa katika mfumo wa kitaalamu wa utekelezaji.

hiki ni chombo cha kubadili changamoto zetu kuwa katika mfumo wa kitaalamu wa utekelezaji.

hiki ni chombo ambacho kikishatoa mkakati wa utekelezaji wa jambo fulani, waziri mkuu anatoa maagizo kwa wizara na taasisi husika kulingana na mkakati wa kitaalamu ulivyo pangwa.

baada ya utekelezaji kuanza chombo hiki kinafuatilia kujua utekelezaji ukoje na kinampa waziri mkuu taarifa na yeye anafanya maamuzi kulingana na taarifa.

kimsingi chombo hiki kinamsaidia waziri mkuu kutekeleza kazi majukumu yake.

tumeona mambo mengi yanatokea katika nchi hii lakini waziri mkuu hana taarifa na mpaka jambo limeibuliwa ndio viongozi wanaunda tume kuchunguza kujua kinachoendelea.

wengine wanasema jambo lililotendwa na waziri kuwa waziri mkuu hakuhusika lakini mpaka linaibuliwa na jamii yeye yuko kimya. sasa kwa kifungu hiki cha katiba waziri mkuu anakuwa accountable kwa kila kosa linalofanyika chini yake.

lakini sasa tujiulize je mfumo wa utendaji ulivyo unampa waziri mkuu nafasi ya kudhibiti na kusimamia kila kinachofanyika?

tujiulize je tuna utaratibu gani wa ambao unatuwezesha kutambua kwa kila changamoto inayotukabili ni wapi mahali sahihi pa kuanzia kulitatua, je tuna utaratibu gani wa kutuwezesha kujua kwa changamoto zetu nyingi tulizonazo je ni changamoto gani tuanze kuzishughulikia kwa mapato yetu kidogo lakini tukichukua kila sekita husika katika kila changamoto tunayoichukua ili kile tunachokiwekeza kiwe na tija?

au kwa kifupi ni kwa jinsi gani waziri mkuu anasimamia na kudhibiti shughuli za kila siku za serikali?

Jitahidi kusummarize your words, yanaboa sana.
 
kwangu mimi naamini elimu inapatikana kwa kusoma.

mimi nilizoea kusoma vitabu inaonekana pengine wewe ulizoea kusoma maswali na majibu.

mara nyingi mambo mageni kama haya bila kueleza ili msomaji apate picha ya kile unachokizungumza anaishia yeye kupata picha nyingine na badala ya kujadili mnabaki kubishana.

hivyo jitahidi usome maana maelezo yanafafanua hoja.

Jitahidi kusummarize your words, yanaboa sana.
 
kwangu mimi naamini elimu inapatikana kwa kusoma.

mimi nilizoea kusoma vitabu inaonekana pengine wewe ulizoea kusoma maswali na majibu.

mara nyingi mambo mageni kama haya bila kueleza ili msomaji apate picha ya kile unachokizungumza anaishia yeye kupata picha nyingine na badala ya kujadili mnabaki kubishana.

hivyo jitahidi usome maana maelezo yanafafanua hoja.
maneno mengi sio ndo mtu kuelewa,msema unazidi kumchanganya zaidi, weka kitu simpo ueleweke.
 
kila mtu ana staili yake, kumbukeni hapa tunajitolea kujenga taifa letu hivyo yeyote aliyeelewa anaruhusiwa kuchangia hakuna wa kudaiwa kuwa na kopywrite ndio achangie.

maneno mengi sio ndo mtu kuelewa,msema unazidi kumchanganya zaidi, weka kitu simpo ueleweke.
 
kila mtu ana staili yake, kumbukeni hapa tunajitolea kujenga taifa letu hivyo yeyote aliyeelewa anaruhusiwa kuchangia hakuna wa kudaiwa kuwa na kopywrite ndio achangie.

Umenena vema ngd ego, hapa tutangulize utaifa na siyo ushabiki, taifa letu litajengwa na wenye moyo ambao ni mimi na wewe na Wanzania wote. Watanzania tuache ushabiki ambao hauna manufaa kwa nchi yetu, tuzingatie msingi wa kuheshimiana. Tuendeleze tunu ya amani ya nchi yetu iliyoasisiwa na Wazee wetu J.K. Nyerere na Abeid Aman Karume.
 
wapo wanaodhani ibara ya 18 "tume ya mipango" inatoa jibu.

binafsi nadhani ni bora tukaunda chombo kilicho chini ya waziri mkuu kwa maana lengo la kukiweka chombo hiki chini ya waziri mkuu ni kukipa madaraka halisi na kukitengenezea ushirikiano na serikali. pili mjukumu ya chombo hiki na ya waziri mkuu vinarandana hivyo nivema kikaundwa chombo kilicho chini ya waziri mkuu.
 
wapo wanaodhani ibara ya 18 "tume ya mipango" inatoa jibu.

binafsi nadhani ni bora tukaunda chombo kilicho chini ya waziri mkuu kwa maana lengo la kukiweka chombo hiki chini ya waziri mkuu ni kukipa madaraka halisi na kukitengenezea ushirikiano na serikali. pili mjukumu ya chombo hiki na ya waziri mkuu vinarandana hivyo nivema kikaundwa chombo kilicho chini ya waziri mkuu.


Niambie best naona bado una moto kweli leo unaikana tume ya mipango ha ha ha sasa si ndio wataalam wenyewe hao?Ibara ya 18 inaeleza vizuri na inakupa majibu ya hoja yako ya msingi.Tume ya Mipango ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndo kitakua chombo cha juu cha kupanga na kuaimamia utekelezaji wa maendeleo ya kiuchumi na kijamii ya Taifa.

Hapo hakuna kuongeza wala kupunguza!! Mambo yote uliyoyasema ukilipendelea sana jiji la Dar es salaam yataangaliwa na hicho chombo na ukisoma kifungu cha 2 unaona nafasi ya Bunge katika kufanikisha ufanisi wa Tume hii,Bunge ni wawakilishi wa wananchi katika kuisimamia Serikali kutekeleza ahadi na majukumu yake kwa wananchi sasa Bunge litatunga sheria kwa ajili ya utekelezaji wa masharti ya ibara hiyo yapo mengi ambayo bunge litahusika katika kuisaidia Tume hii kufanya kazi zake sawasawa!naomba tuelewe pamoja kisha tupige kura kuipa ridhaa katiba inayopendekezwa!
 
katiba sio tu kutaja vitu bila kuangalia ni kwa jinsi gani vitu hivyo vinafanya kazi!

leo hii tunayo tume ya mipango lakini mimi naomba uniambie inapanga nini?

nitakupa mfano

kwa sasa tukipewa mkopo na mataifa ya nje kutekeleza miradi ya maendeleo wanatupa masharti ya kuleta makampuni ya kwao kuja kufanya kazi. mfano mradi wa upanuzi wa mtambo wa maji ruvu juu pale mlandizi na ruvu darajani wahindi wametuletea mkandarasi na mwandisi mshauri kwa ajili ya mradi huo kutokana na fedha zimetoka kwao. tukipata mikopo kutoka korea tunapewa masharti ya wao kufanya kazi hizo.

lengo hapa ni kuhakikisha fedha hizo zinarudi kwao kupitia makampuni yao ingawa ni mkopo.

hili linafanywa na mataifa hayo ni wachumi wamekaa chini wakapanga mbinu za kulinda uchumi wao.

sasa hebu angalia kwetu

tumejenga chuo kikuu cha dodoma kwa kutumia fedha ya nani?

je ni wakandarasi gani wamefanya kazi hiyo?

kimsingi kile chuo tulijenga kwa fedha zetu za ndani lakini tulitumia wakandarasi wa nje na hapa tulididimiza uchumi kulinganisha na kama tungetumia wakandarasi wa ndani.

hivi baada ya kujenga hicho chuo tulipata chuo lakini fedha iliyojenga hicho chuo tunawezakubaini leo hii asilimia kubwa kama bado tunayo kwenye mzunguko wetu wa ndani au tumeipoteza kwa makampuni ya kigeni tuliyoyatumia kuchota fedha hizo na kuzipeleka kwao.

na je tumewahi kujiuliza kama tungeweka sera ya fedha za ndani kutumia makampuni ya kizalendo fedha kiasi gani ingekuwa inabaki katika mzunguko wetu?

tunalo tatizo pengine kwetu sisi kudhani kuongeza export na kupunguza import ni katika goods na services haipo. lakini hata goods nani anaangalia kwa maana ziko wizara tofauti zinahusika.

nani mwenye jukumu la kuangalia haya na kushauri ili serikali iweke taratibu?

kimsingi mimi nakushangaa kwanza kujigamba kwamba tuna tume ya mipango kwa maana ipo kinadhalia lakini haifanyi kazi.

kutokufanya kazi kunaweza kutokana na
1. mfumo wa uongozi wa nchi kutokuwapa madaraka ya kutimiza kile wanachotakiwa kufanya.
2. yawezekana hawana utaalamu wa kufanya kile wanachotakiwa kufanya.
3 muundo wake yawezekana ni kitu tulichowahisha tu tukakipa structurte ambayo haiwezi kufanya chochote.

chombo inachokizungumza hapa mimi kwanza ni taasisi kubwa yenye wataalamu waliobobea ambao wanakaa kuangalia nchi kwa kuangalia rasilimali tulizo nazo na kupanga jinsi ya kuzitumia na kupima utekelezaji wa mipango.

hawa wataangalia kama taifa ili tupige hatua kimaendeleo tunatakiwa kufanya nini kwa kila sekita na je tuanze na lipi kulingana na bajeti yetu.

mfano wanaweza kubaini hawa kuwa ili kuondoa umasikini tanzania kwa haraka tunahitaji kuboresha kilimo na ili tuboreshe kilimo tunahitaji masoko, tunahitaji zana na pembejeo, tunahiji elimu na mengine. watakaa chini na kuangalia masoko kwa maana masoko ya nje, ya ndani, kuangalia miundo mbinu ya kufikia soko, tunahitaji pengine kuprocess mazao na mengine na wao wataangalia ni kitu gani tufanye kwa kila idara na ni taasisi gani au wizara gani inahusika na kuweka time frame ya utekelezaji.

wakimaliza kupanga wanamkabidhi waziri mkuu na yeye pengine anakwenda kujadiliana na serikali kwa utaratibu wao na kuangalia upatikanaji wa fedha za kutelekeza.

mpango huu unatekelezwa kwa waziri mkuu kutoa maagizo ya nini cha kufanya kwa kila taasisi au wizara inayohusika na mda wa kutekeleza maagizo.

lakini unapokuwa huna chombo cha kuangalia matatizo ya taifa kitaifa matokeo yake ni kuandaa mipango ambayo imejikita katika sekita ndogo na kukosa uchangiaji wa sekita nyingine hivyo kuinyima mipango mafanikio.

mfano serikali iliamua kutoa ruzuku kwenye mbole na matrekita. hili bila shaka lilikuwa na lengo la kuongeza uzalishaji lakini bila taasisi inayohusika kuangalia soko hakuna linalofanyika kwa maana ama mazao yatakuwa mengi na kuporomoka bei hivyo wakulima kukata tamaa au watakosa soko kabisa na mazao kuharibika. kilimo hakiwezi kuendelea au hakuna nayeweza kuondoa umasikini katika mazingira haya.

chombo ninachokipendekeza maana yake ni wakati wa utekelezaji huo pia kuangalia kama kinachoptekelezwa kinaendana na mpango na kama kuna matatizo yanayoibuka ambayo hatakutegemewa wanaendelea kushauri taasisi husika.

chombo hiki hakiwezi kuundwa kisiasa bali kinatakiwa kiundwe kitaalamu na kama hatuwezi basi tunaweza kuwaita wageni na kutuwekea mifumo bora ya jinsi tunavyoweza kuwa na chombo ambacho kinatathimini mambo mbalimbali na kutoa mwelekeo wa utekelezaji.

sasa tukirejea katika kuunda chombo kama tulichonacho ambacho hakiwezi kuona matatizo yanayoikabili nchi na kushauri tutokeje mimi sijui tujiiteje.

lakini hiki ndicho chombo cha kupewa bajeti kikiwa cha kwanza ili wafanye kazi na kutueleza kwa kiasi cha fedha tulicho nacho, kwa fursa tulizo nazo tufanye nini kwanza na lipi lifuate na kwa utaratibu gani.

hawa ndio waende kufanya mafunzo na ziara za maendeleo na wakija wanatupa mbinu za kuboresha maisha yetu. ukimpeleka mtu aliyepanga mipango ya kilimo sehemu yenye mafanikio anajua ni vitu gani vya kuuliza kule na akija kwetu atajua cha kuboresha lakini ukimchukua mtu tu anaenda kutalii na kuona matunda ya mwisho lakini hajui "in and out" ya mafanikio yao wala kujua tofauti ya wale na sisi na hivyo kubaini ili sisi tusonge mbele tufanye nini.


Niambie best naona bado una moto kweli leo unaikana tume ya mipango ha ha ha sasa si ndio wataalam wenyewe hao?Ibara ya 18 inaeleza vizuri na inakupa majibu ya hoja yako ya msingi.Tume ya Mipango ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndo kitakua chombo cha juu cha kupanga na kuaimamia utekelezaji wa maendeleo ya kiuchumi na kijamii ya Taifa.

Hapo hakuna kuongeza wala kupunguza!! Mambo yote uliyoyasema ukilipendelea sana jiji la Dar es salaam yataangaliwa na hicho chombo na ukisoma kifungu cha 2 unaona nafasi ya Bunge katika kufanikisha ufanisi wa Tume hii,Bunge ni wawakilishi wa wananchi katika kuisimamia Serikali kutekeleza ahadi na majukumu yake kwa wananchi sasa Bunge litatunga sheria kwa ajili ya utekelezaji wa masharti ya ibara hiyo yapo mengi ambayo bunge litahusika katika kuisaidia Tume hii kufanya kazi zake sawasawa!naomba tuelewe pamoja kisha tupige kura kuipa ridhaa katiba inayopendekezwa!
 
katiba sio tu kutaja vitu bila kuangalia ni kwa jinsi gani vitu hivyo vinafanya kazi!

leo hii tunayo tume ya mipango lakini mimi naomba uniambie inapanga nini?

nitakupa mfano

kwa sasa tukipewa mkopo na mataifa ya nje kutekeleza miradi ya maendeleo wanatupa masharti ya kuleta makampuni ya kwao kuja kufanya kazi. mfano mradi wa upanuzi wa mtambo wa maji ruvu juu pale mlandizi na ruvu darajani wahindi wametuletea mkandarasi na mwandisi mshauri kwa ajili ya mradi huo kutokana na fedha zimetoka kwao. tukipata mikopo kutoka korea tunapewa masharti ya wao kufanya kazi hizo.

lengo hapa ni kuhakikisha fedha hizo zinarudi kwao kupitia makampuni yao ingawa ni mkopo.

hili linafanywa na mataifa hayo ni wachumi wamekaa chini wakapanga mbinu za kulinda uchumi wao.

sasa hebu angalia kwetu

tumejenga chuo kikuu cha dodoma kwa kutumia fedha ya nani?

je ni wakandarasi gani wamefanya kazi hiyo?

hivi baada ya kujenga hicho chuo tulipata chuo lakini fedha iliyojenga hicho chuo tunawezakubaini leo hii asilimia kubwa kama bado tunayo kwenye mzunguko wetu wa ndani au tumeipoteza kwa makampuni ya kigeni tuliyoyatumia kuchota fedha hizo na kuzipeleka kwao.

na je tumewahi kujiuliza kama tungeweka sera ya fedha za ndani kutumia makampuni ya kizalendo fedha kiasi gani ingekuwa inabaki katika mzunguko wetu?

nani mwenye jukumu la kuangalia haya na kushauri ili serikali iweke taratibu?

kimsingi mimi nakushangaa kwanza kujigamba kwamba tuna tume ya mipango kwa maana ipo kinadhalia lakini haifanyi kazi.

kutokufanya kazi kunaweza kutokana na
1. mfumo kutokuwapa madaraka ya kutimiza kile wanachotakiwa kufanya.
2. yawezekana hawana utaalamu wa kufanya kile wanachotakiwa kufanya.

chombo inachokizungumza hapa mimi kwanza ni taasisi kubwa yenye wataalamu waliobobea ambao wanakaa kuangalia nchi kwa kuangalia rasilimali tulizo nazo na kupanga jinsi ya kuzitumia na kupima utekelezaji wa mipango.

hawa wataangalia kama taifa ili tupige hatua kimaendeleo tunatakiwa kufanya nini kwa kila sekita na je tuanze na lipi kulingana na bajeti yetu.

mfano wanaweza kubaini hawa kuwa ili kuondoa umasikini tanzania kwa haraka tunahitaji kuboresha kilimo na ili tuboreshe kilimo tunahitaji masoko, tunahitaji zana na pembejeo, tunahiji elimu na mengine. watakaa chini na kuangalia masoko kwa maana masoko ya nje, ya ndani, kuangalia miundo mbinu ya kufikia soko, tunahitaji pengine kuprocess mazao na mengine na wao wataangalia ni kitu gani tufanye kwa kila idara na ni taasisi gani au wizara gani inahusika na kuweka time frame ya utekelezaji.

wakimaliza kupanga wanamkabidhi waziri mkuu na yeye pengine anakwenda kujadiliana na serikali kwa utaratibu wao na kuangalia upatikanaji wa fedha za kutelekeza.

mpango huu unatekelezwa kwa waziri mkuu kutoa maagizo ya nini cha kufanya kwa kila taasisi au wizara inayohusika na mda wa kutekeleza maagizo.

lakini unapokuwa huna chombo cha kuangalia matatizo ya taifa kitaifa matokeo yake ni kuandaa mipango ambayo imejikita katika sekita ndogo na kukosa uchangiaji wa sekita nyingine hivyo kuinyima mipango mafanikio.

mfano serikali iliamua kutoa ruzuku kwenye mbole na matrekita. hili bila shaka lilikuwa na lengo la kuongeza uzalishaji lakini bila taasisi inayohusika kuangalia soko hakuna linalofanyika kwa maana ama mazao yatakuwa mengi na kuporomoka bei hivyo wakulima kukata tamaa au watakosa soko kabisa na mazao kuharibika. kilimo hakiwezi kuendelea au hakuna nayeweza kuondoa umasikini katika mazingira haya.

chombo ninachokipendekeza maana yake ni wakati wa utekelezaji huo pia kuangalia kama kinachoptekelezwa kinaendana na mpango na kama kuna matatizo yanayoibuka ambayo hatakutegemewa wanaendelea kushauri taasisi husika.

chombo hiki hakiwezi kuundwa kisiasa bali kinatakiwa kiundwe kitaalamu na kama hatuwezi basi tunaweza kuwaita wageni na kutuwekea mifumo bora ya jinsi tunavyoweza kuwa na chombo ambacho kinatathimini mambo mbalimbali na kutoa mwelekeo wa utekelezaji.

sasa tukirejea katika kuunda chombo kama tulichonacho ambacho hakiwezi kuona matatizo yanayoikabili nchi na kushauri tutokeje mimi sijui tujiiteje.

Nina hakika huyu ndugu hawlewi labda ni mimi tu ndo naona hivi,naona mara nyingi michango yake anarudiarudia yaleyale kujaza kurasa, ningekuwa mwalimu wake angeisoma namba huyu! Anazungukazunguka tu kupoteza muda! Nimeona mchangiaji mmoja kamwambia Katiba inayopendekezwa imeweka mfumo wa Kuwa na Tume ya Mipango ambacho ndiyo chombo cha juu kabisa cha kupanga na kusimamianutekelezaji wa maendeleo ya kiuchumi na kijamii ya taifa na Bunge litatunga sheria kukipa nguvu chombo hiki sijui hapa hajaelewa nini, napata shida na elimu yake huyu!!!!!
 
hivi wewe unajua maana ya katiba?

katiba ni sisi wananchi kuweka utaratibu wetu jinsi tunavyotaka kuishi.

na yeyote anayelitambua hilo hawezi kumwambia mtu piga ndio au hapana tu kwa maana anayepiga piga ndio au hapana kwa sababu fulani mesema huyo ni ........

katiba tunatakiwa kutunga sisi hivyo kwa yeyote anapiga kura kilingana na mtizamo wake.

kama anaona yote aliyoyataka na ambayo amebaini yanatakiwa kuwemo yamekuwemo.

kama kuna jambo lolote ambalo mtu anatamani libadilike na anaona ili kulibadilisha ni kubadili kitu fulani na tukiweka taratibu fulani kwa mfano litabadilika hapa kwenye katiba ndio mahala pake.

fanya maamuzi kulingana na lengo la kubadili maisha yetu kuwa mazuri
kuwa mtumwa wa maendeleo yetu lakini usiwe mtumwa wa kundi wala mambo yasiyo na tija kwenye jamii yetu.

Kura ya ndio tu kwa katiba inayopendekezwa
 
hivi wewe unajua maana ya katiba?

Katiba ni sisi wananchi kuweka utaratibu wetu jinsi tunavyotaka kuishi.

Na yeyote anayelitambua hilo hawezi kumwambia mtu piga ndio au hapana tu kwa maana anayepiga piga ndio au hapana kwa sababu fulani mesema huyo ni ........

Katiba tunatakiwa kutunga sisi hivyo kwa yeyote anapiga kura kilingana na mtizamo wake.

Kama anaona yote aliyoyataka na ambayo amebaini yanatakiwa kuwemo yamekuwemo.

Kama kuna jambo lolote ambalo mtu anatamani libadilike na anaona ili kulibadilisha ni kubadili kitu fulani na tukiweka taratibu fulani kwa mfano litabadilika hapa kwenye katiba ndio mahala pake.

Fanya maamuzi kulingana na lengo la kubadili maisha yetu kuwa mazuri
kuwa mtumwa wa maendeleo yetu lakini usiwe mtumwa wa kundi wala mambo yasiyo na tija kwenye jamii yetu.
wewe unamuuliza mwenzio hayo maswali eti anaiujua katiba wakati wewe mwenyewe hujawahi hata kuishika afu unakuwa mbishi kama mbogo, kaisome kwanza vizuri ndo uje kubisha kwa hoja zenye maana na sio ubishi wa kijinga usio na maana.
 
Back
Top Bottom