Pre GE2025 Makada 20 wa CHADEMA wakamatwa wakielekea kwa Mkuu wa Mkoa Mwanza kufuatilia mwenzao aliyepotea kwa siku 12

Pre GE2025 Makada 20 wa CHADEMA wakamatwa wakielekea kwa Mkuu wa Mkoa Mwanza kufuatilia mwenzao aliyepotea kwa siku 12

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Wanachama na viongozi 20 wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Kanda ya Viktoria wamekamatwa na Polisi wakiwa njiani kwenda kuonana na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Said Mtanda.

Makada hao akiwemo Katibu wa Chadema Kanda ya Viktoria, Zakaria Obadi na wenzake wamekamatwa leo Jumatano, Februari 26, 2025 nje ya ofisi za mkuu wa mkoa na kuwekwa mahabusu kwa dakika kadhaa kisha kuachiwa kwa dhamana.

Habari za kuaminika zinaeleza kuwa makada na viongozi hao walikuwa kwenye harakati za kumuona Mtanda ili kufahamu hatima ya Katibu wa Baraza la Vijana wa chama hicho (Bavicha) Mkoa wa Mwanza, Amani Manengelo aliyetoweka tangu Februari 14, 2025 akiwa wilayani Misungwi.

Akizungumzia kukamatwa kwa makada hao, Mjumbe wa Kamati Kuu Chadema, Salma Kasanzu amesema wanachama hao walikuwa sehemu ya ujumbe wa ufuatiliaji alipo Manengelo na walikwenda kumuona Mtanda, lakini wakakamatwa kabla ya kumuona bila kuelezwa sababu.

Snapinst.app_482260834_18462641290065701_5311933402763139024_n_1080.jpg
 
Wanachama na viongozi 20 wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Kanda ya Viktoria wamekamatwa na Polisi wakiwa njiani kwenda kuonana na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Said Mtanda.

Makada hao akiwemo Katibu wa Chadema Kanda ya Viktoria, Zakaria Obadi na wenzake wamekamatwa leo Jumatano, Februari 26, 2025 nje ya ofisi za mkuu wa mkoa na kuwekwa mahabusu kwa dakika kadhaa kisha kuachiwa kwa dhamana.

Habari za kuaminika zinaeleza kuwa makada na viongozi hao walikuwa kwenye harakati za kumuona Mtanda ili kufahamu hatima ya Katibu wa Baraza la Vijana wa chama hicho (Bavicha) Mkoa wa Mwanza, Amani Manengelo aliyetoweka tangu Februari 14, 2025 akiwa wilayani Misungwi.

Akizungumzia kukamatwa kwa makada hao, Mjumbe wa Kamati Kuu Chadema, Salma Kasanzu amesema wanachama hao walikuwa sehemu ya ujumbe wa ufuatiliaji alipo Manengelo na walikwenda kumuona Mtanda, lakini wakakamatwa kabla ya kumuona bila kuelezwa sababu.


"We were forced to form a Paramilitary Wing of uMkhonto we Sizwe within the ANC because the Government of Whites Minorities of South Africa was terrorising us by using the State Security Forces."
Oliver Reginald Tambo, a former President of African National Congress (ANC) from 1967 to 1993.
 
Back
Top Bottom