Pre GE2025 Makalla amkaribisha Lissu CCM, ajibu kuna nini mpaka ahamie huko?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Amos Makalla amemkaribisha Makamu Mwenyekiti wa Chadema (Bara), Tundu Lissu kujiunga na chama hicho akidai tayari chama chake kimeacha misingi yake.

Makalla ameeleza hayo Agosti 9, 2024 kwenye mkutano wa Katibu Mkuu wa CCM, Dk Emmanuel Nchimbi uliofanyika katika Wilaya ya Missenyi mkoani Kagera anakoendelea na ziara ya siku nne.

Soma Pia:
Ukaribisho huo umetolewa zikiwa zimepita siku chache baada ya Lissu kunukuliwa akisema CHADEMA si mama yake na kwamba, atakuwa tayari kukihama chama hicho endapo kitakiuka misingi yake.

Hata hivyo, alipotafutwa Lissu amesema, "Mimi nijiunge na chama chao? Yaani niende CCM kwa sababu gani au wana misingi ipi?CCM kuna nini niende kufuata? Tukajenge Taifa kwa... muulizeni Makalla anafikiria mimi nitajiunga na CCM?,’’ amehoji.

Chanzo Mwananchi digital
 
aje tu maana kuna nafasi wazi ya afisa tawala wilaya fulani inamsubiri 🐒
 
Bumbuli, Mtama, Msoga na Arusha wanasemaje
 
Mwambieni huyo guluguja Makalla kuwa ameshindwa Dulla mwenye fuko la dolari ataweza yeye?
 
Sarakasi hizi tunazozishuhudia ni maandalizi ya kisaikolojia ya Lissu. Iko siku atahama CHADE.MA.

Tayari Wenje ametangaza kugombea umakamu mwenyekiti, ukizingatia kuna mabilioni yanaweza kumiminwa na Wenje ( ambayo amepewa toka nje) kwa wajumbe wanaopiga kura na Lissu akashindwa uchaguzi unadhani atabaki CHADEMA? Au CHADEMA akitokea mtu akanwaga pesa na kuteuliwa kugombea urais mwaka 2025 unadhani Lissu atakubali na kuendelea kuwa CHADEMA?

Kauli CHADEMA soo mama yangu ipigie mstari kisha subiri.
 
Kumbe kuna vita vya nafasi au vyeo, siyo uzalendo na utetezi wa wananchi.Wanagombea fito wakati wanajenga nyumba moja.
Kama wanaokosa vyeo wanahama upinzani, kwenda chama tawala.Kuna siku utarudi mfumo wa chama kimoja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…