Pre GE2025 Makalla: Hatuhitaji mbereko yoyote Tutashida Uchaguzi kwa haki

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo Chama cha Mapinduzi (CCM), Amos Makalla amesema wamejipanga kuwafikia wananchi kupitia ziara zinazofanywa na viongozi wao ikiwa ni maandalizi kuelekea uchaguzi wa Serikali za mitaa na uchaguzi mkuu.

Makalla amesema hayo leo Jumanne Agosti 6, 2024 katika ziara ya Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Emmanuel Nchimbi mkoani Kigoma.

“Viongozi wetu wanafanya ziara, kwa maana hiyo haya ni maandalizi ya CCM kushinda uchaguzi, ni sawa na timu ya mpira, sisi tunafanya usajili timu nyingine zinazurura,”amesema Makalla.


Your browser is not able to display this video.

Your browser is not able to display this video.

 
Kwani zamani mlikua mnashinda kwa mbeleko sio?😂😂😂 mnakaribia kusema ukweli.
 
Hili nalo bumunda tu
 
Nakubaliana naye kuwa CCM tutashinda bila mbeleko.
Lakini chonde akina Makalla msimsimamishe Mama 2025.
 
#HABARI: Wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM), kutoka Chanika, Buguruni, Tandika na Ukonga, wamevamia ofisi za CCM, Mkoa wa Dar es Salaam kwa madai ya kutaka uchaguzi urudiwe baada ya kutokea fujo na wizi wa kura katika uchaguzi wa ndani uliofanyika hivi karibuni.

#ITVDigital #ITVUpdates #ITVTanzania.

#Follow RadioOneStereo
 
Sawa CPA
 
Mbona wamewaelekeza watendaji wa kata kuwanyima fomu wagombea wa upinzani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…