Pre GE2025 Makalla: Wagombea Urais Tanzania na Zanzibar kutambulishwa Februari 5

Pre GE2025 Makalla: Wagombea Urais Tanzania na Zanzibar kutambulishwa Februari 5

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Chama Cha Mapinduzi (CCM), kinatarajia kuwatambulisha kwa Wanachama Wagombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 katika maadhimisho ya miaka 48 ya Chama hicho February 05,2025, uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.

Taarifa ya kuelekea maadhimisho hayo iimetolewa na Katibu wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa,Itikadi,Uenezi na Mafunzo CPA. Amos Makalla ambapo amesema sherehe hizo zitakuwa na matukio mbalimbali ikiwemo hilo la utambulisho.

Ikumbukwe hivi karibuni Mkutano Mkuu Maalum wa Chama hicho wa January 18 na 19,2025 ulipitisha majina ya Dkt. Samia Suluhu Hassan,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa Mgombea Urais na Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi kuwa Mgombea mwenza kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Dkt. Hussein Ally Mwinyi kuwa Mgombea Urais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Soma, Pia: Wajumbe Mkutano Mkuu CCM wapitisha Rais Samia, Dkt. Mwinyi kugombea Urais 2025
 
Walianza na kusema watatoa fomu moja, Saiv hata hiyo moja hawataki kutoa.

Basi, Watafute wadhamini tu, Wajumbe walizike nalo hapana.

Kweli CCM ina wenyewe.
 
Wagombea gani tena? Na hawa ni kina nani? Au mmedata?

1738601271209.jpeg

1738601304553.jpeg
 
Ule upuuzi waliofanya Dodoma mwezi uliopita utawatafuna sana, huku Kanda ya Ziwa wanaccm wamefura sana lazima itatokea shida kubwa.JK kawaingiza chaka nene sana tena lenye miba.
 
Unajua vitu vingine inabidi mtu uwe huna akili tu ili maisha yaende. Ukitaka kutumia akili utaishia magonjwa ya moyo na sonona.

Kwenye mkutano mkuu walishateuliwa na wakatangazwa kwa wanachama na jumuia ya kitanzania yote, sifa zikamwagwa na pongezi zikatolewa sasa wanataka kuwatambulisha kiaje tena? Kuwatambulisha kwamba kuna mtu hamjui Dr Samia humu Tanzania?

Yani ndio vitu tunavipa kipaumbele kweli hivi? Of all the shit we have?
 
Sheria ya vyama vya siasa inasemaje kuhusu tarehe za kuwatambulisha wagombea
 
Unajua vitu vingine inabidi mtu uwe huna akili tu ili maisha yaende. Ukitaka kutumia akili utaishia magonjwa ya moyo na sonona.

Kwenye mkutano mkuu walishateuliwa na wakatangazwa kwa wanachama na jumuia ya kitanzania yote, sifa zikamwagwa na pongezi zikatolewa sasa wanataka kuwatambulisha kiaje tena? Kuwatambulisha kwamba kuna mtu hamjui Dr Samia humu Tanzania?

Yani ndio vitu tunavipa kipaumbele kweli hivi? Of all the shit we have?
Hawa wajinga hawana mawazo yoyote ya kutatua changamoto lukuki zinazolikabili taifa hili wao wanachowaza ni uchaguzi na wizi wa kura, ni majitu ha hovyo kabisa yaani walistahili kuishi zama za mawe.
 
Kwa nini ni wa TANZANIA na ZANZIBAR na sio TANGANYIKA na ZANZIBAR?
 
kinatarajia kuwatambulisha kwa Wanachama Wagombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025
Mla Urojo na Ubuyu ndio wagombea wetu.
 
Chama Cha Mapinduzi (CCM), kinatarajia kuwatambulisha kwa Wanachama Wagombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 katika maadhimisho ya miaka 48 ya Chama hicho February 05,2025, uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.

Taarifa ya kuelekea maadhimisho hayo iimetolewa na Katibu wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa,Itikadi,Uenezi na Mafunzo CPA. Amos Makalla ambapo amesema sherehe hizo zitakuwa na matukio mbalimbali ikiwemo hilo la utambulisho.

Ikumbukwe hivi karibuni Mkutano Mkuu Maalum wa Chama hicho wa January 18 na 19,2025 ulipitisha majina ya Dkt. Samia Suluhu Hassan,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa Mgombea Urais na Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi kuwa Mgombea mwenza kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Dkt. Hussein Ally Mwinyi kuwa Mgombea Urais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Soma, Pia: Wajumbe Mkutano Mkuu CCM wapitisha Rais Samia, Dkt. Mwinyi kugombea Urais 2025
Kinawatambulisha as if hawajulikani!!
CCM wameishiwa hoja sasa wanaleta vihoja na viroja.
 
Back
Top Bottom